Parliament of Tanzania

Questions By: Hon. Bernadeta Kasabago Mushashu

Primary Questions
MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU aliuliza:-
Walimu wamekuwa wakiidai Serikali stahiki zao mbalimbali na tatizo hili la kutowalipa kwa muda muafaka limekuwa likijirudia rudia:-
(a) Je, walimu wanadai stahiki zipi na kwa kiasi gani?
(b) Je, Serikali imejipangaje kutatua tatizo hilo na kulimaliza kabisa?
MHE. JOSEPHINE J. GENZABUKE (K.n.y. MHE. BERNADETA K. MUSHASHU) aliuliza:-
Wazabuni wanaotoa huduma shuleni wanaidai Serikali fedha nyingi kwa huduma walizotoa miaka iliyopita.
(a) Je, Serikali inadaiwa fedha kiasi gani na kwa miaka ipi na wazabuni hao?
(b) Je, ni lini madai hayo yatalipwa?
MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU aliuliza:-

Kahawa ni zao la biashara na la kimkakati ingawa kwa miaka kadhaa bei ya zao hilo imeendelea kuwa chini:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuinua zao hilo Mkoani Kagera ikiwemo kupandisha bei ili kumnufaisha mkulima?
MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza:-

Miundombinu ya Shule ya Sekondari Rugambwa ilijengwa mwaka 1964 na Sekondari ya Bukoba imejengwa mwaka 1939, hivyo imechakaa sana:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuzifanyia ukarabati shule hizo?
MHE. HALIMA A. BULEMBO (K.n.y. MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU) aliuliza:-

Mkoa wa Kagera una vijiji 134 ambavyo havijafikiwa na umeme wa REA; Biharamulo Vijiji 29, Bukoba Vijiji 9, Karagwe Vijiiji 8, Kyerwa Vijiji 31, Misenyi Vijiji 5, Muleba Vijiji 25 na Ngara Vijiji 27:-

(a) Je, ni lini Serikali itapeleka umeme wa REA katika Vijiji hivyo?

(b) Umeme wa REA ulifika kwenye vijiji vingi lakini haukusambazwa: Je, mradi wa ujazilizi utaanza lini Mkoani Kagera ili wananchi waliorukwa wapatiwe umeme?
MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza:-

Mafuriko yanayotokea katika Mji wa Bukoba husababisha uharibifu mkubwa wa chakula, mali, barabara na hata kusababisha vifo kwa watu na mifugo; mafuriko hayo husababishwa na Mto Kanoni kujaa mchanga na takataka:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kuwaondolea kero ya mafuriko kila mwaka ikiwemo kusafisha na kuongeza kina cha Mto Kanoni?
MHE. BENARDETHA K. MUSHASHU Aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kujenga Chuo Kikuu katika Mkoa wa Kagera?
MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, ni lini wananchi waliokuwa wameweka fedha zao katika Benki ya Wakulima wa Kagera ya KFCB iliyofungwa na Benki Kuu Mwaka 2018 watarejeshewa fedha zao?
MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kukomesha ukatili wa kijinsia nchini?
MHE. BERNADETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, ni vijiji vingapi havijapatiwa umeme wa REA na nini mpango wa Serikali kusambaza umeme kwenye vijiji vyote vya Mkoa wa Kagera?
MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itatafuta soko la uhakika la zao la vanilla?
MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga hospitali kubwa katika Mkoa wa Kagera?
MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kudhibiti Magonjwa yasiyoambukiza?
MHE. BENARDETA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, Serikali ina mpango gani wa kutokomeza kabisa ugonjwa wa Malaria nchini?
MHE. BERNADETHA K. MUSHASHU aliuliza: -

Je, ni lini Serikali itahakikisha kuwa Mto Kanoni uliopo katika Manispaa ya Bukoba unasafishwa, kina kinaongezwa na kingo za mto zinajengwa?

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's