Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 35 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 308 2022-06-01

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:-

Je, nini utaratibu wa Serikali kutoa msamaha wa kodi ya jengo kwa wale wanaostahili baada ya kodi kuhamishiwa kwenye za LUKU?

Name

Dr. Mwigulu Lameck Nchemba Madelu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Magharibi

Answer

WAZIRI WA FEDHA NA MIPANGO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kutoa msamaha wa kodi ya majengo kwa wale wanaostahili unaendelea kutekelezwa kwa mujibu wa Sheria ya Serikali za Mitaa ya Utozaji wa Kodi ya Majengo Sura 289 ambapo mwenye jengo husika anatakiwa kuwasilisha maombi ya kupata msamaha wa kodi ya jengo kwa Mamlaka ya Mapato Tanzania. Baada ya TRA kujiridhisha kuwa muombaji anastahili msamaha kwa mujibu wa matakwa ya sheria, makato yake katika ununuzi wa umeme kupitia LUKU yatasitishwa. Aidha, kifungu cha 7(a) hadi (i) cha Sheria ya Serikali za Mitaa ya Utozaji wa Kodi ya Majengo, Sura 289, kimeainisha majengo yaliyosamehewa kulipa kodi ya majengo.

Mheshimiwa Spika, utaratibu wa kutoa msamaha wa kodi ya majengo umeainishwa katika Kanuni za Mamlaka za Serikali za Mitaa, Ukusanyaji wa Kodi ya Majengo, 2020 sehemu ya nne, Na. 16(1) hadi (6).

Mheshimiwa Spika, utozaji wa kodi ya majengo kupitia manunuzi ya umeme wa mfumo wa LUKU hauondoi haki ya msamaha wa kodi ya majengo kwa anayestahili kisheria bali umeongeza ufanisi katika kujiridhisha kuwa muombaji anastahili msamaha ili kuepuka kuwaondolea makato hata wanaostahili.