Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Zaytun Seif Swai

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZAYTUN S. SWAI aliuliza:- Je, ni lini Daraja la Mto Nduruma litakalounganisha Kata za Mlangarini, Nduruma na Bwawani Wilayani Arumeru litajengwa?

Supplementary Question 1

MHE. ZAYTUN S. SWAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Namshukuru sana Mheshimiwa Naibu Waziri kwa majibu yake mazuri lakini pia kwa niaba ya wananchi wa Wilaya ya Arumeru, naishukuru Serikali kwa kutenga kiasi hiki cha fedha Milioni 70 kwa ajili ya ujenzi wa daraja hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la kwanza, je, ni lini ujenzi wa daraja hili utaanza?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, katika Wilaya ya Ngorongoro, kuna mto, unaitwa Mto Yuhe, mto huu ni hatari sana hasa kipindi cha mvua kwa kuwa watoto wetu wanashindwa kwenda shule upande wa pili vilevile akina Mama wajawazito wanashindwa kwenda kujifungua upande wa pili.

Je, Serikali haioni umuhimu sasa kujenga daraja hili ili kunusuru Maisha ya wananchi hawa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali madogo mawili ya Mheshimiwa Zaytun Seif Swai, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninachoweza kumuahidi Mheshimiwa Mbunge ni kwamba daraja hili litajengwa katika mwaka fedha unaonza na tutalipa kipaumbele kuhakikisha kwamba linakuwa ni moja ya madaraja ambayo yatajengwa haraka iwezekanavyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, jambo la pili, katika Halmashauri ya Ngorongoro ambako kuna daraja la Nyuki ambalo na lenyewe linahitaji kujengwa, ninamuahidi tu Mheshimiwa Mbunge kwamba tutatafuta fedha na tutatuma wataalam wetu waende wakafanye tathmini ili na daraja hilo tulitafutie fedha ili liweze kujengwa, ahsante. (Makofi)