Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Lameck Okambo Airo

Primary Questions
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI (K.n.y MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-
Serikali chini ya uongozi wa Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete ilitangaza Jimbo la Rorya kuwa Wilaya mpya na sasa ina miaka saba tangu kutangazwa na hitaji kubwa la kwanza ni kutekeleza ahadi ya Rais Mstaafu Mheshimiwa Jakaya Mrisho Kikwete na kurudiwa tena kuahidiwa na Mheshimiwa Rais wa Awamu ya Tano za kujenga kwa lami barabara ya kutoka Mika - Utegi - Shirati - Kirongwe yenye urefu wa kilometa 58, kwa kuzingatia umuhimu wake kwamba ni kiungo kati ya Tanzania na Kenya kupitia Rorya, itainua pato la Halmashauri kupitia ushuru wa mpakani na tarafa tatu kati ya nne kupata urahisi kuingia nchi jirani ya Kenya kwa ukaribu zaidi kuliko kutumia barabara ya kwenda Sirari:-
Je, ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa barabara hii ambayo ni muhimu kwa maendeleo ya Wilaya ya Rorya?
MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-
Usambazaji wa umeme kupitia REA ulikusudiwa kufikishwa kwenye vijiji na senta 54 kwenye Awamu ya II na ingewezesha upatikanaji wa umeme asilimia 25-30, kwani upatikanaji wa umeme kabla ya mpango huo ulikuwa ni asilimia 5 na kwa kuzingatia mahitaji makubwa ya umeme kwa maendeleo ya wananchi wa Rorya umeme wa asilimia 25 bado ni wa chini na hata hivyo bado mradi unasuasua:-
(a) Je, Serikali ina mpango gani wa kuongeza kasi ya usambazaji umeme katika Wilaya ya Rorya?
(b) Je, ni lini Mpango wa REA II utakamilika na kuanza REA III?
(c) Je, REA III ina vijiji na senta ngapi ndani ya Wilaya ya Rorya?
MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-
Wilaya ya Rorya ilianzishwa mwaka 2007, ina ukubwa wa kilometa za mraba 9,345 na idadi ya watu wapatao 400,000, lakini inakabiliwa na tatizo la uhaba wa watumishi katika Mahakama ya Mwanzo ya Kineri, Ryagoro, Obilinju na Shirati. Hadi sasa Wilaya ya Rorya inatumia Mahakama ya Wilaya ya Tarime inayosababisha kesi kuchelewa kusikilizwa kwa wakati.
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Mahakama ya Wilaya kwenye Jimbo la Rorya?
MHE. KISWAGA B. DESTERY (K.n.y. MHE. LAMECK O.
AIRO) aliuliza:-
Wananchi wa Kata ya Koryo kwa kushirikiana na Mbunge wao na wananchi wa Rorya wanaoishi Mwanza, Arusha na Dar es Salaam wamejenga wodi ya akina mama na watoto pamoja na kununua jokofu lakini mapungufu yaliyopo sasa ni Jengo la upasuaji.
Je, Serikali sasa haioni ipo haja ya kusaidia jengo hilo pamoja na vifaa vyake?
KITETO Z. KOSHUMA (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-
Wavuvi wa Wilaya ya Rorya wanaovua katika Ziwa Victoria wamekuwa wakitekwa, kunyang’anywa nyavu zao pamoja na injini za boti. Aidha, majambazi wanaofanya vitendo hivyo hutumia silaha nzito na inasemekana ni wanajeshi kutoka Uganda.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongea na Serikali ya Uganda ili kukomesha uvamizi huo?
MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) Aliuliza:-
Wakati Rais akiwa kwenye ziara Wilayani Rorya aliahidi ujenzi wa Daraja la Mto Mori linalounganisha Tarafa ya Suba Luoimbo na Nyancha, lakini kwenye bajeti ya mwaka 2016/ 2017 ujenzi wa daraja hilo haukuwepo.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kujenga daraja hilo ili kutimiza ahadi ya Mheshimiwa Rais?
MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-
Katika mpaka wa Tanzania na Kenya uliopo Wilayani Rorya, kuna Ofisi za Uhamiaji na Customs za nchi yetu zipo kwenye makontena.
Je, ni lini Serikali itajenga majengo ya kisasa kwa ajili ya ofisi katika eneo hilo?
MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-
Mheshimiwa Naibu Spika, Wilaya ya Rorya ilianzishwa mwaka 2007 na ina ukubwa wa kilometa za mraba 9,345 na idadi ya watu wapatao 400,000, lakini inakabiliwa na tatizo la uhaba wa watumishi katika Mahakama za Mwanzo za Kineri, Ryagoro, Obilinju na Shirati; hadi sasa Wilaya ya Rorya inatumia Mahakama ya Wilaya ya Tarime hali inayosababisha kesi kuchelewa kusikilizwa kwa wakati:-
Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Mahakama ya Wilaya kwenye Jimbo la Rorya?
MHE. DKT. DAMAS D. NDUMBARO (K.n.y. MHE. LAMECK AIRO) aliuliza:-
Wilaya ya Rorya iliyoanzishwa mwaka 2007 sasa ina wakazi wapatao 400,000 na ina kata 26 na vijiji takriban 87 na ina vituo vya afya 4 lakini haina Hospitali ya Wilaya na wananchi wake hulazimika kutembea umbali wa takribani kilomita 30 kufuata huduma za afya Tarime na akina mama ambao ni asilimia 52 wanahitaji huduma ya hospitali kamili:-
Je, ni lini Wilaya ya Rorya itajengewa Hospitali ya Wilaya?
MHE. ALHAJ ABDALLAH M. BULEMBO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-

Wakati wa ziara ya Kampeni za Uchaguzi Mheshimiwa Rais aliahidi kujenga daraja la kuunganisha Tarafa tatu za Luoimbo, Suba na Nyancha na tayari Halmashauri imeshapeleka makadirio Wizarani:-

Je, ni lini Serikali itatenga fedha kwa ajili ya ujenzi wa daraja hilo?
MHE. VENANCE M. MWAMOTO (K.n.y. MHE. LAMECK O. AIRO) aliuliza:-

Mheshimiwa Rais akiwa kwenye ziara ya kujinadi wakati wa kampeni Wilayani Rorya aliwaahidi wananchi wa Rorya kujenga barabara ya lami kutoka Mika-Utegi hadi Shirati;lakini hadi sasa ahadi hiyo haijatekelezwa:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutekeleza ahadi hiyo?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's