Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Dr. Raphael Masunga Chegeni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busega

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:- Mradi wa REA II ulitarajia kuvipatia umeme vijiji vyote vya Jimbo la Busega na kumekuwepo na kusuasua kwa utekelezaji wa mradi huo jimboni humo:- (a) Je, mpaka sasa ni vijiji vingapi vimepatiwa umeme kupitia mradi huo? (b) Je, ni lini vijiji vilivyobaki vitapatiwa umeme?

Supplementary Question 1

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI: Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri sana ya Mheshimiwa Naibu Waziri, napenda niipongeze Serikali kupitia Mradi huu wa REA I, II na III. Kwa kuwa kuna Kata ya Badugu yenye vijiji vya Mwaniga, Manala, Badugu yenyewe na Busani mpaka leo wanaona nguzo za umeme zimepita tu, lakini hawajapewa transfoma. Je, Mheshimiwa Waziri ananihakikishia kwamba vijiji hivi vitapata umeme sasa kuanzia Julai?
Mheshimiwa Naibu Spika, swali la pili, kwa kuwa vijiji vya Nyakaboja vilivyoko kwenye njia kuu ya kwenda Musoma, Vijiji vya Mngasa, Kalago na Lukungu ambako kuna kituo cha afya mpaka leo hakuna umeme. Je, Mheshimiwa Waziri vilevile atanihakikisha kwamba vijijni hivi ambavyo vinatoa na huduma za Hospitali ya Lukungu pamoja na Hoteli ya Serenity na Speke Bay ambazo zinaingiza mapato kwa nchi hii, vitapatiwa umeme?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, kuhusiana na Kata ya Badugu kupatiwa umeme, nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge kwamba vijiji vyote vya Kata ya Badugu, kama anavyojua Mheshimiwa mwenyewe ni kwamba maeneo yote ya Nyamikoma, Nyakaboja, Nyakungula pamoja na yale yote ambayo yanaunganishwa Kata ya Badugu yatapatiwa umeme kwenye awamu hii.
Mheshimiwa Naibu Spika, hata hivyo, vijiji vya Kata ya Badugu ambavyo vimebaki ambavyo vinajumuisha maeneo ya Nyamanara, Nyamikoma, Nyazikungura pamoja na maeneo mengine ya Lamadi yatapatiwa umeme kwenye transfoma itakayofungwa kuanzia Julai, 2016.
Mheshimiwa Naibu Spika, swali lake la pili kuhusu umeme kwa vijiji ambavyo vinaungainisha hospitali ya Lukungu pamoja na hoteli ya Serenity iliyopo Lamadi, nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Chegeni kwamba vijiji vyote vilivyobaki ambavyo ni vijiji 16 vitapatiwa umeme. Awamu ya kwanza ya REA kwenye Jimbo la Busega tulipeleka vijiji 22 na katika Awamu ya II ya REA kwenye Jimbo hilo hilo la Busega tumepeleka vijiji 18 na Awamu ya III ya REA kwenye Jimbo hilo hilo tunapeleka vijiji 19 vyote vilivyobaki. Vijiji hivyo ni pamoja na Ng‟wanangi, Ng‟wanale, Vijiji vya Lamadi vilivyobaki vyote vitawaka umeme kwenye Jimbo la Busega.
Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante.

Name

Dr. Shukuru Jumanne Kawambwa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bagamoyo

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:- Mradi wa REA II ulitarajia kuvipatia umeme vijiji vyote vya Jimbo la Busega na kumekuwepo na kusuasua kwa utekelezaji wa mradi huo jimboni humo:- (a) Je, mpaka sasa ni vijiji vingapi vimepatiwa umeme kupitia mradi huo? (b) Je, ni lini vijiji vilivyobaki vitapatiwa umeme?

Supplementary Question 2

MHE. DKT. SHUKURU J. KAWAMBWA: Mheshimiwa Naibu Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali moja la nyongeza. Kwa kuwa changamoto za Jimbo la Busega zinafanana na zile za Jimbo langu la Bagamoyo, vijiji viwili, Kijiji cha Kongo na Kijiji cha Kondo ambavyo vilikuwa ndani ya mradi wa Umeme Vijijini, Awamu ya II ambapo mpaka hivi sasa havijaanza kuwekewa umeme. Naomba Mheshimiwa Waziri aniambie kuna mkakati gani wa kuwezesha vijiji hivi kuwekewa umeme kabla ya mwaka huu wa fedha kumalizika?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa katika Jimbo la Mheshimiwa Kawambwa kuna vijiji 12 vimebaki ambavyo nataka tu kumhakikishia Mheshimiwa Mbunge kwamba vijiji vyote 12 vilivyobaki tumeviingiza kwenye REA Awamu ya III.
Mheshimiwa Naibu Spika, Kijiji cha Kondo pamoja na maeneo ya jirani ambayo ameyataja ni maeneo ambayo yataanza kuwashiwa baada ya Julai. Mwezi wa Septemba na Oktoba kati ya vijiji ambavyo vitawashiwa umeme kwenye Jimbo la Bagamoyo ni pamoja na Kijiji cha Kondo ambacho amekitaja Mheshimiwa Mbunge.
Mheshimiwa Naibu Spika, naomba nimhakikishie Mheshimiwa Mbunge na namshukuru sana Mheshimiwa Dkt. Kawambwa ameendelea kufuatilia sana mahitaji ya wananchi wa Bagamoyo kuhakikisha kwamba vijiji vyote na kwa vile viko karibu na Dar es Salaam vinapata umeme wa uhakika.
Nimhakikishie Mheshimiwa Dkt. Kawambwa umeme atakaoupata kwenye Vijiji vya Kondo na maeneo ya jirani utakuwa ni umeme ambao utaunganishwa na kilovoti 400 ambao utakuwa haukatiki mara kwa mara.

Name

Emmanuel Papian John

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kiteto

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:- Mradi wa REA II ulitarajia kuvipatia umeme vijiji vyote vya Jimbo la Busega na kumekuwepo na kusuasua kwa utekelezaji wa mradi huo jimboni humo:- (a) Je, mpaka sasa ni vijiji vingapi vimepatiwa umeme kupitia mradi huo? (b) Je, ni lini vijiji vilivyobaki vitapatiwa umeme?

Supplementary Question 3

MHE. EMMANUEL P. JOHN: Mheshimiwa Naibu Spika, ahsante kwa kutuona, kambi mbadala tuko wachache lakini tunajipanga kukuletea orodha yetu upange Baraza la Mawaziri vizuri hapo. (Kicheko/Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, pamoja na majibu mazuri ya Waziri, lakini napenda kuuliza swali la nyongeza. Wilaya ya Kiteto tuna Kata za Songambele, Magungu, Dongo, Raiseli na Sunya zenye jumla ya vijiji karibu 21. Vijiji hivi vyote vilipangiwa kwenye Awamu ya II ya REA. Napenda kuuliza, ni lini tutapatiwa umeme katika awamu hii ili maeneo hayo yaweze kuwa na umeme? Ahsante.

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, napenda kujibu swali moja la nyongeza la Mheshimiwa Papian, Mbunge wa Kiteto, kama ifuatavyo:-
Mheshimiwa Naibu Spika, kwanza, niruhusu tu nisahihishe kidogo alichosema Mheshimiwa Mbunge, vijiji vilivyobaki siyo 21, tunakuongezea, viko 22 Mheshimiwa Mbunge. (Makofi)
Mheshimiwa Naibu Spika, baada ya kusema hayo, napenda sasa nijibu kwamba vijiji vyote ambavyo amevitaja vya Songambele, Dongo, Raiseli pamoja na Sunga vitapata umeme kwenye REA Awamu ya Tatu inayoanza mwezi Julai.

Name

Cosato David Chumi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafinga Mjini

Primary Question

MHE. DKT. RAPHAEL M. CHEGENI aliuliza:- Mradi wa REA II ulitarajia kuvipatia umeme vijiji vyote vya Jimbo la Busega na kumekuwepo na kusuasua kwa utekelezaji wa mradi huo jimboni humo:- (a) Je, mpaka sasa ni vijiji vingapi vimepatiwa umeme kupitia mradi huo? (b) Je, ni lini vijiji vilivyobaki vitapatiwa umeme?

Supplementary Question 4

MHE. COSATO D. CHUMI: Mheshimiwa Naibu Spika, nashukuru kwa kuniona. Kwa kuwa nguzo nyingi za umeme katika nchi hii zinatoka Sao Hill huko kwetu Mafinga ambako pia kuna Kata ya Sao Hill yenye vijiji vya Sao Hill na Mtula. Je, Serikali iko tayari kuenzi Kijiji cha Sao Hill na maeneo jirani ambayo mpaka leo hakuna umeme kwa kufanya upendeleo maalum wa kupatiwa kwa kuwa huko ndiko zinakotoka nguzo?

Name

Dr. Medard Matogolo Kalemani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chato

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI NA MADINI: Mheshimiwa Naibu Spika, ni kweli kabisa eneo la Mafinga linazalisha nguzo nyingi hapa nchini. Wala hakuna haja ya kuwa na upendeleo kwa sababu vijiji vyake vyote vimo kwenye REA Awamu ya III. Eneo la Sao Hill alilosema liko REA Awamu ya Tatu lakini mpaka eneo la Isalanavu pia liko kwenye REA Awamu ya III. Kwa hiyo, maeneo yake yote yatapata umeme kwenye REA Awamu ya III.