United Republic of Tanzania
Parliament of Tanzania

Spika wa Bunge Mhe. Anne Makinda (Mb) anasikitika kutangaza kifo cha Mbunge anayemaliza muda wake (Jimbo la Ludewa)Mhe. Deo Filikunjombe (Mb), kilichotokea jana kwa ajali ya Ndege (Helicopter). Ajali hiyo, iliyohusisha abiria wanne akiwemo Mhe. Filikunjombe ilitokea jana Jioni tarehe 15 Oktoba, 2015 wakati Helicopter waliyokuwa wakisafiria kutokea Jijini Dar es Salaam kuelekea Jimboni kwake Ludewa kuanguka katika Hifadhi ya Selous Maeneo ya Msolwa Mkoani Morogoro