Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Salum Mwinyi Rehani

Primary Questions
MHE. SALUM MWINYI REHANI aliuliza:-
Kamisheni ya Vyuo Vikuu Tanzania (TCU), Baraza la Elimu ya Ufundi (NACTE) na Baraza la Mitihani Tanzania (NECTA) ni Taasisi za Muungano na zina Ofisi Zanzibar.
(a) Je, kuna Wazanzibari wangapi watendaji katika taasisi hizo?
(b)Kama hakuna, je, Serikali haioni kuwa hakuna uwiano kwa vile taasisi hizo ni za Muungano na kwa nini kusiwe na watendaji wa pande zote mbili za Muungano baina ya pande mbili?
(c) Je, kuna mipango gani ya kufanya taasisi hizi kuwa na watendaji wa pande zote mbili hasa Ofisi ya Zanzibar?
MHE. SALUM MWINYI REHANI aliuliza:-
Je, ni lini Serikali itawatambua rasmi dereva bodaboda au bajaji kuwaandikia mikataba, kuwekewa akiba na kulipiwa Mifuko ya Hifadhi ya Jamii na waajiri wao kwani vijana hao wameshajiajiri kwa zaidi ya asilimia 15 - 25 kwenye kila Wilaya au Halmashauri?
MHE. SALUM MWINYI REHANI aliuliza:-
Serikali inatekeleza mradi mkubwa wa umeme wa Bwawa la Kidunda ambapo pia kutakuwa na miradi ya kilimo na ufugaji samaki.
• Je, kuna tathmini ya kitaalamu iliyofanyika ya kudhtibiti kemikali zinazotokana na utumiaji mkubwa wa dawa za kudhibiti magugu kwenye mashamba ya miwa na mpunga na utumiaji wa mbolea za SA ambazo husababisha uharibifu wa ardhi?
• Je, Serikali inaweza kuleta Bungeni ripoti ya tathmini pamoja na Environmental Impact Assessment juu ya mradi huo?
• Je, mradi wa umwagiliaji utachukua ekari ngapi na imepanga kulima nini katika mashamba hayo?
MHE. MACHANO OTHMAN SAID (K.n.y. MHE. SALUM MWINYI REHANI) aliuliza:-
Kambi za Jeshi za Ubago na Dunga zinawanyanyasa wananchi wa Shehia ya Kidimi kwa kuwataka waondoke katika maeneo hayo ambayo ni ya iliyokuwa Wizara ya Kilimo, Mifugo na Ushirika kwa zaidi ya miaka 40 wameanza kupima na kuweka bikoni:-
Je, Serikali inatoa tamko gani juu ya hali hiyo na hatma ya wananchi wanaoishi kwenye maeneo hayo?
MHE. SALUM MWINYI REHANI aliuliza:-

(a) Je, ni lini Mamlaka ya Hali ya Hewa itakuwa inatoa taarifa sahihi na za wakati kuhusiana na mabadiliko ya hali ya hewa nchini?

(b) Je, ni lini Mamlaka ya Hali ya Hewa kwa kushirikiana na Idara ya Earthy Warming watakuwa wanatoa taarifa za hali ya upatikanaji wa mvua na ukame ili kuwaepusha wakulima wengi kulima na kupata hasara kwa kukosa mvua wakati wao wanajua hali itakavyokuwa?
MHE. SALUM MWINYI REHANI Aliuliza:-

Dawa ya Sulphur ndiyo dawa ya udhibiti wa fungue (fangi) kwenye mazao ya korosho na mazao mengine, na Serikali imeunda mfumo wa kuagiza dawa hii ya kupuliza kwa njia bubu procurement; na mwaka jana baadhi ya wakulima waliathirika kwa kuchelewa na kupata dawa feki.

(a) Je, ni lini Serikali itakuwa tayari kuleta dawa mbadala ambazo ni rahisi zaidi?

(b) Je, ni lini Serikali itakaa na Vyama vya Msingi ili kupanga ratiba ya kuagiza na kuleta dawa na kupiga na pia kuzuia dawa za msimu uliopita?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's