Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Vedastus Mathayo Manyinyi

Primary Questions
MHE.VEDASTUS M. MANYINYI aliuliza:-
Baada ya Serikali kutoa tamko la elimu bure wananchi wamekuwa wagumu sana kutoa michango mbalimbali ya kuboresha elimu.
Je, Serikali ina mikakati gani ya kumaliza tatizo la upungufu wa vyumba vya madarasa na vyumba vya maabara katika shule za msingi na sekondari?
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI aliuliza:-
Wenyeviti wa Mitaa, Madiwani, Wabunge na Rais huchaguliwa na watu wanaoishi katika eneo la mipaka yake na wote hawa wanafanya kazi ya kuwahudumia wananchi katika maeneo yao.
Je, Serikali imeridhika na malipo wanayopata Wenyeviti wa Mitaa pamoja na Madiwani?
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI aliuliza:-

Uvuvi haramu bado unaendelea licha ya adhabu kubwa inayotolewa kwa watu wamaojihusisha nao.

(a) Je, Serikali ina mkakati gani katika kuwasaidia wananchi wake fursa zilizopo badala ya kutoa adhabu kali zinazowaumiza?

(b) Je, Serikali inavisaidiaje vikundi vya Beach Mananagement Unit vinavyojihusisha kuona faida ya kazi wazofanya?
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI aliuliza:-

Serikali katika kuhakikisha inapata watumishi bora na wenye sifa iliamua kuwaondoa watumishi wasio na sifa pamoja na wenye vyeti feki, lakini zoezi hilo lilikumbwa na changamoto mbalimbali ambapo Afisa Utumishi aliwaondoa watumishi kwenye payroll bila sababu maalum na walipofuatilia Wizarani walirudishwa kazini:-

(a) Je, kwa nini Serikali isiunde timu maalum ili ipite kila Halmashauri kupitia taarifa juu ya zoezi hili ili haki itendeke hasa kwa wale ambao hawana uwezo wa kwenda Wizarani?

(b) Wapo watumishi ambao baada ya kuajiriwa kwa kutumia vyeti feki walijiendeleza kielimu zaidi ya Darasa la Saba na wameondolewa kwa kosa la udanganyifu wa vyeti: Je, Serikali haioni kuwa hao ni bora kuliko wale ambao hawakujiendeleza?
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI aliuliza:-

Ikiwa lengo la Serikali ni kuhakikisha inawahudumia na kutatua kero za wananchi, kero hizo zisipotatuliwa katika ngazi za Mitaa, Kata, Wilaya na Mkoa wananchi hao hulazimika kuandika na kushika mabango kila Mheshimiwa Rais anapofika majimboni ili kupaza sauti zao:-

(a) Je, ni kwa nini Viongozi wa Wilaya na Mkoa huzuia mabango hayo yasionekane na kusomwa na Mheshimiwa Rais?

(b) Je, wananchi watumie njia gani kufikisha ujumbe wao kwa Mheshimiwa Rais pale matatizo yanaposhindwa kutatuliwa katika ngazi ya chini?
MHE. BONIPHACE M. GETERE (K.n.y. MHE. VEDASTUS M. MANYINYI) aliuliza:-

Licha ya kazi nzuri ya waendesha bodaboda ya kurahisisha usafiri na kupunguza tatizo ya ajira bado ziko changamoto mbalimbali wanazosababisha kama ajali za mara kwa mara pamoja na wizi.

(a) Je, Serikali ina mkakati gani wa kupunguza tatizo hilo?

(b) Je, Serikali haioni umuhimu wa kutofautisha adhabu ya waendesha bodaboda na ile ya magari makubwa kulingana na vipato vyao?
MHE. VEDASTUS M. MATHAYO Aliuliza:-

Jeshi la Polisi linashikilia pikipiki nyingi katika Vituo vya Polisi kwa muda mrefu.

(a) Je, Serikali haioni fedha nyingi zinapotea kwa pikipiki nyingi kuchakaa zikiwa katika Vituo vya Polisi na hivyo kuleta hasara kwa Taifa?

(b) Je, kwa nini Serikali isiunde Kamati Maalum kila baada ya miaka mitatu kupitia sababu zilizosababisha pikipiki hizo zishikiliwe kwa muda mrefu?
MHE. VEDASTUS M. MANYINYI aliuliza:-

(a) Je, Serikali ina mkakati gani mahususi wa kupunguza tatizo la ukosefu wa ajira kwa vijana wanapomaliza vyuo vikuu?

(b) Je, ni kwa nini vijana hao wasitumie vyeti vyao kama dhamana kupata mikopo ili wajishughulishe na shughuli mbalimbali za kiuchumi?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's