Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Hassan Selemani Kaunje

Supplementary Questions
MHE. HASSAN S. KAUNJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali ya nyongeza.
Mheshimiwa Naibu Spika, mchango wa eneo hili la bahari unaendana na shughuli za wavuvi na Lindi kuna wavuvi. Nilipenda niulize nini msimamo wa Serikali kuwasaidia wavuvi wa Lindi kuhusiana na kodi mbalimbali ambazo ni kero kwao? Vilevile wana mpango gani wa kuwasaidia zana za uvuvi ili waweze kuleza pato katika Halmashauri ya Manispaa ya Lindi?
MHE. HASSAN S. KAUNJE: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwanza kwa majibu ya ziada ya Mheshimiwa Naibu Waziri. Swali langu la msingi ilikuwa ni lini, kwa maana ni mwaka gani katika miaka hii mitano au bajeti ipi hizi program za Maendeleo ya Sekta ya Utalii Kusini zitaanza?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali langu la pili, kwa maana ya vivutio alivyovitaja, sambamba na vivutio vingine vya fukwe za Kisuele na Mitema ambazo ni bora kuliko zote katika ukanda wa Pwani ya Afrika Mashariki, kuanzia Somalia mpaka South Africa: Je, yuko tayari kuviwekea vipaumbele katika kuvitangaza kupitia taasisi zake zinazotangaza utalii wa nchi hii?
MHE. HASSAN S. KAUNJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kwa jibu la Mheshimiwa Naibu Waziri, lakini nisikitike tu kwamba jibu lake haliendani na uhalisia.
Mheshimiwa Mwenyekiti, uhalisia uliokuwapo Lindi ni kwamba takwimu za watu wanaokadiriwa 100,000 ni wa Jimbo la Lindi Mjini. Vilevile nimkumbushe Naibu Waziri katika mchakato wa bajeti iliyopita ya mwaka jana kwamba maafisa wa Halmashauri walishakaa vikao tofauti na maafisa wa Wizara yake katika kuangalia uwezekano wa kubadili bajeti kutokana na idadi ya watu. Sasa anaposema kwamba idadi ya wakazi wa Lindi na akitumia takwimu za wapiga kura ni sahihi nakataa kukubali jibu lake. (Makofi)
Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba niulize maswali ya nyongeza kama tu Mheshimiwa Naibu Waziri na Wizara yake walikubali kwamba idadi ya watu wa Lindi ni kidogo na hivyo watafanyia kazi mchakato wa kuongeza bajeti katika bajeti inayokuja, je, yuko tayari kuthibitisha hilo au kulifanyia kazi hilo kwa bajeti inayokuja?
Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile kutokana na idadi ya watu kutotumika idadi stahiki katika Jimbo la Lindi imepelekea huduma za afya kupelekwa katika kituo kimoja tu cha afya katika Lindi Mjini na hivyo kupelekea shida kubwa kwa watu wa Lindi.
Je, Mhehsimiwa Waziri anayehusika yuko tayari kuiboresha hospitali inayotoa huduma ambayo inaendeshwa na Jeshi la Polisi Lindi ili kuweza ku-accommodate matatizo ya afya ya wananchi waJimbo la Lindi? Ahsante sana.
MHE. HASSANI S. KAUNJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Naibu Waziri yuko tayari kuwaambia wananchi wa Lindi kumwambia Mbunge wao na Mheshimiwa Rais kwamba ahadi ya Mheshimiwa Waziri wake ya kwamba mradi huu utakamilika tarehe 3 Julai, 2017 kwamba, itatekelezwa kama walivyoahidi? Swali la kwanza.
Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, naomba Mheshimiwa Naibu Waziri awe tayari kuweza kunifikishia salamu zangu za pongezi kwa Mheshimiwa Waziri, Katibu Mkuu na yeye mwenyewe kwa kuweza kukamilisha mradi mwingine pacha na huo wa kijiji cha Chikondi. Je, Mheshimiwa Waziri atakuwa tayari kunifikishia salamu zangu hizo? Ahsante sana.
MHE. HASSAN S. KAUNJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Mheshimiwa Waziri wa Maji, tulifanya ziara ya kukagua vyanzo vya maji katika eneo la Manispaa ya Lindi na kuna mradi mkubwa wa maji wa Ng‟apa, Lindi. Je, Mheshimiwa Waziri anaweza kuniambia mradi ule utakamilika lini na wananchi wa Lindi wakaweza kupata maji ya kunywa? Ahsante.
MHE. HASSAN S. KAUNJE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante Mheshimiwa Waziri kwa majibu mazuri nina maswali mawili ya nyongeza.
La kwanza Serikali ya Awamu ya Nne ilitoa ahadi ya kujenga kituo cha Afya katika kata ya Mnazi Mmoja. Ahadi hii ilikuwa ina inataka kutekelezwa na Serikali Kuu, mpaka tunapozungumza hakuna chochote kinachoendelea ikiwa ni mwaka wa saba sasa. Nini kauli ya Serikali kuhusu jambo hilo?
Swali la pili, wananchi wa Lindi tuliwahamasisha waanze kujenga vituo vya afya katika kata zao. Wamepata maelekezo kutoka TAMISEMI ya kwamba vituo hivyo visimame kujengwa kwa muda mrefu mpaka sasa. Nini kauli za Wizara dhidi ya watu wale ambao wameamua kujitolea kuweza kujenga vituo vile vya afya? Ahsante.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's