Parliament of Tanzania

Naibu Spika apokea vifaa vya Zahanati ya Bunge

OFISI ya Bunge imepokea msaada wa vifaa vya zahanati. Msaada huo ulitolewa Mjini Dodoma jana kutoka Kampuni ya Jaffery Ind. Sainiz Funiture na kupokelewa na Naibu Spika wa Bunge, Dkt. Tulia Ackson.


Akikabidhi msaada huo Mkurugenzi Mtendaji wa Kampuni hiyo,Vishal Singh Saini alisema Kampuni hiyo ilipewa zabuni ya kutengeneza samani mbalimbali za Bunge na kwamba baada ya kumaliza kazi hiyo ikaamua kutoa sehemu ya mapato waliyoyapata kutoa msaada huo.


Alivitaja vifaa vilivyotolewa kwamba ni vitanda viwili vya kulaza
wagonjwa, pazia la kijani, stendi ya kutundikia dripu za wagonjwa na kabati dogo la wodini.


Mbali na kutoa msaada huo, Kampuni hiyo pia ilitumia nafasi hiyo
kuonyesha samani mbalimbali zinazotengenezwa na Kamapuni hiyo.


Kwa upande wake Naibu Spika mbali na kushukuru kwa msaada huo lakini pia aliipongeza kwa kutengeneza samani zenye ubora ikiwemo madawati.


Aliitaka Kampuni hiyo kuangalia uwezekano wa kupunguza bei za samani zao ikiwemo kwa madawati hasa kwa wale ambao watahitaji kununua samani
hizo kwa wingi.


Aidha, alizihamasisha taasisi mbalimbali ikiwemo wananchi mmojammoja kununua samani za ndani ili kulinda viwanda vya ndani na kutoa ajira kwa Watanzania.


Awali Mbunge wa Iringa Mjini, Mh. Peter Msigwa akizungumza katika hafla hiyo alIitaka
bei ya madawati ipunguzwe ili wabunge waweze kununua na kusaidia maeneo yao yenye upungufu.

Hon. Dr. Tulia Ackson

Speaker

Legislative Role

Profile

Ask the Speaker / Comments

Ms. Nenelwa J. Mwihambi

Clerk of the National Assembly

Legislative Role

Profile

Ask the Clerk / Comments

View All MP's