Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Upendo Furaha Peneza

Primary Questions
MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Wananchi wa Mtaa wa Katoma, Kata ya Kalawala Wilaya ya Geita wameathirika sana na shughuli za Mgodi wa geita Gold Mine (GGM) ambapo nyumba zimepata nyufa na kuanguka kutokana na mitetemo, milipuko ya mara kwa mara inayoletwa na kelele na vumbi linaloathiri afya za wananchi wa mtaa huo pamoja na vyanzo vya maji.
Je, ni lini wananchi hao wa Katoma watapewa fidia za mali zao ili waondoke katika eneo hilo jirani kupisha shughuli za Mgodi?
MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Serikali ya Awamu ya Tano imeonesha nia ya kutaka kuongeza mapato kwa ufuatiliaji na kuondokana na ukwepaji kodi bandarini, lakini kwa miaka mingi Serikali imekuwa ikikosa mapato kwa kutoa misamaha ya kodi kwa kampuni za uwekezaji katika sekta ya madini:-
Je, Serikali inachukua hatua gani ili kuondokana na misamaha ya kodi inayotolewa kwa kampuni ya uwekezaji?
MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itatekeleza ahadi yake ya kupunguza misamaha ya kodi kufikia asilimia moja (1%) ya GDP?
MHE. RITTA E. KABATI (K.n.y MHE. UPENDO F. PENEZA) aliuliza:-
Kufuatia vifo vyenye utata vya kisiasa na vinavyohusisha vyombo vya dola, aliyekuwa Waziri Mkuu Mheshimiwa Mizengo Pinda alitoa ahadi katika Bunge la Kumi ya Serikali kuunda Mahakama ya Coroner (Coroner‟s Court) kwa ajili ya kuchunguza vifo mbalimbali vyenye utata:-
Je, Serikali iko katika hatua gani kutekeleza ahadi hiyo?
MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Je, Serikali ina mkakati gani wa kusambaza maji katika Kata za Kasamwa, Shiloleli, Bulela, Nyarugusu, Bukeli na maeneo mengine ya Wilaya ya Geita na Mkoa wa Geita kwa ujumla?
MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Tatizo la makazi duni kwa wananchi husababisha afya mbovu na hivyo kupunguza nguvu ya uzalishaji.
Je, Serikali ina mkakati gani wa kuhakikisha kuwa wananchi wanapata makazi bora?
MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Je, Serikali inatumiaje fedha za Mfuko wa Kuhimili Mabadiliko ya Tabia Nchi (Adaptation Fund) zinazotolewa kukabiliana na mabadiliko ya tabia nchi?
MHE. CECIL D. MWAMBE (K.n.y MHE. UPENDO F. PENEZA) aliuliza:-
Je, Serikali imeweka mikakati gani kuimarisha huduma za umeme, maji, afya na elimu katika maeneo ya vijijini ili kuongeza uzalishaji katika maeneo hayo na kuzuia wimbi la watu kukimbilia mijini?
MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itawapatia wachimbaji wadogo wadogo maeneo yaliyopimwa na kuwa na uwepo wa madini kama dhahabu, ikiwemo Moroko katika Mkoa wa Geita na maeneo mengine yenye madini nchini?
MHE. DKT. IMMACULATE S. SEMESI (K.n.y. MHE. UPENDO F. PENEZA) aliuliza:-

Je, katika mwaka 2016/2017 na 2017/2018 Serikali ilikusanya kiasi gani cha kodi ya 18% (VAT) kwa taulo za kike (sanitary pads) zote zilizotengenezwa nchini na zile zilizoingizwa nchini kabla ya kodi hiyo kuondolewa?
MHE. UPENDO F. PENEZA aliuliza:-

Wananchi wa Mtaa wa Mgusu wanaoishi ndani ya mipaka ya Mgodi wa Geita Gold Mine wanaathirika sana na uchafuzi wa mazingira unaotokana na taka zinazomwagwa katika maeneo karibu na wananchi.

Je, ni lini Serikali itatoa agizo kwa Geita Gold Mine kulipa wananchi fidia ili watoke katika eneo lililomilikishwa Mgodi?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's