Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza:- Je, fedha za Mfuko wa Jimbo zinaweza kutumika kununulia samani za Ofisi ya Jimbo? Na kama jibu ni hapana, samani hizi zinapaswa kununuliwa na nani?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA: Mheshimiwa Spika, ofisi ya jimbo ni nyenzo muhimu sana katika utekelezaji majukumu ya jimbo. Ofisi nyingi sana za jimbo zimekuwa hazina samani wala vitendea kazi vya ofisi. (Makofi)

Je, Serikali haioni sababu ya kuimarisha ofisi kusudi iwe inafanya kazi zake kikamilifu?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, ni lini Serikali itatoa fedha ya kutosha kuhakikisha Mfuko wa Jimbo unafanya kazi inayostahili jimboni?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela, Mbunge wa Jimbo la Lulindi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, natambua kwamba ofisi nyingi za Wabunge katika majimbo yao hazina samani na tunaziagiza Halmashauri zote nchini kupitia kwa Wakurugenzi kutenga fedha na kuzikamilisha ofisi hizo ili Wabunge waweze kuzitumia. Kwa hiyo, hilo ni agizo kwa Halmashauri na wakurugenzi wote.

Mheshimiwa Spika, jambo la pili amezungumzia kuhusu ongezeko la fedha katika Mfuko wa Jimbo. Nimshukuru sana Rais wa Jamhuri ya Muungano wa Tanzania ambaye ndiyo anasimamia Ilani ya Chama cha Mapinduzi, kwa kuongeza fedha za Mfuko wa Jimbo kwa mwaka huu kutoka shilingi bilioni 11 ambazo zilitumika mpaka shilingi bilioni 15.99 kwa hiyo ni ongezeko kubwa. (Makofi)

Mheshimiwa Spika, kwa hiyo, katika mwaka unaouja huu kutakuwa na ongezeko la fedha za Mfuko wa Jimbo katika majimbo yote nchini. Ahsante.

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza:- Je, fedha za Mfuko wa Jimbo zinaweza kutumika kununulia samani za Ofisi ya Jimbo? Na kama jibu ni hapana, samani hizi zinapaswa kununuliwa na nani?

Supplementary Question 2

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Ni nini kauli ya Serikali kuhusiana na majimbo ambayo hayana ofisi kabisa mpaka sasa ikiwa ni sambamba na kuona kama wanaweza wakaziboresha ofisi ambazo zilijengwa na Bunge na zimechakaa?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Condester Sichalwe, Mbunge wa Jimbo la Momba kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli Wabunge wengi bado hawajafikiwa kupata ofisi kamili katika maeneo yao na Serikali tumekuwa tukitenga bajeti kila mwaka kulingana na upatikanaji wa fedha kuhakikisha tunajenga. Kwa hiyo, ninaamini kabisa kwa muda ambao Serikali imejipangia, ninaamini Wabunge wote watapata ofisi kulingana na hadhi yao. Ahsante sana.

Name

Abeid Ighondo Ramadhani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Singida Kaskazini

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza:- Je, fedha za Mfuko wa Jimbo zinaweza kutumika kununulia samani za Ofisi ya Jimbo? Na kama jibu ni hapana, samani hizi zinapaswa kununuliwa na nani?

Supplementary Question 3

MHE. ABEID R. IGHONDO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa kunipa fursa hii nzuri na muhimu sana, naomba kuuliza swali la nyongeza kwamba muda mwingi Wabunge wako hapa Dodoma kwa shughuli za Kibunge na kama unavyofahamu Mbunge wakati wote anafanya kazi za wananchi. Lakini kwa hapa Dodoma Wabunge hawana ofisi, ofisi zao zimekuwa ni magari, ukienda kwenye gari unakuta amerundika makabrasha mengi ambayo angepaswa kuwa na ofisi ili aweze ku-attend issues mbalimbali za kibunge.

Mheshimiwa Spika, naomba kumuuliza Mheshimiwa Naibu Waziri, Serikali ina mpango gani wa kuwajengea ofisi Wabunge hapa wawapo kwenye shughuli zao za Kibunge?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Abeid Ramadhani Ighondo, Mbunge wa Singida Kaskazini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mheshimiwa Mbunge ameleta mapendekezo, na kila mapendekezo yanahitaji bajeti, tunahitaji kwanza kufanya tathmini na kuona uwezekano wa utekelezaji wa jambo hilo. Kwa hiyo, niseme tu kwamba tumepokea jambo hilo, tutakwenda kulifanyia tathimini, ahsante.