Spika wa Bunge la Jamhuri ya Muungano wa Tanzania, Mhe. Mussa Azzan Zungu (Mb), amekutana na kufanya mazungumzo na uongozi wa Chama cha Wamiliki wa Viwanda Vidogo na Wazalishaji Wadogo Tanzania (TASSIM), wakiongozwa na Afisa Mtendaji Mkuu wa Chama hicho, Ndg. Elia Joseph. Kikao kicho kimefanyika tarehe 28 Januari, 2026 Ofisini kwake Bungeni Jijini Dodoma.