Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

George Natany Malima

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpwapwa

Primary Question

MHE. GEORGE N. MALIMA aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kutatua tatizo la kukatika kwa umeme katika Mji wa Mpwapwa?

Supplementary Question 1

MHE. GEORGE N. MALIMA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, nina maswali mawili ya nyongeza.

Swali la kwanza, pamoja na ujenzi wa njia mpya ya kusambaza umeme bado upatikanaji wa umeme katika Wilaya ya Mpwapwa na hasa maeneo ya vijijini siyo ya kuridhisha. Ni nini tamko la Serikali juu ya kuondoa tatizo hili kabisa? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili; ni lini Serikali itaanza zoezi la kubadilisha nguzo za miti ambazo zimekaa kwa miaka mingi na nyingi zimechakaa na kuanza kuweka nguzo za zege? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa George kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, nianze na la pili kama nilivyosema kwenye jibu la msingi kuanzia mwaka wa fedha ujao, fedha imeshatengwa, itatengwa na kwa ajili ya kuweza kubadilisha nguzo zilizochakaa kuweka za zege, waya na vikombe na maeneo kama hayo.

Mheshimiwa Spika, kwenye swali la kwanza; kwanza nipende kuwaambia Waheshimiwa Wabunge kwamba tarehe moja na tarehe mbili tutaleta habari njema ya faraja kwa Watanzania kutoka kwa Mheshimiwa Rais kupitia bajeti ambayo tutakuja kuisoma hapa ikiwa imetengwa takribani shilingi bilioni 500 kwa ajili ya kuboresha Gridi ya Taifa na maeneo yanayohusika na Gridi ya Taifa.

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, kwenye eneo hili, eneo la Mpwapwa litapata maendeleo ya ziada kwa sababu imetengwa pesa kwa ajili ya kujenga kitu kinaitwa switch station pale Mbande ambacho sasa kitapunguza urefu wa njia ya kutoa umeme Zuzu kwenda mpaka pale na tukishakijenga station pale Mbande itatoka na njia nne mojawapo itakuwa ikienda Mpwapwa. Kwa hiyo, itafikisha umeme kwa urahisi na utakuwa ni umeme mkubwa.