Mpambe wa Rais (ADC) Brigedia Jenerali Nyamburi Mashauri alipowasilisha Bungeni ujumbe maalum kutoka kwa Mhe. Rais kuhusu uteuzi wa Waziri Mkuu tarehe 13 Novemba, 2025. Rais wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania, Mhe. Dkt. Samia Suluhu Hassan, amemteua Dkt. Mwigulu Nchemba kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Jina la Mbunge huyo wa Iramba Magharibi limewasilishwa Bungeni kwa ajili ya Waheshimiwa Wabunge kumthibitisha kuwa Waziri Mkuu wa Jamhuri wa Muungano wa Tanzania.