Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Ester Alexander Mahawe

Primary Questions
MHE. FLATEI G. MASSAY (K.n.y MHE. ESTER A. MAHAWE) aliuliza:-
Serikali kupitia mpango mkakati wa kuwawezesha wananchi wa vijijini iliahidi kutoa shilingi 50,000,000 kwa kila kijiji na mtaa:-
(a) Je, ni lini fedha hizo zitatolewa?
(b) Je, Serikali imejipanga vipi kutoa elimu ya ujasiriamali kwa wananchi juu ya njia bora ya kutumia fedha hizo?
MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-
Bajeti ya mpango wa barabara inayopelekwa katika Halmashauri zetu ni ndogo na haikidhi mahitaji:-
Je, Serikali haioni ni wakati muafaka sasa kuongeza bajeti hiyo ili Halmashauri nchini ziweze kununua vifaa vya kutengenezea barabara zao za ndani ili kuondoa kero isiyokuwa ya lazima?
MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-
Wilaya ya Simanjiro haina Hospitali ya Wilaya na hivyo kusababisha mateso kwa wakazi wa maeneo mbalimbali ya Wilaya hiyo hususan wanawake ambao wanakosa huduma za kujifungua lakini pia kutokana na uchache wa vituo vya afya na zahanati.
(a) Je, ni lini Serikali itavipa hadhi vituo vya afya vya Mererani na Orkesment ili kupunguza tatizo?
(b) Wilaya ya Simanjiro ina gari moja tu la wagonjwa; je, ni lini Serikali itapeleka gari lingine kwenye Kituo cha Afya Mererani ili kuokoa maisha ya akina mama wajawazito?
MHE. ZACHARIA P. ISSAAY (K.n.y MHE. ESTHER A. MAHAWE) aliuliza:-
Vituo vya Afya na Zahanati zilizo karibu na Hospitali za Wilaya zina changamoto ya utoaji huduma bora kwa sababu ya upungufu wa dawa na watumishi wa kada ya afya hivyo kusababisha kuhudumiwa na Hospitali za Wilaya ambazo bajeti za dawa hazikidhi:-
Je, Serikali haioni umuhimu wa kuongeza bajeti ya Hospitali za Wilaya zilizoko katika Mkoa wa Manyara?
MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-
Fedha zinazokusanywa za asilimia 0.3 ya service levy zimeshindwa kusaidia Halmashauri nchini kwa uwiano unaolingana.
Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka fedha hizo kukusanywa na TAMISEMI ili kila Halmashauri iweze kupata mgao unaolingana?
MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-
Kadi za kulipia Ngorongoro zimekuwa kero kwa wageni na wahudumu kwani muda mwingi umekuwa ukipotea wakati kufanya malipo.
Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ili kuwe na mfumo wa kadi kama za TANAPA?
MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-
Madini ya Tanzanite yanachimbwa Mkoani Manyara katika Wilaya ya Simanjiro, lakini madini hayo huchakatwa na kuuzwa Mkoani Arusha hali inayosababisha wananchi wa Manyara kutofaidika kiuchumi.
(a) Je, ni nini kauli ya Serikali kuhusu kujenga kiwanda cha kuchakata madini hayo Mkoani Manyara?
(b) Je, ni kiasi gani cha fedha kimeshachangiwa na madini haya katika mapato ya Mkoa wa Manyara?
MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-
Takwimu zinaonesha upungufu mkubwa wa matundu ya vyoo zaidi ya 200,000 katika shule mbalimbali za sekondari na msingi.
(a) Je, nini mkakati wa Serikali wa kumaliza tatizo hilo?
(b) Je, Serikali haioni sasa ni muda muafaka wa kuja na mkakati mbadala kama ilivyofanya wakati wa kumaliza tatizo la madawati na maabara nchini?
MHE. ESTHER A. MAHAWE aliuliza:-
Sera ya Elimu ya mwaka 2014 inaelekeza utoaji wa elimu bila malipo kuanzia ngazi ya chekechea hadi kidato cha nne ikiwemo kuondoa gharama za kulipia mitihani ya kitaifa katika shule za msingi na sekondari lakini wanafunzi wanaosoma katika shule zisizo za Serikali wanalipishwa gharama hizo wakati wazazi wao wanalipa kodi inayowezesha kutolewa elimu hiyo bila malipo:-
Je, ni lini Serikali itafuta ada hiyo ya mitihani kwa wanafunzi wanaosoma katika shule binafsi?
MHE. ESTER M. MMASI (K.n.y. MHE. ESTER A. MAHAWE) aliuliza:-
Gharama za kupanda Mlima Kilimanjaro ni mara mbili ya gharama za kupanda Mlima Kenya; hali hii imesababisha kushuka kwa idadi ya watalii na kuinyima Serikali mapato. Je, ni lini Serikali itafanya marekebisho ya bei hizo?
MHE. INNOCENT L. BASHUNGWA (K.n.y. MHE. ESTER A. MAHAWE) aliuliza:-
Sekta ya utalii inachangia pato kubwa la fedha za kigeni katika nchi yetu.
Je, ni lini Serikali itatengeneza barabara ya Serengeti ambayo ni mbovu kiasi cha kufanya watalii kukataa kupita huko?
MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-

Mkoa wa Manyara, hususani Wilaya ya Mbulu, umewahi kutoa wanariadha mahiri ambao walililetea Taifa heshima kubwa, lakini cha kushangaza wanariadha hao wametelekezwa:-

(a) Je, ni lini Serikali sasa itaandaa utaratibu wa kuwaenzi wanariadha hao?

(b) Je, ni lini sasa Serikali itajenga uwanja kwa ajili ya riadha katika Mkoa wa Manyara ili kuwahamasisha wanariadha wapya?
MHE. ESTER A. MAHAWE Aliuliza:-

Halmashauri ya Mbulu haina Hospitali ya Wilaya hivyo wananchi wa Kata za Gidhim, Yayeda, Ampatumat hutembea umbali mrefu kufuata huduma katika kituo cha Afya Dongobeshi.

(a) Je, ni lini Serikali itapandisha hadhi Kituo cha Afya Dongobesh ili kiweze kuwahudumia wananchi wa Mbulu Vijijini na kupunguza msongamano katika Hospitali ya Rufaa ya Hydom?

(b) Je, ni lini Serikali itaongeza Watumishi wa Afya, dawa na vifaa tiba katika kituo hicho cha afya?
MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-

Kata za Naberera, Kitwai, Lorbene, Loibosroit, Norakauwo na Komolo katika Wilaya ya Simanjiro hazina huduma ya mawasiliano ya simu:-

Je,ni lini sasa Serikali itapeleka minara ya simu ili wananchi hao waweze kupata huduma ya mawasiliano ya simu?
MHE. ESTER A. MAHAWE aliuliza:-

Je, ni lini Serikali itawalipa fidia wananchi wa Sinai, Hangoni, Kwere na Mruki waliopitiwa na barabara ya “By Pass” ya magari makubwa yatokayo Dodoma na kutokea stendi mpya ya Babati Mjini?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's