Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Contributions by Hon. Haji Amour Haji (11 total)

Hotuba ya Mheshimiwa Rais, Dkt. John Pombe Joseph Magufuli aliyoitoa wakati wa Ufunguzi wa Bunge la Kumi na Mbili, Tarehe 13 Novemba, 2020
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwanza napenda kushukuru kupata nafasi hii ya kuja kushiriki katika Bunge letu hili Tukufu ikiwa ni mara yangu ya kwanza.

Napenda kukishukuru Chama changu Cha Mapinduzi kwa kuweza kunichagua kwa kura nyingi sana katika Jimbo langu la Pangawe, Zanzibar. Pia napenda kuishukuru familia yangu kwa kunipa ushirikiano mzuri hadi kufikia hii leo na kushinda katika Uchaguzi Mkuu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, Kisha napenda kumpongeza Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mheshimiwa Dkt. John Joseph Pombe Magufuli, hasa katika hotuba yake hii aliyoitoa mwezi wa Novemba, tarehe 13 ambayo mimi naiita ni hotuba shirikishi, ni hotuba ambayo imetupa mtazamo ambao ni mkubwa sana katika nchi yetu kwa kipindi cha miaka mitano.

Mheshimiwa Naibu Spika, tunasema kwamba hii ni hotuba ambayo inazungumzia masuala ya maono, yaani masuala ya programu ya miaka mitano kwa kipindi ambacho kimeanzia kipindi hiki, hasa ntazungumzia katika ushirikishi uliokuwa humo kwa upande wa nchi zetu mbili; Tanzania Zanzibar pamoja na Tanzania Bara, kazungumza mengi sana kiasi ambacho ametupa moyo sisi Wazanzibari ambao tumeshiriki katika Bunge letu hili Tukufu la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania.

Mheshimiwa Naibu Spika, katika hotuba hii pia, Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania alizungumza vizuri sana katika kumpa ushirikiano Rais wetu wa Zanzibar, Dkt. Hussein Ali Mwinyi, ambaye pia nampongeza kwa jitihada zake kubwa ambazo anazifanya na kwa weledi ambao ameupata kutoka katika Bunge hili na kwa fikra ambazo amezipata kwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. Nadhani kwamba huko kila mmoja anasikia kuwa kazi ambayo anaifanya Rais wetu wa Zanzibar, Dkt, Hussein Ali Mwinyi, ni nzuri sana na nampongeza. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, hotuba hii imezungumzia suala la kimuungano hasa katika masuala ya kiuchumi, ushirikiano wa uvuvi hasa katika Sekta ya Bahari Kuu ambayo ni sekta ya Muungano. Namshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa jitihada zake na ushirikiano wake mzuri na kwa kuona ule umuhimu wetu wa kuunganisha nchi zetu wa kusema kwamba atanunua meli nane ambazo nne zitakuwa kwa upande wa Zanzibar na nne zitakuwa kwa upande wa Tanzania Bara.

Mheshimiwa Naibu Spika, vilevile tumeona jitihada na tunaona umuhimu wa meli zile katika hotuba ile na kipengele kile kimezungumzia suala la ajira 30,000. Tunatumai katika ajira hizo Wazanzibari labda tutapata ajira 15,000 na upande wa Bara zitakuwa ajira 15,000, itakuwa si haba.

Mheshimiwa Naibu Spika, nina mengi hasa kuzungumzia suala la ajira. Nitazungumzia suala mtambuka la upande wa Muungano; tuna tatizo kubwa la ajira hasa ajira ambazo wakati mwingine tunazizungumzia kwamba ni ajira rasmi na kuna ajira ambazo siyo rasmi. Nadhani kwamba Waziri wa Ajira upande wa Tanzania yupo hapa; kuna suala ambalo limekuwa ni tatizo hasa linalohusiana na suala la ajira hizi za nje, employment agencies, ambazo hizi kwa upande mmoja kama tutaweza kuziwekea mkazo hasa ni ajira ambazo wakati mwingine linaweza likaleta soko kubwa, hasa kwa vijana wetu waliomaliza na hawana kazi. Kwa sababu wakati mwingine tunazungumzia suala la ajira kwamba labda watu waende kwenye kilimo, waende wapi. Ukiangalia hasa kuna fursa kubwa kwa kwa upande wa Tanzania kwa fursa zinazotokea nje ya nchi ambazo wakati mwingine zinakuwa ni ajira ambazo nazo ni rasmi lakini zinahitaji kuangaliwa ule umuhimu wake.

Mheshimiwa Naibu Spika, kwa mfano, kuna ajira ambazo zipo katika Nchi za Kiarabu kule, wakati mwingine tunakuwa na ufahamu ambao ni hasi kuziona kwamba zile ajira wakati mwingine kama ni human trafficking, lakini zipo ambazo zinakuja katika hali ya urasmi na zinakuja kwa mpangilio maalum, hasa kwa mikataba maalum na kwa muda maalum.

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kinachosikitisha ni kwamba wakati mwingine zile ajira zinakuja. Zipo ajira karibu, kwa mfano kwa upande wa Zanzibar kipindi hiki niliona zimekuja ajira kwa Tanzania karibu 1,200. Kwa kampuni moja ambayo ni Transguard ambayo iko Dubai pale, lakini utakuta kwamba Watanzania fursa ile tunashindwa kuitumia na kushindwa kwetu maana yake ni kwamba inawezekana milango ime…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

NAIBU SPIKA: Kengele ya pili imeshagonga Mheshimiwa.

MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, naomba dakika moja tu nifafanue kidogo tu.

Mheshimiwa Naibu Spika, tatizo linalokuja ni kwamba milango kwa upande wa Tanzania Bara ile milango imefungwa kwa kuwaruhusu wale vijana kwenda kufanya kazi kule nje, ile fursa ya kupewa vile vibali, lakini kwa upande wa Zanzibar ile fursa inatumika.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa namwomba Waziri mhusika kwamba hiyo fursa aitoe na tupange mipangilio mizuri itakayoweza kuwapatia ajira vijana wetu wa Tanzania kwa ujumla na zinapotokea zile fursa maana yake ziwe kwa wote.

Mheshimiwa Naibu Spika, wakati mwingine zile fursa kwa upande wa Zanzibar tunazitumia vizuri, lakini upande wa Tanzania Bara inakuwa kidogo kama kuna milango ambayo imefungwa kwa zile fursa kwa upande wa vijana wetu kwa upande wa huku. Sasa nahisi kwamba tufanye mipango mizuri kupitia Balozi zetu kuunganisha suala hili ili kwamba nayo iwe ni fursa kwa vijana wetu kupata ajira.

Mheshimiwa Naibu Spika, mwisho, kutokana na muda, naunga mkono hotuba ya Mheshimiwa Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano. Ahsante sana. (Makofi)
Hali ya Uchumi wa Taifa kwa Mwaka 2020 na Mpango wa Maendeleo wa Taifa kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 pamoja na Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwa ruhusa yako nami nisiwe mchoyo wa kushukuru, kwa kunichagua katika kuwasilisha mchango wa bajeti yetu ya Serikali, ambao ni mapendekezo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kabla ya kuchangia kwanza napenda kumpongeza pamoja na timu yake, Waziri wa Fedha na Mipango, kwa hotuba yake nzuri na mtiririko wake mzuri katika kuwasilisha katika hadhira yetu hii ya Bunge. Pia, nampongeza Rais wetu, mama Samia Suluhu Hassan, kwa kuweza kutufikisha hapa tulipo na kwa kuweza kuweka maelekezo yake mazuri sana kama ambavyo katika bajeti zetu hizi tunavyokwenda nazo. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika uchangiaji wangu, nitajaribu kugusa mambo matatu. Cha mwanzo, nitajaribu kuangalia suala la uchumi wa nchi yetu. Unajua kukua kwa uchumi maana yake wakati mwingine watu wanajaribu kutafuta, ile tafsiri ya uchumi. Kwa nini uchumi unaambiwa kwamba umekua kwa asilimia nne au asilimia ngapi. Mwananchi wa chini mara nyingi huwa hawezi kujua uchumi namna unavyokua, lakini kwa namna ambavyo maendeleo ya nchi yetu yanavyopiga hatua, hasa katika masuala ya ujenzi wa miundombinu yetu, maana yake ile ni dhahiri kwamba uchumi wa nchi yetu unakua. Kigezo cha mwanzo ni kuona ile miradi mikubwa iko katika hali ya uendelevu, kwamba, tangu ilivyoanza miradi hiyo maana yake iko katika hali ya uendelevu. Sasa uendelevu ule maana yake ni kigezo dhahiri kwamba nchi yetu ya Tanzania inakua. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala la pili, tukizungumzia suala la bajeti, bajeti yetu hii tutasema kwamba ni ya ushirikishwaji wa watu kulipa kodi bila ya hiari. Kwa nini nazungumza kwamba ni bajeti ya shirikishi ya watu kulipa kodi bila ya hiari, kutokana na kwamba kwa namna ya zile kodi zilivyowekwa. Wabunge wengi wanajaribu ku-question suala la kodi ya nyumba kwamba, labda pengine litampa mzigo mwenye nyumba au mpangaji katika nyumba. Suala lile kiukweli na kiundani kabisa maana yake ile ni dhahiri kwamba, tunashirikisha ile jamii iliyokuwepo katika makazi yetu katika nchi yetu ya Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tusijaribu kulaumu au kujaribu kulalamika kwa Sh.1,000/= ambayo inalipwa kwa kila mwezi kwamba, ikawa ni suala ambalo ni kubwa sana kwa kushirikishwa wananchi wetu kulipa katika tozo ya nyumba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine, nasema kwamba bajeti yetu ni uendelezaji wa kazi za Awamu ya Tano ambayo imeziacha. Nasema kwa mujibu wa bajeti ambayo iliyokuwepo, ni dhahiri kwamba mfumo wa bajeti uliokuwepo, haya mambo yote ambayo yameachwa, kwa upande wa Serikali ya Awamu ya Tano, maana yake ni dhahiri kwamba kodi inalenga hasa kumalizia yale yote ambayo yameachwa. Kwa imani yetu, tuna uhakika kwa uongozi tuliokuwa nao kwamba, yale yote ambayo yameachwa na Hayati Dkt. Pombe Magufuli, mambo yale yote yataweza kuendelea. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sina wasiwasi kwa mujibu wa timu tuliyokuwa nayo na kwa uongozi wetu wa mama na kwa namna ambavyo, yeye mwenyewe binafsi anavyofanya kazi katika kuishirikisha jamii. Kaanza kuishirikisha jamii ya wanawake, akaweza kuwaeleza namna ya uchumi wa nchi tunaokusudia kwenda nao. Tangu juzi tunamwona Rais wetu akiwa kule Mwanza, nako vile vile akishajihisha masuala haya haya ya ulipaji kodi. Ni dhahiri anaweka ile picha ya namna ya mfumo wa Serikali ya Awamu ya Sita namna ilivyo, leo tumemuona akiwashirikisha vijana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, akawaeleza vizuri sana kuhusu kuwaundia Mabaraza yao ya Vijana kwamba, huku upande wa Tanzania Bara hakuna Baraza la Vijana, lakini kutokana na hotuba yake ile, nasema kwamba vijana wamepata moyo mkubwa sana. Kutokana na maneno yake ni dhahiri kwamba vijana wamepata mwamko na hasa katika masuala ya hii bajeti yetu, vijana wataleta mchango mkubwa sana na wanaweza kusababisha kuleta maendeleo makubwa katika nchi yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukija suala la bajeti iliyoletwa, maana yake imekidhi mapendekezo yote yaliyokuwa yamependekezwa na Wabunge katika Bunge letu hili. Wabunge wengi walikuwa na vilio vingi kabisa, walikuwa wanalia kuhusiana na suala la TARURA na mambo mengi ambayo walikuwa wanaeleza au wanatoa vilio vyao yameweza kupatiwa muarobaini. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa nasema kwamba mama kaja, kwa ajili ya kutatua muarobaini kama lilivyo jina lake Mama Samia Suluhu kweli kaja kuleta suluhu ya uchumi wa nchi yetu. Kwa muktadha huo maana yake kitu cha mwanzo kabla ya bajeti, mama alianza kutatua tatizo la TARURA, akazungumza suala la Mfuko wa kila Jimbo kuwapatia shilingi milioni 500.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati wa kuzungumza suala hili, nadhani kwamba, nijaribu kumuuliza Waziri tu kwamba huu Mfuko ambao tayari mama kausema, kuhusiana na shilingi milioni 500 kwenye majimbo. Huu Mfuko, je, sisi wa upande wa Zanzibar unatuhusu? Najaribu kuuliza hivyo kwa sababu, kuna Mfuko ule wa Jimbo ambao unatuhusu sote, lakini sasa je, hizi shilingi milioni 500 kwa kila Jimbo kwa sababu zimezungumzwa kwa kila Jimbo, sasa je, kwa upande wa kule Tanzania Visiwani au Tanzania Zanzibar, je, watapata kiasi gani? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na hayo, nitazungumzia suala la VAT. Pia katika hili nalo nashukuru kwamba, Waziri kajaribu kuzungumiza suala vizuri sana kuhusuana na VAT kwamba, upande wa Zanzibar na kwa upande wa Tanzania Bara. Alisema kwamba, kutakuwa na ule unafuu wa kusameheana, kwamba kutakuwa hakuna ulipaji; bidhaa itakayolipiwa Zanzibar ikija Bara maana yake haitotozwa VAT. Hata hivyo, tatizo bado linabaki kwa upande wa bidhaa nyingine, hasa kwa upande wa zile bidhaa ambazo ni kubwa, kwa mfano, kama magari. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nashauri Serikali zote mbili zikae pamoja, maana yake wawe na ushuru wa aina moja, kuliko kwamba kuna bidhaa ambayo inatozwa Zanzibar, ikija huku unaambiwa kwamba ulipe different. Serikali yetu ni moja, Tanzania yetu ni moja, Watanzania ni wamoja. Kwa hivyo, tusijaribu kujenga kitu ambacho kitaleta hitilafu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala lingine kuhusiana kwa upande wa VAT, kuna suala la vitu ambavyo ni tangible na vitu ambavyo ni intangible. Tangible havina tatizo kwa sababu vinajulikana kwamba kama ni bidhaa zenye kushikika, lakini kuna bidhaa ambazo ni intangible, kama suala la mawasiliano, hili suala hili sijui tutalifanyaje katika ugawanaji wa mapato? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakumbuka kuna Mbunge wetu mmoja, aliwahi kulizungumza suala hili kwamba, Zanzibar wana asilimia 18 kwa upande wa Tanzania Bara kuna asilimia 15. Je, katika utozwaji huu ile different maana yake itakuwaje? Nadhani kwamba viongozi wote wawili kwa upande wa Zanzibar na upande wa Tanzania Bara, wangekaa pamoja kujaribu kulijadili suala hilo. Suala hili pia lipo hata kwa upande wa miamala na nadhani kwamba nalo litaweza likaja likaleta hitilafu hiyo. Kwa hivyo, nashauri Waziri suala hilo aweze kuliangalia vizuri, ili lisije kuleta hitilafu yoyote kwa pande zetu zote mbili. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho kabisa nitazungumzia suala la upande wa kilimo. Tanzania ili kuweza kukua kwa uchumi ni vizuri zaidi tukajaribu kuangalia sekta ya uchumi katika hali bora kabisa. Kilimo chetu hiki nadhani kinaweza kikakua na Serikali ina nia kabisa kabisa na ndiyo maana ikaweza kupeleka hizi fedha, kwa ajili ya kutengeneza njia au barabara vijijini kwa ajili ya kurahisisha watu kuweza kusafirisha mazao yao kwa njia ya urahisi. Hata hivyo, ni vizuri zaidi kwa upande wa kilimo tukajaribu kuangalia na miundombinu. Je, miundombinu ambayo iliyokuwepo katika sekta ya kilimo, inaweza kukidhi haja ya uchumi wetu wa Tanzania kuweza kukua? Maana yake hilo lote tujaribu kuliangalia. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, napongeza sana bajeti, nampongeza sana Mheshimiwa Rais Samia, kwa jitihada yake kubwa anayoifanya na kwa mwelekeo wote ambao anauonyesha. Kwa namna ambavyo nchi yetu ya Tanzania kama ulivyokuwa msemo wa Rais wetu wa Zanzibar kule “yajayo yanafurahisha” kwa maana hiyo tutegemee kwamba Tanzania “yajayo yatakuwa yanafurahisha”. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana na naunga mkono hoja ya bajeti yetu hii. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Hesabu zilizokaguliwa za Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Hesabu za Serikali za Mitaa zilizokaguliwa na Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021, na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kuhusu Uwekezaji wa Mitaji ya Umma kwa Mwaka wa Fedha ulioishia Tarehe 30 Juni, 2021
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, nami namshukuru Mwenyezi Mungu kwa kuweza kunipa nafasi hii. Kwanza napenda kutoa shukrani zangu za dhati nikiwa kama mjumbe niliyetoka katika Kamati ya PIC.

Mheshimiwa Spika, kuanzia juzi tumekuwa tukijadili hoja za kamati tatu, ambapo tuna hoja ya PIC, LAAC pamoja na PAC. Bahati nzuri nashukuru sana kwamba kwa kila moja amechangia au tunachangia kwa mujibu wa kuweza kuishauri Serikali; na kwa kweli tunafanya kazi ya kuishauri Serikali vizuri sana na kuweza kusema kwamba, kuishauri Serikali pamoja na kutoa mawazo ambayo kila kamati maana yake yaliyokuwa yamo.

Mheshimiwa Spika, sasa nasema kuna mambo mengi ambayo yamo katika zile ripoti, lakini mimi niweze kujielekeza zaidi katika Kamati yangu ya PIC. Kamati yetu ya PIC ni kamati ambayo ipo kama jicho la Bunge katika kusimamia uwekezaji wa mitaji ya umma. Pamoja na hayo katika uwekezaji wa mitaji ya umma suala ambalo tunalitazama, tunaangalia vitu vitatu katika uwekezaji wetu wa mitaji ya umma. Kitu cha kwanza tunachokiangalia pale ni suala la ufanisi katika mashirika yetu; tunajaribu kuangalia suala la sheria kama zinafuatwa katika hali ya utaratibu katika ile mitaji ya umma katika mashirika yetu; na vilevile tunajaribu kuangalia suala la kibiashara.

Mheshimiwa Spika, sasa katika muktadha huo kamati yetu, kupitia katika uwekezaji wetu, tuna mashirika 237 ambayo ndiyo tunayoyasimamia kupitia hazina. Sasa katika mashirika hayo 237 kuna mashirika ambayo yana hisa chache, kuna mashirika ambayo yana hisa 100 kwa 100 na Serikali na kuna mashirika kama 10 yako nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, sasa katika mashirika hayo kuna mashirika ambayo ni ya kibiashara na kuna mashirika ambayo ni ya kutoa huduma tu kama kawaida, lakini yote yanatumia fedha za Serikali. Sasa kwa muktadha huo maana yake tujaribu kuangalia suala la fedha kwa sababu, sisi tunasimamia mitaji ya umma. Tukizungumzia mitaji ya umma maana yake tunazungumzia suala la fedha, suala la mali zote ambazo zinamilikiwa na Serikali.

Mheshimiwa Spika, sasa hap ani mahali pake. Nadhani kwamba wakati wa bajeti pale tunakuwa tunasema tu fungu limepita au limekubaliwa. Na kwa kweli mafungu mengi tumeyapitisha, lakini utakuta kwamba kwa wakati huu ambapo tunaishauri Serikali, tunapokuja hapa kwa kamati zetu tatu maana yake utakuta kwamba kila mmoja anakuja kuangalia mapungufu yaliyotokana na yale mafungu. Kwa upande wa mashirika ya umma sisi tutakuwa tunaangalia suala la ufanisi, kwamba kuna ufanisi gani, una tija gani katika mashirika yetu? Tunaangalia je, sheria zilizopo maana yake zinafuatwa au hazifuatwi? Na vilevile yale mashirika kweli yanafuata taratibu za kibiashara?

Mheshimiwa Spika, na upande wa LAAC nao wataangalia upande wao kwa upande wa fedha zinazopelekwa katika taasisi za Serikali za mitaa; pamoja na PAC nao wataangalia fedha zile za umma zote kwa ujumla. Sasa leo hii tupo hapa kwa ajili ya kuishauri Serikali. Kuna ambao wanaweza kuishauri Serikali lakini wakati uleule kuna wanaoweza kuisema Serikali, kwa sababu kuna kuisemea na kuisema Serikali.

Mheshimiwa Spika, kwa nini nazungumza kwamba, kuna kuisema Serikali? Ni kwa sababu wakati mwingine kunakuwa na ule ukiukwaji wa zile sheria au taratibu zinakuwa hazikufuatwa. Pale sisi Wabunge tutakuwa badala ya kuisema Serikali maana yake tutakuwa tunaisema Serikali kwamba hatua hazifuatwi wala hazichukuliwi. Sasa kwa hali hiyo maana yake utakuta kwamba Wabunge wote kila mmoja anapokuja hapa kaja na ukali wa namna ambavyo alivyoona katika ule ufuatiliaji wetu au katika kuona kwetu katika haya mashirika maana yake hayaendi sawa.

Mheshimiwa Spika, sasa mimi nije kwa upande wa Kamati yangu ya PIC ambapo pale tumependekeza mambo 11. Moja katika mambo ambayo tumependekeza, mimi nije katika mapendekezo mawili. Pendekezo la mwanzo linahusu mchakato wa upatikanaji wa wajumbe wa bodi kwa wakati, lakini mimi pale badala ya kwamba, kwa wakati nimeingiza neno la wenye weledi. Sasa kwa nini nimezungumza hili kwa kuingiza na neno weledi? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu, wakati mwingine mashirika mengi ambayo tumeyapitia humo, maana yake kuna mashirika mpaka hii leo yana kipindi cha miaka miwili yanakuwa hayana bodi. Sasa pale tukipima ufanisi wa shirika au ufanisi wa kampuni pale maamuzi yanakuwa si sahihi na ufanisi wenyewe unakuwa si mzuri. Na hata kibiashara kama shirika lile litakuwa ni la kibiashara maana yake biashara ile itakuwa inakwenda pasipo na maamuzi yaliyokuwa sahihi. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sasa bodi zetu, kwa mujibu wa huo ushauri tulioutoa, ningependa sana kwamba, uangaliwe sana. Na ninajua kwamba, wajumbe wengi sana suala la wajumbe wa bodi wamelizungumza, kila mmoja kalizungumza kwa upande wake na kwa upana wake. Sisi kwa upande wetu tutaangalia kwamba, bodi nyingi zinapomaliza muda wake zisichukue muda, ziteuliwe bodi mpya. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, Rais wetu Mama Samia Suluhu Hassan alipoizindua hii Taarifa ya CAG alisema wazi kwamba, kama kuna tatizo la bodi basi mimi sina tatizo hilo endapo tu nitakapoletewa katika meza yangu ndani ya wiki moja nitateuwa. Hapa inaonekana wazi kwamba inawezekana tatizo likawa liko katika zile taasisi zetu kuu, ikiwa ni pamoja na Wizara, maana hapo katika utendaji na ufanisi huo inawezekana pengine kunakosekana ufanisi na ndio maana hizo taarifa haziendi kwa Rais na inasababisha hata mashirika mengi yakawa yanachelewa kuteua bodi.

Mheshimiwa Spika, sasa hoja yangu iko hapa; katika utaratibu wa kuendesha taassisi zetu hizi bodi ndiye msimamizi wa kila kitu katika yale mashirika, ikiwemo mali pamoja na rasilimali zote za shirika au kampuni. Sasa ikiwa kama bodi au pengine taasisi haina mchunga maana yake hapo kitakachokwenda ni kitu gani?

Mheshimiwa Spika, kitakachokwenda hapo ni ubadhirifu katika shirika lile, au ufanisi na tija katika shirika lile inawezekana pengine usipatikane. Kwa mfano, wakati tulipokuwa tumekaa na mashirika yetu kuna Bodi hii ya Maji ambayo imekaa zaidi ya miaka miwili ambayo tunaita kwamba ni Bodi ya Mfuko wa Maji, bodi ile ina miaka miwili, utakuta kwamba anayekaimu nafasi ile ni Katibu Mkuu. Katibu Mkuu ana muda wake si zaidi ya mwaka mmoja, lakini bado mpaka leo taasisi ile, mfuko ule, hauna bodi, sasa hilo ni tatizo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, na ninaweza kusema kwamba, wakati mwingine hii tija au ufanisi tunaoutaka katika mashirika yetu unakuwa haupatikani vile inavyopaswa. Sasa kinachotokea ni kitu gani?

Mheshimiwa Spika, badala ya kuishauri Serikali kwa Wabunge kinachofuata ni kuisema Serikali. Kwa sababu, tutakuwa sasa hatuisemei Serikali, tutakuwa sasa tunaisema Serikali kwa sababu, kila mmoja atakuwa anasema kwa mujibu wa ukali na hatua zake.

Mheshimiwa Spika, sasa nije na suala jingine ambalo katika mapendekezo tuliyopendekeza, Serikali iweke utaratibu wa kuzipatia taasisi zinazojiendesha kibiashara vibali vya kuajiri wenyewe ajira za moja kwa moja. Hilo nalo limekuwa ni tatizo; kwa sababu, uajiri wa Serikali ikiwa ni taasisi ya shirika, ikiwa ni kampuni ambayo inamilikiwa na Serikali uajiri wake, vibali vyake mpaka vitoke utumishi. Sasa, ikiwa shirika ni la kibiashara na linajiendesha vizuri, maana yake kuna haja gani mpaka kwamba vibali vile viwe na utaratibu? Pengine shirika lina mahitaji ya wafanyakazi zaidi ya 20 au 50 na uwezo wa kifedha wanao wa kuweza kuwalipa, kwa nini wanashindwa kupewa ile ruhusa ya kuweza kuajiri?

Mheshimiwa Spika, na tukikosa ufanisi huo wa wafanyakazi ambao ni rasilimali ya watu, maana yake tutakosa ufanisi wa ile kazi yenyewe, kwa sababu ufanisi wa rasilimali watu haupo. Sasa tukikosa rasilimali watu maana yake na tuna biashara na tunataka ufanisi, maana yake hapo ufanisi utakuwa haupo.

Mheshimiwa Spika, niishauri Serikali, yale mashirika au zile taasisi tunazoziona zinajiendesha kibiashara na zina uwezo wa kujilipa au kuwalipa wafanyakazi ni vyema zikapewa ruhusa ya kuweza kuajiri. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nije na suala la tatu katika mchango wangu. Wajumbe wengi hapa wamechangia na kila mmoja kachangia hasa katika hali ya ufanisi wa Serikali. Katika suala la ufanisi wa Serikali kuna suala la ufuatiliaji. Hili suala la ufuatiliaji katika hizi taasisi zetu za Serikali linakosekana. Mashirika yetu haya yanaunda mpango kazi (work plan) wa miaka mitano au miaka kumi. Pamoja na kwamba kuna cap eye ziwekwa, lakini kunakuwa hakuna ufuatiliaji. Kwa hiyo, naomba sana suala la ufuatiliaji Serikali iandae tools ambayo siyo unit, iwe ni idara ya moja kwa moja ya monitoring and evaluation kuweza kuzifuatilia taasisi zetu. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, naona unaniangalia sana; baada ya kusema hayo nasema, ahsante sana. (Makofi)
Mapendekezo ya Mpango wa Tatu wa Maendeleo wa Taifa kwa Miaka Mitano (2021/2022 – 2025/2026) na Mapendekezo ya Mpango wa Maendeleo wa Mwaka 2021/2022 pamoja na Mapendekezo ya Muongozo wa Maandalizi ya Mpango wa Bajeti ya Serikali kwa Mwaka 2021/2022
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Nami kwa niaba ya wananchi wangu wa Jimbo la Pangawe, nipo hapa kwa ajili ya kuchangia Mpango wa Taifa wa mwaka 2020/2021 pamoja na Mipango yote miwili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza, nami sina budi kuipongeza Serikali ya Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuwasilisha Mpango huu ambao ulikuja na theme ya uchumi wa viwanda kwa maendeleo ya watu. Sasa mpango huu kwa kweli nauunga mkono na kwa kweli nasema kwamba jitihada kubwa zimefanyika katika Serikali hii ya Muungano na mambo mengi ambayo nimeyaona katika Mpango uliopo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika uchumi wowote ule wa dunia kitu kikubwa ambacho unaangalia ni suala la amani. Amani yetu tuliyokuwa nayo katika nchi yetu ya Tanzania inatosheleza kuweza kufanya uchumi wa aina yoyote. Bahati nzuri katika nchi yetu ya Tanzania, kwa mujibu wa jinsi tulivyo katika maumbile yetu, maana yake tuna uwezo wa kufanya kitu chochote. Tukija katika suala la elimu, tuna uwezo wa kuwasomesha vijana wetu na kuweza kufikia katika hatua kubwa sana ya kimaendeleo katika nchi yetu ya Tanzania.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu nilichokuja nacho kwa pamoja katika ushirikishwaji wa nchi mbili kwa pamoja ni suala la utalii. Bahati nzuri nchi yetu ya Tanzania ikiwemo Tanzania Bara pamoja na Visiwani ina kitu ambacho ni cha kimaumbile ambacho tukija katika suala la kiutalii, tuna uwezo wa kuziunganisha nchi hizi mbili zote tukasema kwamba tuwe na utalii wa pamoja ambao ni kwa maendeleo ya nchi zote mbili. Kwa sababu kwa maumbile ya nchi yetu, kwa upande wa Bara tuna mbuga ambazo tunaweza tukazitangaza kwa pamoja na zikaleta matunda kwa ajili ya maendeleo ya watu wote. Kwa upande wa visiwani kule, tuna utalii unaotokana na fukwe pamoja na bahari tuliyokua nayo, tukizishirikisha nchi hizi, maana yake kwa Tanzania tutaleta uchumi ambao ni endelevu na mkubwa sana. Vilevile kwa kufanya hivyo tutakuwa tumeunga mkono ile azma ya Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar katika ule uchumi wa bluu ambapo ndiyo theme ambayo kwa sasa hivi inazungumzwa. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nitoe rai kwamba kuna vitu vitakuwa vinaonekana kwamba siyo shirikishi, lakini kimaumbile yake na kwa mujibu wa nchi yetu ilivyo, hivi ni vitu ambavyo ni shirikishi. Kama tutaweza kuunganisha utalii wa Tanzania ukawa ni utalii tunaoutangaza kwa pamoja, nadhani tunaweza tukafanya kitu ambacho ni kikubwa sana kwa mujibu wa maumbile ya nchi yetu ambayo tunayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kutoa rai katika Mpango huu, pamoja na kwamba yamezungumzwa mengi; kulizungumzwa suala la utalii hasa kwa upande wa vivutio vya mbuga, ila mimi napenda zaidi tukauzungumzia katika utalii wa fukwe, tukaipa nguvu na Serikali ya Mapinduzi ya Zanzibar, kwa kuichanganya ili tuwe na utalii wa pamoja. Pato litakaloweza kupatikana maana yake litaweza kuleta tija kwa nchi zetu zote mbili. Hii itaweza kufanikisha ule umoja wetu ambao tumekuwa nao katika nchi zetu kuweza kuwa shirikishi hasa katika maendeleo ya pamoja. Tanzania ni moja, watu wa Tanzania ni wamoja. Hiki siyo kitu cha ubishi. Maendeleo yoyote yale ambayo yataweza kufanyika kwa upande wa Bara, ikiwa ni kilimo maana yake faida itakuwa ni ya kwetu sote (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, naunga mkono Mpango wa Maendeleo, ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana kwa ruhusa yako nami nichangie Katika Wizara ya Elimu. Kwanza namshukuru Rais wetu wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania kwa kuweza kuondosha ile tozo ya asilimia sita katika mkopo wa elimu ya juu.

La pili nije katika mchanganuo wa hoja zetu ambazo kila mmoja katika kusimama kwetu hapa kwa mujibu wa Wabunge wengi wanacholilia ni vitu viwili. Kwanza, wanalilia mfumo wa elimu ambao tulokuwa nao na la pili wengi wao wanazungumzia suala la curriculum.

Mheshimiwa Naibu Spika, nadhani nije kwa upande wa kuangalia mfumo wa elimu. Mfumo wa elimu kwa upande wa Tanzania, mie nimetokea upande wa Tanzania Zanzibar. Kule Zanzibar zamani tulikuwa tumeanzia ile base, tulikuwa tuna kitu ambacho tunakiita uzalishaji mali, ambapo kwa zamani uzalishaji mali maana yake ilikuwa imeanzia kuanzia standard one hadi standard seven, maana yake tunajifunza masuala ya elimu ya vitendo kama kulima pamoja kufuma na mambo mengine.

Mheshimiwa Naibu Spika, kutokana na kukua kwa leo, kwa sababu tuna uleo, maana yake tunasema kwamba tuna elimu ya ujasiriamali. Sasa katika vitu viwili hivyo maana yake nilikuwa najiuliza huu uzalishaji mali na ujasiriamali sijui tofauti yake ipo wapi. Kikubwa zaidi nijaribu kuzungumza kwamba, ningekuwa naulizwa, ningesema kwamba, tungekuwa tunaanza na ile elimu ya uzalishaji mali kuanzia ile standard one au kuanzia darasa la chini huku maana yake kwenda juu ili kumkuza mtoto katika misingi ya kujua ujuzi. Bila ya hivyo, kwa kusema kwamba tusubiri tu wanafunzi watakaomaliza katika elimu za juu au kuanzia kumaliza darasa la saba wajiunge katika mafunzo ya ufundi maana yake pale tutakuwa kuna kitu tunakipoteza.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa ushauri wangu kwa Wizara ya Elimu ni kwamba haya mafunzo ya ufundi hasa ambayo kwa huku tunaita ni mafunzo ya ufundi, tungeanzia huku kwenye standard one tukaanza na huo uzalishaji mali. Tukizungumzia suala la uzalishaji mali maana yake yule mwanafunzi unaanza kumjenga namna ya kuanza kujua kama ni kulima anajua nini maana ya kulima; kama ni kufuma, anaanza kujua nini maana ya kufuma. Sasa tunapokuja katika hatua ya juu, hapo ndio tunakuja katika suala la entrepreneurship, suala la ujasiriamali.

Mheshimiwa Naibu Spika, ningeomba kwa upande wa Wizara ya Elimu, suala hilo lazima wajaribu kuliangalia, mbali na mitaala yetu ambayo tunayo hapa Tanzania, kwa sababu kila mmoja maana yake analaumu mtaala, lakini suala la mitaala hili linakuja kutokana na mfumo wetu na namna ambavyo watendaji wetu wanavyohisi, kwa sababu Tanzania tuna mfumo ule wa kwamba kila mmoja anapokwenda katika nchi fulani kwenda kusoma anarudi na mfumo wake. Anayekwenda China akirudi akija Wizara ya Elimu atakuja na mfumo wa Kichina; anayekwenda Japani atakuja na mfumo wa Kijapani; na anayekwenda Marekani atakuja na mfumo wa Kimarekani.

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa bado sisi wenyewe hatujajijua hasa tunachokitaka ni kipi katika mfumo, kama Watanzania ukilinganisha na tamaduni zetu pamoja na silka zetu. Bila kujua hilo maana yake itakuwa ni vigumu sana na kila siku tutasema mtaala sio au tunakokwenda siko, lakini kitu muhimu zaidi, tunapotengeneza hii mitaala yetu, kitu cha msingi tujaribu kuangalia tamaduni zetu zinatuelekeza wapi na mazingira yetu yanatuelekeza wapi.

Mheshimiwa Naibu Spika, nikizungumzia suala la mazingira, Tanzania ina mikoa mingi, kila eneo lina vitu vyake katika masuala ya uzalishaji. Kuna mikoa ambayo inazalisha sana katika kilimo, kuna mikoa ni madini, kuna mikoa ni mambo mengine, maana yake kila mkoa una sifa ya aina yake. Nadhani kwamba tungejaribu kuangalia kuangalia elimu kwa kutazama hasa mifumo ya mikoa pamoja na uzalishaji wao. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, pale zamani wakati ule ambapo sisi tupo kwa sababu kwa upande wa kule Zanzibar unapoanza primary school, unapokwenda sekondari kulikuwa kuna ile kwamba mtu anapokuja kufauli kutoka darasa la sita au darasa la nane, kwa sababu kulikuwa kuna darasa la nane kwenda la tisa kulikuwa kuna fani maalum ambayo mwanafunzi yule anatoka pale kuelekea katika ile fani. Kwa mfano tuwe na wanafunzi ambao watakwenda kusomea kilimo tangu sekondari, tuwe na wanafunzi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana na naomba kuunga mkono hoja. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante sana. Kwa ruhusa yako nami nawashukuru watu wote wa Wizara ya Utalii kwa ujumla. Mimi sitakuwa na maelezo mengi ya kuchangia hasa kwenye mambo ya Maliasili nitagusa kwenye masuala ya Utalii. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, katika utalii zaidi nizungumzie mambo matatu au manne. Kwanza tufahamu wazi kwamba utalii ni biashara, utalii ni huduma, utalii ni miundombinu. Sasa wakati mwingine, wakati wa hoja hapa nilikuwa najaribu kusikiliza hoja zote hizi za Wabunge wote ambao wanaozungumza, nikaona kwamba kuna haja ya Wizara yenyewe maana yake kuwa na mdahalo maalum utakaowahusisha Wabunge pamoja na wataalam wa utalii kujadili suala la mfumo wa utalii wetu Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, nasema hivi kutokana na ile michango mingi ambayo imetolewa ambapo kila mmoja kajaribu kuzungumzia upande wake hasa unaouzungumzia suala la utalii, kuna wale watu waliozungumza kwa kutoa mifano mbalimbali katika nchi tofauti ambazo wameshabihisha Misri, South Africa pamoja na nchi zote zilizokuwa na utalii wa hali ya juu. Tufahamu wazi kwamba nchi hizo zote hizo ambazo zimezungumzwa kwa mifano, tukiangalia ile nature ya zile nchi maana yake kunakuwa na identification ya kitu wanachokitangazia hasa katika nchi zao. Kwa mfano kama nchi ya Misri, ukiangalia hasa kivutio chao kikubwa maana yake pale watakuwa wanazungumzia suala la pyramid. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, tukizungumzia suala la South Africa, utalii wao mkubwa maana yake unategemea kumbi za mikutano. Sasa sisi Tanzania maana yake tujaribu kuangalia kwamba identity ya Tanzania yetu hasa ni kitu gani? Maana yake ni kitu ambcho cha kuweza kukitizama kwamba, sisi Tanzania tunataka kuingia katika suala la utalii au tuko katika suala la utalii ambao ni biashara, ambao ni ajira kwa Watanzania, je sisi hasa identity yetu kuhusiana na utalii hasa ni kitu gani? Utakuta kila mmoja anazungumzia suala la vivutio mbalimbali, kwamba kuna kuna kivutio cha Mlima Kilimanjaro, kuna kivutio cha wanyama, kuna kivutio cha utamaduni, lakini kuna vivutio vingine tunaviita kwamba ni alternative katika suala la utalii. Sasa hapa tunatakiwa tuwe na utalii ule ambao ni identity kwa nchi yetu. Katika nchi yetu ukijaribu kutazama hasa sisi kwa Tanzania kipaumbele chetu hasa kwenye utalii ni kitu gani. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kitu kingine ambacho nijaribu kuishauri Wizara ni kwamba, wakati mwingine utalii kama ulivyo katika suala la mzunguko wake, utalii ndiyo kichwa ambacho nitasema kwamba kwa Wizara kinachoweza kuleta ile biashara yenyewe na kwa nini nazungumza hivyo? Nasema hivyo kwa sababu utalii wenyewe ndiyo uliosababisha vichochezi vya hizi maliasili maana yake kuweza kutambulika. Sasa bila ya utalii maana yake hivi vichochezi vyote, vivutio vyote hivi vya maliasili maana yake visingeweza kufahamika. Sasa ukiangalia kutokana na mfumo wetu wa Wizara ya Maliasili na Utalii maana yake maliasili imekuja juu sana ambapo ningetegemea sana utalii uje juu, ikisha maliasili ndio iwe ndani ya utalii, lakini sasa sisi tuko katika hali ambayo ni kinyume. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, kingine tujaribu kuangalia suala la utalii; ukiangalia kwenye bajeti zetu hizo tumejaribu kugusa sana masuala ya international tourism, lakini suala la domestic hatukuligusa hata kidogo. Suala la domestic ambalo nalo lina umuhimu wake, lakini katika domestic nako tunahitaji tufanye kazi kubwa sana. Ili tuwe na domestic, wakati mwingine, pamoja na vivutio vyote tulivyokuwa navyo, lakini ningeshauri tutengeneze hizi amusement park katika yale maeneo ambayo tunakusudia wale wenyeji wawe wanafika na kupumzika. Kwa mfano kama hapa kuna Mbunge mmoja kazungumzia suala la Dodoma, kuna jiwe pale, kule kungetengenezwa amusement park, maana yake pengine ingekuwa moja ya kivutio cha ile jiwe na kisha ile amusement maana yake watu pengine wanaweza wakapumzika na kuendelea na shughuli nyingine. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, sasa suala la utalii ni suala ambalo ni kubwa sana linahitaji huduma ambazo zilizokuwa bora, tunahitaji miundombinu iliyokuwa bora. Ili tuweze kufanikiwa katika suala hili la utalii, hayo yote yanatakiwa yazingatiwe kwa ubora wake, tuwe na huduma zilizokuwa bora, tuwe na miundombinu bora.

Mheshimiwa Naibu Spika, kimsingi, yote hayo juu ya utalii maana yake ni kuwa na amani. Bahati nzuri sisi Tanzania amani yetu inajitosheleza, kwa hivyo amani yetu ndiyo inaweza kutusababisha kwamba kila mmoja akawa ni kivutio kwa mtalii kuja nchini Tanzania kutokana na amani yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya hayo, naomba kuunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Ofisi ya Waziri Mkuu
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kuweza kunipa nafasi na mimi niweze kuongea machache kujaribu kuzungumzia hotuba ya Waziri Mkuu.

Kwanza napenda kuishukuru Serikali yangu kwa kazi kubwa ambayo wameifanya, na katika moja ya kazi ambazo wamefanya; nimejaribu kuangalia miradi ambayo ni miradi mikubwa sana ambayo imezungumzwa katika taarifa ya Waziri Mkuu; kwamba kuna miradi takriban saba ambayo imetumia fedha nyingi sana; na fedha hizo ni kweli nitasema kwamba ni pesa ambazo kwa kiasi fulani tujipe moyo Tanzania inasonga mbele. Kama alivyozungumza Rais wetu mpendwa mama Samia Suluhu Hassan kazi iendelee, kweli kazi inaendelea.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumejaribu kufanya ziara na Kamati yangu ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma, tumepita miradi kadhaa. Ndani ya nchi hii kuna vitu ambavyo vinafanywa ni vikubwa sana; na hii inaonesha uhalisia kwamba nchi yetu inapiga hatua na uchumi unaweza ukakua kwa kiasi fulani. Hata hivyo, kwenye miradi hii ningependa pengine kuishauri Serikali; miradi ni mikubwa lakini kitu muhimu zaidi ni kuweza kujua namna na adhma ya ile miradi yetu. Lengo ni kuhakikisha uchumi wa nchi unakua.

Mheshimiwa Mwenyekiti,Serikali ilipojenga reli ya Standard gauge ilikuwa na dhima maalum. Maana yake ni kwamba tukimaliza ujenzi wa reli hiyo tujue adhma ya Serikali ni kitu gani pamoja na miradi yote ambayo ilikuwepo, ikiwemo ya meli na miradi mingine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pili nije katika mchango wangu kuhusiana na taarifa ya Bajeti ya Waziri Mkuu, nijaribu kugusia taasisi moja ambayo inahusiana na masuala ya Wakala wa Huduma za Ajira Tanzania (TaESA). Hii taasisi kwa kweli inafanya kazi zake kubwa sana kwa mujibu ambavyo ilivyo na objective zake zilivyo au malengo yake yalivyo, lakini shida ambayo iliyokuwepo ni kwamba TaESA ni kama ni agency; tunasema kwamba imemeza kila kitu. Tukiangalia katika hali ya sasa kwa dunia hii ya leo TaESA mimi nadhani kungelikuwa na uwezekano tukawa na kamisheni itakuwa inafanya uratibu wa shughuli hizo. Baadhi ya shughuli za TaESA tuwaachie mawakala wa ajira ili kuhakikisha kwamba tunaleta muunganiko mzuri katika masuala ya uajiri; na hii inakuja kwa sababu ya mtazamo wa kidunia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mtazamo wa kidunia ni mpana sana. Mtazamo wa kidunia hasa katika suala la soko la ajira limekuwa la pembe tatu. Kuna suala la mawakala wa ajira, kuna suala la muajiri pamoja na yule anayeajiriwa, sasa ili kuweza kupata ajira maana yake ni lazima uanze kwa wakala wa ajira twende kwa mwajiri pamoja na yule candidate kuweza kufikiwa katika shughuli zake. Kwa sasa hivi inakuwa kama kuna monopolize ya hili soko, maana hata hao mawakala wa ajira waliokuwepo katika Taifa letu hili la Tanzania wanafanya, kisheria, kama ni brokers kwa sababu wale sio mawakala hasa. Kwa sababu wao watafute ajira au watafute kazi kisha wazipeleke kwa TaESA ambapo TaESA ndiye atakayeweza kuhakikisha kwamba mtu yule anapatiwa ajira kwa namna gani na hususani katika ajira ambazo ni za nje ya nchi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hili mimi pengine ningeshauri Wizara, ili kuwe na ufanisi mzuri na mkubwa zaidi katika hii taasisi ambayo inahusiana na masuala ya ajira iache baadhi ya loop hole kwa upande wa mawakala wa ajira. Hii ni kwa sababu sasa hivi kidunia tumesaini mikataba (conventions) mbalimbali ya kimataifa zinazohuaiana na labour, ambayo ni lazima tuifuate. Kuna mashirika kwa mfano kama A.I.O, I.O.M ambayo yanahusiana na masuala ya uhamiaji, wale wote wanatakiwa kuratibiwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni vizuri zaidi kila mhamiaji anapokuja, anapotafuta nafasi ya ajira apitie kwa wakala maalum ambaye ndiye ataweza kumpatia nafasi ya ajira. Sasa kazi ya taasisi inayoshughulika na ajira maana yake ifanye kazi ya coordinate na kuchukua data kupitia kwa wale mawakala. Nadhani kwamba inaweza ikafanyika kazi nzuri zaidi na hii inakuja hata kwenye vibali vya ajira.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tutasema tuna vibali almost 8,576 vya kazi, vibali vile ndizo kazi zenyewe za watu wetu ambazo wamepatiwa watu wa nje. Tusiseme kwamba tumepata vibali vingi, kwamba sasa vimetuongezea mapato, tujaribu kuangalia kwa upande wa pili; kwamba zile ni ajira za watu wetu kwamba sasa wamepatiwa ajira watu wengine.

Mheshimiwa Mwenyekiti, sasa hili suala ili kuwe na ufanisi kwa suala la ajira na kusiwe na ule ulegevu ambao; kama kuna Mbunge mwenzangu mmoja alizungumza jana; kwamba imekuwa kama TaESA haina meno, shida yenyewe ni kwamba taasisi ya TaESA ilivyozinduliwa kwa wakati ule ilikuwa kuna haja hiyo. Hata hivyo kwa wakati ambao tunao kwa sasa hivi ni wakati ambao unakwenda katika sayansi na teknolojia, hivyo lazima kuna baadhi ya mambo wajipunguzie ili kuweza kwenda katika hali ya usawa, vinginevyo siku zote ajira zitakuwa zina shida; lakini kama zitakuwa zinapitia katika mlengo wa kimawakala kwenda kwa waajiri ingekuwa ni vizuri zaidi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, na lingine ambalo naweza kulizungumza ni kwamba TaESA kama ni mawakala ni vizuri zaidi kila baada ya mwaka wakatengeneza kitu kinaitwa career fare; ambacho kitakuwa kinakusanya mawakala, waajiri pamoja na candidate kwa mujibu wa fani zao walizo nazo. Sasa kama mwajiri atakuwa anahitaji mfanya kazi…

(Hapa kengele ililia kuashiria kwisha kwa muda wa Mzungumzaji)

MWENYEKITI: Ahsante sana.

MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana, shukrani.
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza nakushukuru sana kwa kuweza kunipatia nafasi hii. Pili, nampongeza Rais wetu, Mama Samia Suluhu Hassan kwa namna ambavyo anafanya kazi kubwa ya kuweza kuipatia Wizara hii ya Ujenzi pamoja na Uchukuzi fedha nyingi sana katika kutimiza miradi yake. Kwa kweli Wizara hii ya Ujenzi na Uchukuzi ni Wizara mama. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi ni Wizara kubwa sana na Wizara ambayo ni kiunganishi cha uchumi katika nchi yetu. Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi tukiangalia kwa hali ya kawaida, maana yake uchumi wa nchi yetu unategemea Wizara hii. Ukiangalia suala la utalii, linategemea Wizara hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa nini ninazungumza hivyo? Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi imebeba mambo yote makubwa, tukiangalia barabara pamoja na masuala yote ya miundombinu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuliangalie suala hili kiukweli kabisa katika Wizara ambayo imefanya mambo makubwa sana ni Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi. Wizara hii kwa kweli ni Wizara ambayo inatakiwa kupigiwa mfano wa hali ya juu sana. Nizungumze ukweli wangu, kwa namna yote ile na niweze kuwasifu viongozi wa Wizara hii akiwepo Mheshimiwa Prof. Mbarawa pamoja na timu yake, kwa kweli wanafanya kazi kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni mjumbe wa Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma. Bahati nzuri tumezunguka sehemu nyingi sana zenye miradi mikubwa sana, tukianzia suala la Mpanda kuelekea Uvinza, Uvinza – Kigoma, kwa kiasi fulani maana yake huko mahali kuna miradi ambayo ni mikubwa sana tukielekea na Mwanza kuangalia miradi ya meli.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tuzungumze ule ukweli, katika sekta ambayo imefanya kazi kubwa ni Wizara hii ya Ujenzi na Uchukuzi. Nazungumza hivi kutokana na kwamba, watu wanasema kwamba mwenye macho haambiwi tazama. Ukweli ndugu zangu Waheshimiwa Wabunge, nasema labda pengine tungefanya safari ya kuzunguka katika maeneo ya Tanzania tukaona namna Wizara hii inavyofanya kazi, ni Wizara ambayo inafanya kazi kubwa sana, ni Wizara ambayo inafanya jitihada kubwa sana. Kiukweli kama alivyozungumza mama kwamba kazi iendelee, miradi yote ambayo imeachwa na mtangulizi wake Marehemu John Pombe Magufuli, miradi yote mpaka sasa hivi kwa 70%, au 80% naweza kuthubutu kusema kwamba kupitia Wizara hii, maana yake imeshakamilika. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije na suala langu la upande wa sekta ya PPP ambayo mara nyingi watu wanaizungumza sana hapa kwamba katika suala la uunganishaji, hii Private Public Partnership kwamba kuna suala la huu uunganishaji wa bandari yetu ya Tanzania kupitia Bandari ya Dar es Salaam, hili suala kwa kweli nasema kwamba ni suala zuri na ninaweza kusema kwamba kwa Tanzania nzima, maana yake ni suala ambalo tusiliache.

Mheshimiwa Mwenyekiti, suala hili kwa upande wa Zanzibar, kitu kama hiki cha uwekezaji wa bandari, maana yake tayari Zanzibar wameshaingia mkataba na Kampuni ya South Africa katika suala la PPP (Private Public Partnership), sasa na sisi kwa kuangalia suala la ufanisi wa bandari yetu ni lazima suala hili tuliangalie katika hali kubwa sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wakati mwingine mimi nitakuwa nashangaa sana kuona watu wanabeza suala la uwekezaji wa pande tatu; Private Public Partnership kwa dunia nzima. Maana yake kwa sasa hivi, maendeleo mengi makubwa yanaendeshwa kwa mpango wa PPP. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuna suala la barabara ambalo nalo Mheshimiwa Waziri alizungumza kwamba kuna barabara ambayo nayo itakwenda kwa mfumo wa PPP. Mimi nadhani kwamba suala hili tujaribu kuliangalia katika hali ya umadhubuti mkubwa sana, isipokuwa suala ambalo ninalolishauri tuwe madhubuti ni katika suala la kuangalia sheria zetu.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nije katika suala la taasisi zetu hizi ambazo ziko chini ya uendeshaji wa Wizara yetu hii ya Ujenzi na Uchukuzi. Tukiangalia kwa mfano, kama taasisi ya TEMESA, inafanya kazi vizuri, lakini kama ilivyozungumzwa kwa upande wa hotuba ile ya Mheshimiwa Waziri kwamba TEMESA ipo kama ni kutoa huduma, nashauri TEMESA iwe ni taasisi ya kibiashara. Kwa sababu inavyokwenda, haiendi katika suala la kuleta tija isipokuwa ni sekta ambayo iko upande wa kutoa service.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mwisho, naipongeza Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi, nampongeza Mheshimiwa Waziri pamoja na timu yake kwa kazi kubwa ambayo wanaifanya katika utekelezaji wa majukumu yake. Pia namshukuru mama kwa kiasi kikubwa sana kwa kuweza kutekeleza miradi yote ambayo ipo ikiwemo ya barabara, ikiwemo ya reli, ikiwemo ya meli na miradi yote ya madaraja makubwa ikiwemo ya daraja la Kigongo - Busisi pamoja na Bwawa la Mwalimu Nyerere. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya kusema hayo, naunga mkono hoja. Ahsante sana. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2023/2024 – Wizara ya Maliasili na Utalii
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana kwa kunipa nafasi hii, kwanza kabla ya yote nampongeza Mheshimiwa Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mama Samia Suluhu Hassan. (Makofi)

Pili nakupongeza wewe kwa namna ya unavyoweza kufanyakazi zako pia na namna ya philosophy ambazo unazozitumia katika Bunge letu hili la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tatu nawapongeza, nampongeza Waziri pamoja na Naibu Waziri wa Wizara yetu hii ya Utalii pamoja na mambo ya natural resource mambo ya Maliasili na Utalii, lakini pamoja na yote, pamoja na kuwapongeza lakini pia nawapa pole. Kwa sababu asilimia kubwa ya Wabunge hapa wanawapongeza lakini wakati huo huo wanakuwa na kitu kama lawama kidogo na hasa kwa upande ule wa maliasili. Kwa hiyo, kwa upande ule kule mimi nawapa pole sana, kwa sababu hili jukumu la maliasili ni jukumu ambalo ni zito na kwa nini nazungumza kwamba ni suala zito? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa sababu ya namna ambavyo ya uasili wake, na siku zote kitu ambacho ni cha asili maana yake siku zote kitakuwa na lawama na ulawama wa asili maana yake huja pale kwamba huna namna ya kuweza kubadilisha. Kwa sababu hapa katika Bunge letu hili utakuta kwamba Wabunge wengi wanalalamika juu ya tembo na mambo mengine kitu ambacho tembo kwa namna ya uasili wake inakuwa ni vigumu sana kuweza kubadilisha na huna namna. Naamini pengine nitakwambia kwamba muweze kukubaliana tu na hizo lawama mnazopewa kwa sababu ya ule uasili wa mambo yake. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, pili nadhani kwamba leo nijikite zaidi kwa upande wa utalii. Utalii wetu wa Tanzania ni utalii ambao ni wakimaumbile, kwa ufupi kwamba naweza kusema kwamba Tanzania hatujawa na ile vision ya moja kwa moja katika suala la utalii kwamba tunaelekea katika utalii wa aina gani?

Mheshimiwa Spika, utalii ni kitu ambacho ni kikubwa sana, na mimi kama ningekuwa natoa ushauri kwa namna ya ukubwa wa Wizara na namna ambavyo ilivyo kwamba Wizara ya Maliasili na Utalii maana yake mimi nigeliweza kushauri tu kwamba huu utalii kutokana na namna ambavyo uwekezaji wake pengine mimi ningeshauri Serikali pengine suala na maliasili likabaki na upande wake na utalii ukabaki upande wake, na kwasababu utalii kwa namna yoyote ile ni sekta ambayo inayojitegemea. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, tukizungumzia suala la utalii. Utalii ndiyo unaojenga kila kitu, tukiangalia hasa katika masuala ya component za utalii, utalii maana yake umejigawa katika component karibu sita, kuna suala la vivutio vya utalii. Vivutio vya utalii maana yake vinajenga pamoja na hizo rasilimali ambazo ndiyo tunazozungumza za misitu pamoja na vitu vingine. Sasa huo wote ni utalii. Tukizungumzia suala la accessibility maana yake yale mambo ambayo ambayo yaliyokuwemo katika ile nchi, maana yake tukiangalia suala la fukwe na mambo mengine, haya yote maana yake tunazungumzia suala la utalii.

Mheshimiwa Spika, tukizungumzia suala la accommodation ambalo ni malazi ambayo nalo ni suala utalii. Tukizungumzia suala la amenity ambalo ni suala pengine la yale mahitaji yaliyomo katika nchi ni suala la kiutalii, pamoja tukizungumzia na activity zile shughuli zilizomo maana yake ni suala la tunazungumzia ni utalii. Sasa utalii ni kitu ambacho nachozungumza kwamba ni sekta moja ambayo ni muhimu sana na ndiyo ni sekta ambayo mama. Kwa sababu kwa nchi za wenzetu mara nyingi jina la utalii hutangulizwa mwanzo lakini sisi maana yake kwamba kama Tanzania tumetanguliza maliasili na utalii.

Mheshimiwa Spika, sasa maliasili na utalii lakini utakuta kwamba maliasili kwa upande wetu maana yake imebeba sehemu kubwa sana hasa katika masuala ya majadiliano, ukiangalia hata kwenye Bunge letu hili maana yake utalii unazungumzwa kama ni component ndogo sana. Wakati utalii ndiyo inayojenga hivyo vitu vingine, hata suala la utalii maana yake tukisema suala la utalii maana yake utalii unatakiwa iwe ni sekta mama, kwamba ni utalii ambao ni sekta ya Wizara ya Utalii na Mambo ya Kale au Wizara ya Utalii na Maliasili. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, utalii pengine mimi ningesema kwamba uwe unaanza mwanzo kisha baadaye ije maliasili, kwa sababu kwenye maliasili ni kitu ambacho kuna vivutio kule. Kwa sababu vivutio vile maana yake ndivyo vinavyoitengeneza hiyo sekta ya utalii katika masuala ya kibiashara, na biashara yetu maana yake tunategemea nini? Tunategemea hizo mbuga za wanyama, tunategemea nini? Tunategemea misitu, tunategemea nini? tunategemea hoteli, tunategemea nini? tunategemea fukwe, tunategemea nini? tunategemea kila aina utamaduni wetu maana yake yote, maana yake ni moja ya utalii hasa utalii maana yake tukiwa tunauweka katika sehemu ndogo itakuwa kidogo tunaupa nafasi ndogo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, najua kwamba unaniangalia kwa sababu ya dakika cha msingi niunge hoja mkono. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, baada ya kusema hayo nasema ahsante sana kwa kuweza kunipa nafasi hii. (Makofi)
Makadirio ya Mapato na Matumizi ya Serikali kwa Mwaka wa Fedha 2022/2023 – Wizara ya Ulinzi na Jeshi la Kujenga Taifa
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Nami sina budi kukushuruku kwa kuweza kuniona kuchangia katika Bajeti hii ya Wizara ya Ulinzi wa Tanzania.

Mheshimiwa Spika, pili napenda kumshukuru Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye pia ndiye Amiri Jeshi Mkuu wa nchi yetu katika ulinzi wa nchi yetu na vilevile Amiri Jeshi Mkuu ndiye mpambanaji wa mambo yote katika nchi yetu hii. Rais wetu ambaye ndiye Amiri Jeshi wetu Mkuu hatuna namna ya kuweza kumpongeza yaani inabidi tumpongeze kwa kiasi kikubwa sana maana yake haya yote ambayo anayoyafanya ni kutimiza wajibu wake na kutekeleza Ilani yetu ya Chama cha Mapinduzi hasa katika Sura 505 katika Ilani ya Chama cha Mapinduzi ambayo inahusiana na Ulinzi.

Mheshimiwa Spika, pili tumpongeze Mkuu wetu wa Majeshi Ndugu Venance Mabeyo kwa umakini wake na uzalendo wake wa kipekee katika kuliongoza Jeshi letu la Tanzania na pia uzalendo wake wa kufanikisha nchi yetu hii kuwa katika hali ya amani. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, nije katika mchango wa Wizara; moja katika jukumu la msingi la Wizara ya Ulinzi ni kuwapa vijana wa Kitanzania mafunzo ya awali ya kijeshi, ya stadi za kazi, utamaduni, uzalendo, umoja wa kitaifa na uwezo wa kujitegemea. Lakini mimi vilevile ningeongezea kitu kimoja ambacho ni uwezo wa kuzalisha mali, ambalo hilo ni moja ya jukumu lililokuwa katika moja ya Wizara. Sasa tuje katika uzalishaji mali huu nadhani kwamba Jeshi letu au Wizara yetu inafanya kazi kubwa sana ya kuweza kuwachukua vijana wetu kuwapa mafunzo pale ya stadi mbalimbali na vilevile kuwafundisha ukakamavu pamoja na uzalendo. Lakini bado tunatakiwa kwamba bado tuendelee kujiuliza katika haya mafunzo tunayowapatia vijana wetu je, bado yanakidhi katika uzalishaji mali katika nchi yetu. Maana yake lengo kujenga uzalendo, lengo ni kuwapa stadi, sasa mimi pengine ningeishauri Wizara pamoja na mambo ambayo tunayafanya huko maana yake wakapatiwa zile stadi mbali za kilimo, lakini pia tukawa na stadi za ufundi kama vilivyo vituo vyetu hivi vya mafunzo hivi vituo vya vocational ambako nako huko labda pengine tungeweza kujenga wigo zaidi ili vijana waweze kupata ule ujuzi ambao utakaoweza kuwasaidia. Watakapoweza kumaliza mafunzo wakaweza kujitegemea na kuweza kujiendeleza na tusiangalie tu kwamba suala la kuwapeleka vijana kule kujenga uwezo au kupata ukakamavu ikawa ndiyo sababu ya kwenda kuwachukua kwa kuwaajiri. Wao lengo kubwa maana yake twende kwa kuweza kuwaajiri na kuweza kujenga uchumi wa nchi yetu.

Mheshimiwa Spika, pili, nije katika kuimarisha Ulinzi na Usalama wa nchi na mipaka yetu yaani katika suala la ibara ya chama chetu inazungumzia suala la ulinzi na usalama ambalo hilo lipo katika hali njema. Lakini muhimu zaidi ambayo nije vilevile katika kazi zinazotekelezwa kupitia fedha za maendeleo. Katika kifungu kimoja ambacho cha fedha za maendeleo kifungu (h) kinazungumzia kutatua migogoro ya ardhi kwa kupima na kufanya uthamini wa maeneo ya Mikoa kama Singida Kaskazini, Mkoa wa Mjini Magharibi na kulipa fidia kwa wananchi wa maeneo matano ambayo yametajwa pale katika fedha za maendeleo. Lakini katika ulipaji wa fidia zile maana yake kuna migogoro ambayo hii imeshazungumzwa, lakini migogoro…

SPIKA: Sekunde 30 malizia Mheshimiwa, kengele imeshagonga.

MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Katika migogoro hiyo kuna baadhi ya maeneo sijaweza kuyaona pia kama Ndunga, pamoja na Udunga, Ubago pamoja na Unguja Ukuu. Ningependa au ningeshauri Serikali waweze kuliangalia suala hilo ili kuweze kutatua migogoro ya wananchi kwa ukaribu zaidi.

Mheshimiwa Spika, napenda kuunga mkono hoja Wizara yetu hii, ahsante sana. (Makofi)
Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa na Serikali Kuu, Mashirika ya Umma na Kaguzi za Ufanisi kwa Mwaka wa Fedha uliuoishia tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Hesabu za Serikali za Mitaa kuhusu Taarifa ya Mdhibiti na Mkaguzi Mkuu wa Hesabu za Serikali kwa hesabu zilizokaguliwa za Mamlaka za Seriakli za Mitaa kwa Mwaka wa Fedha ulioishi tarehe 30 Juni, 2022 na Taarifa ya Kamati ya Kudumu ya Bunge ya Uwekezajiwa wa Mitaji ya Umma kuhusu uwekezaji wa mitaji ya umma kwa Mwaka wa Fedha 2021/2022
MHE. HAJI AMOUR HAJI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipatia nafasi hii ya kuweza kutoa yangu ambayo yapo katika uchambuzi wa Taarifa zetu ambazo tunazijadili leo kuanzia asubuhi.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja katika taarifa ambazo tulizonazo tuna taarifa ya Mahesabu ya Umma, Taarifa ya LAAC na kuna Taarifa ya PAC. Mimi nadhani kwamba nijielekeze zaidi kwenye taarifa inayohusiana na Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji ya Umma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi ni Mjumbe ambae nipo katika Kamati ile ambayo moja kabla ya yote hayo nipende kumshukuru Mheshimiwa Rais, Mama Samia Suluhu Hassan kwa kuweza kuyajali mashirika yetu haya na kuweza kukaa nayo kwa pamoja kutafuta namna ya ufanisi na tija ya mashirika yetu alikaa nayo katika kikao kimoja pale Arusha, ambapo pale kulikuwa na mazungumzo mengi na kuweza kuyajenga yale mashirika kama ni semina.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja katika shughuli ambayo tunaifanya katika Kamati ya Uwekezaji na Mitaji ya Umma ni kwamba kuangalia ufanisi wa mashirika yetu ya umma pamoja na tija yake. Tunavyojua kwamba moja katika vitu viwili hivi lazima kwamba vinakuwa vinaendana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye ufanisi au kukosekana kwa ufanisi maana yake kutakuwa kutakosekana kwa tija katika mashirika yetu. Katika taarifa zetu tulizozipitia katika mashirika yetu ya umma tumejaribu kuangalia mashirika mengi sana kwa sababu kwenye Kamati yetu ya Mitaji ya Umma tuna mashirika karibu 287 ambayo ndiyo tunatakiwa kuyajadili na kuyajengea hoja katika ufanisi na tija katika mashirika hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya mambo ambayo yalikuwemo katika mashirika yetu tumejaribu kuangalia tija pamoja na ufanisi wa mashirika yale, katika mashirika na tija ambayo ipo katika mashirika yetu yamejigawa katika makundi matatu. Kuna kundi la mashirika ya umma ambayo yanatoa gawio na kwa mujibu wa sheria, kuna makundi na kundi la mashirika ya umma ambayo yanatoa asilimia 15 na kuna kundi la mashirika ambayo yanatoa ziada na kuna kundi la mashirika ya umma yanatoa kwa mujibu wa vile ambavyo wanajihisi namna ya kutoa katika Serikali, ndicho ambacho tulikibaini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tukilinganisha mlingano wa takwimu ya mwaka jana na mwaka huu wa fedha maana yake ukitizama katika mashirika yenye kutoa gawio kuna mashirika 66. Kwa mujibu wa taarifa ya Mwenyekiti wangu wa Kamati ya Uwekezaji wa Mitaji wa Umma, alitaja mashirika 66 ambayo kati ya mashirika 66, mashirika 25 tu ndiyo yaliyotoa gawio. Hiki ni kitu ambacho ukiangalia upande mwingine ukiangalia kwamba, ule ufanisi na ile azma ya kuweza kuyajenga yale mashirika yetu maana yake maana yake hayajafikiwa katika hali nzuri. Pamoja na kwamba mashirika 25 ndiyo yaliyotoa gawio na kupata shilingi 37,528.000.000 na kuendelea bado ukiangalia mashirika yote 66 yenye kutoa gawio maana yake hapo tungekuwa tuna fedha nyingi sana katika ukusanyaji wa mapato yetu. Kimsingi nitasema kwamba kazi bado tunayo ya kuweza kuifanya, maana yake hili ambalo tutasema kwamba mashirika 25 waliotoa na ukilinganisha mwaka jana maana yake mashirika haya kidogo tumejitutumua kidogo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, upande wa mashirika yale yanayotoa asilimia 15 kwa kiasi fulani nayo si haba maana yake kwa sasa hivi yametoa karibu asilimia 70. Lakini kuna tatizo ambalo ni la kiutendaji na kiufanisi katika haya mashirika yetu, kwanza tulichokigundua katika mashirika yetu kuna kitu ambacho kimekuwa kinagomba kwa mashirika yetu. Kwanza hawaangalii namna ambavyo zile K.P.I zilizowekwa na Msajili wa Hazina hawazizingatii ipasavyo, kwa sababu utakuta kwa mfano kama taasisi ya maji kwamba kigezo walichowekewa kwa mfano kama upungufu wa maji maana yake usizidi au katika umwagikaji wa maji maana yake usizidi asilimia 25. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, utakuta kwamba katika K.P.I zao maana yake wapo zaidi ya hapo. Kuna baadhi ya mashirika mengine maana yake hata ule utendaji wao unaonekana dhahiri kwamba hauko vizuri na kwa sababu kuna baadhi ya mashirika tumeyakuta katika hata ule mpango mkakati wao hauko vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile tumelikuta hata shirika, kuna baadhi ya mashirika ambayo tumekuwa nayo tumelikuta hata ule mpango mkakati hakuna. Sasa katika kupima zile K. P.I maana yake utakuta shirika lile hujui hata ulipime namna gani.

Mheshimiwa Mwenyekiti, mimi niweze kumpongeza Msajili wa Hazina kwa jitihada zake kubwa ambazo anazozichukua katika namna ya kuweza kutafuta mwarobaini wa kuyafanya mashirika yetu yawe ya kibiashara, kwa sababu pamoja na yote hayo maana yake kuna mashirika ambayo wakati mwingine yanapatiwa ruzuku, lakini ile ruzuku wanayopatiwa maana yake hakuna tija yoyote inayorudi katika Serikali. Kuna mashirika yale ya kibiashara moja kwa moja maana yake yanafanya biashara zaidi ya zile ruzuku wanazopewa na Serikali yake hakuna kitu chochote. Ufanisi pale unakuwa unakosa na tija inakuwa haipo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tumegundua kwamba kuna baadhi ya mashirika hata wale Watendaji wake wa Bodi ukiwapima hawawezi kupimika. Mimi ninaiomba Serikali pamoja na yote hayo lakini kuna haja kubwa sana ya Msajili wa Hazina kuweza kukamilisha mchakato wake wa sheria ili waweze kuja hapa Bungeni lengo kubwa ni kuweza kuwahakikishia kwamba mashirika yetu ya umma yanafanya vizuri.

Mheshimiwa Mwenyekiti, pamoja na yote hayo nasema kwamba nampongeza sana TR kwa kazi yake kubwa anayoifanya, nampongeza sana Mheshimiwa Rais kwa kuweza kuyajali mashirika yetu na kwa namna ambavyo anavyokusudia kuyafanya kwamba yaweze kuleta ufanisi na tija. Natumai kwamba mabadiliko yoyote yatakayokuja ya sheria yatakayotoka kwa Msajili wa Hazina yatakuwa ni mabadiliko yenye kuleta tija na ufanisi kwa mashirika yetu. (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, baada ya hapo naunga mkono hoja taarifa za Kamati zetu zote tatu ambazo zimewasilisha taarifa zao hapa, Ahsante sana. (Makofi)