Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Khadija Hassan Aboud

Supplementary Questions
MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Naibu Spika, namshukuru Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri. Napenda kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, baada ya ushahidi kutolewa na mhukumiwa kupata adhabu, je, kuna mikakati gani au mipango gani inayochukuliwa kuwasaidia hawa watoto hasa wa jinsia ya kiume ili kuwaepusha na unyanyapaa pia kuathirika kisaikolojia. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali namba mbili; naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri kwamba ni hatua gani zinachukuliwa kuharakisha kesi hizi za udhalilishaji wa watoto ili kuepusha kukosekana au kupotoshwa kwa makusudi ushahidi na vielelezo muhimu na pia kwa sababu mtoto huyu anakuwa mdogo kupoteza kumbukumbu zake yeye mwenyewe binafsi? (Makofi)
MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, kwanza nawapongeza Wizara kwa juhudi zao za kuwasaidia wakulima wetu. Pamoja na majibu yaliyojitosheleza suala langu, naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa wananchi wamehamasika sana kulima kilimo cha pamba, nauliza Serikali ni kwa nini haioni umuhimu wa kuanzisha soko huria la uzalishaji wa mbegu bora ili kumrahisishia na kumpa unafuu mkulima wa pamba na kuachia kampuni moja tu ya Quton ambayo inazalisha mbegu hizo.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, kutokana na majibu ya Serikali, pamba imehamasika sana na kwa wastani tani 600,000 itazalishwa na itakuwa sokoni. Je, Serikali imejipanga vipi kuhakikisha pamba yote iliyozalishwa inanunuliwa ili kuwaondolea usumbufu wakulima wa pamba?
MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante na nina swali dogo kwa Mheshimiwa Naibu Waziri.
Je, Serikali ina mpango gani wa kuanzisha katika Halmashauri zote hawa mawakala wa maji, pre-paid meter ili kuepusha wananchi kubambikiziwa bili na kuepusha wananchi au taasisi kutokulipa bili za maji? (Makofi)
MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. Namshukuru Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu mazuri yenye kutia moyo lakini naomba niulize maswali mawili ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la kwanza, kwa kuwa kuna minara imejengwa katika Kata ya Mapanda, Kijiji cha Mapanda na Kata ya Ikweha Kijiji cha Ikweha, lakini mpaka nauliza swali hili hakuna mawasiliano na Mheshimiwa Mahmoud Hassan Mgimwa ameonana na Mheshimiwa Waziri wa Mawasiliano. Je, ni lini watapata mawasiliano katika kata hizo? (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, Mheshimiwa Naibu Waziri baada ya Bunge hili yuko tayari kwenda katika Kata ya Mapanda, Ikweha, Mpangatazara, Ihanu kujionea mwenyewe matatizo ya mawasiliano yanayowapata wananchi wa maeneo hayo? Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante. (Makofi)
MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, ahsante. Nashukuru kwa majibu haya ya Serikali, pia nachukua nafasi hii kuipongeza Serikali kwa hatua mbalimbali inazochukua katika kusaidia mashirika haya ya Kiserikali na kuyawekea utaratibu mzuri. Hata hivyo, nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Taasisi Zisizo za Kiserikali, Ofisi za Mrajisi wa Mashirika hayo kati ya Zanzibar na Tanzania Bara wana ushirikiano mzuri na ushirikiano wa pamoja, lakini kuna changamoto moja. Taasisi zisizo za Kiserikali zinapotaka kufungua upande mmoja wa Muungano aidha Bara au Zanzibar taasisi hizo zinalipishwa sawasawa na taasisi za kigeni zinapotaka kufungua Mashirika ya Kiserikali hapa Zanzibar.

Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua changamoto hiyo ili mashirika yetu ya kiserikali ya Zanzibar na Bara yasiwe yanalipishwa sawasawa na taasisi ambazo zinatoka nje ya nchi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, la pili, Taasisi Zisizo za Kiserikali zimekuwa zikitoa mchango mkubwa sana katika kuinua mchango wa nchi na uchumi wa wananchi, zimekuwa zikisaidia sana kutatua baadhi ya changamoto mbalimbali za kusaidia jamii na huduma mbalimbali za kijamii. Je, Serikali inatambua vipi mchango huo wa Mashirika Yasiyo ya Kiserikali? (Makofi)
MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Watanzania tuna shauku kubwa;

Je, ni lini reli yetu ya kisasa ya mwendokasi itaanza kutoa huduma kwa wananchi kutoka Dar es Salaam hadi Dodoma?
MHE. KHADIJA HASSAN ABOUD: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru, kwanza naipongeza Serikali katika kuhamasisha kilimo na huduma za ugani suala langu Serikali kupitia Wizara ya Kilimo imenunua pikipiki kwa ajili ya Maafisa Ugani, lakini bado pikipiki hayo hayajagawiwa ili kuepusha uchakavu, ni lini Serikali itayagawa pikipiki hizo kwa walengwa ili yakafanya kazi kwa wakulima? Ahsante. (Makofi)

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's