Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:- Je, nini utaratibu wa Serikali kutoa msamaha wa kodi ya jengo kwa wale wanaostahili baada ya kodi kuhamishiwa kwenye za LUKU?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALEKO: Mheshimiwa Spika, ahsante sana nina maswali mawili ya nyongeza; mwaka jana wakati wa Waziri wa Fedha akihitimisha hotuba ya bajeti ya mwaka 2021/2022 alisema kwamba wale wote ambao wana haki ya kupata msamaha huo watapata msamaha wa kodi hiyo, lakini mpaka sasa wanaendelea kutozwa.

Je, Serikali haioni ni wakati muafaka TRA na TANESCO kuweza kubadilisha mifumo hiyo ili watu hawa waendelee kupata msamaha wa kodi hiyo? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, je, Serikali ina mpango gani wa kurudisha fedha hizo ambazo wamekuwa wakiwakata watu hawa ambao tayari walikuwa wamewaahidi kwamba fedha hizo hazitaendelea kukatwa? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, kwanza nimpongeze sana Mheshimiwa Esther Malleko, Mbunge wa Viti Maalum, Mkoa wa Kilimanjaro, shemeji yangu huyu kwa kuwatetea sana Watanzania hasa wanyonge.

Mheshimiwa Spika, nakumbuka wiki moja iliyopita alisimama kidete kuhusu ruzuku ya kahawa na Serikali tumechukua jambo hilo. Hata hili alilolileta, ni kweli tulipoanza tulianza tukiwa tuna ujaribisha mfumo huku tukiwa tunatekeleza sheria ya Bunge, kwa maana hiyo ni kweli kulitokea baadhi ya watu waliendelea kukatwa huku wakiwa wanastahili kusamehewa. Lakini tulirekebisha kwa kiwango kikubwa mifumo hiyo, kwa hiyo kama bado wapo ambao wamebakia wachache ambao wameendelea kukatwa nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba jambo hilo tutalifanyia kazi na nielekeze Mamlaka ya Mapato kufanya haraka kumalizia wale ambao bado hawajanufaika na msamaha huo. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa mwaka wa fedha unakwenda kuanza tutafanyia kazi na hilo la kimfumo ili kuweza kufanya sorting zote ili tunapoanza mwaka mpya tuwe tumekamilisha jambo hilo kikamilifu, nakushukuru.

Mheshimiwa Spika, kwanza nachelea kusema kiendacho kwa mganga hakirudi kwa sababu Kilimanjaro hata waganga walishakwisha, ninachoweza kusema tu ni kwamba kwa wale ambao kumbukumbu zao zinaonesha wamekatwa na walitakiwa wasilipe wawasiliane na Mamlaka ya Mapato kwa sababu kwenye kodi huwa kuna utaratibu wa kufanya offsetting kile ambacho ulishakilipa in advance ili kiweze kuwa offsetted wakati unalipa kinachofuata. (Makofi)

Name

Mwita Mwikwabe Waitara

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tarime Vijijini

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:- Je, nini utaratibu wa Serikali kutoa msamaha wa kodi ya jengo kwa wale wanaostahili baada ya kodi kuhamishiwa kwenye za LUKU?

Supplementary Question 2

MHE. MWITA M. WAITARA: Mheshimiwa Spika, ahsante, naomba nimuulize Mheshimiwa Waziri wa Fedha kwamba mpaka wa Sirari ni mkubwa sana kutoka Sirari mpaka kule Nyanungu ambako ukimtaka mwananchi atoke aje apishe Sirari pale alipe kodi ya Serikali ni ngumu kidogo. Kwa nini kusiwe na kituo kidogo cha Forodha pale Witembe Itirio ili wananchi walipe mapato halali ya Serikali badala ya kufanya magendo kugombana na polisi? Ahsante. (Makofi)

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi, nimpongeze babu yangu Mheshimiwa Mwita kwa kuleta swali hilo. Nilishapokea swali la aina hiyo pia kutoka kule Kakonko kwa ndugu yangu Aloyce, niunganishe tu kwamba baada ya Bunge wale Waheshimiwa Wabunge ambao kwenye maeneo yao wangehitaji kuwa na mpaka mpya nizungukie mimi pamoja na Naibu wangu ama wataalam wetu ili tujiridhishe na zile sifa ambazo zinatakiwa kwa ajili ya kuanzisha mpaka mpya wa Tanzania na nchi jirani kwa upande wa ofisi ya Mamlaka ya Mapato ili tuweze kuwarahisishia wananchi wanapotaka kupata huduma ya Mamlaka ya Mapato.