Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 7 Sitting 28 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 239 2022-05-23

Name

Issa Ally Mchungahela

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Lulindi

Primary Question

MHE. ISSA A. MCHUNGAHELA aliuliza:-

Je, fedha za Mfuko wa Jimbo zinaweza kutumika kununulia samani za Ofisi ya Jimbo? Na kama jibu ni hapana, samani hizi zinapaswa kununuliwa na nani?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais -TAMISEMI naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Ally Mchungahela mbunge wa Jimbo wa Lulindi kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Spika, mfuko wa kuchochea maendeleo ya Jimbo ulianzishwa kwa Sheria Na.16 ya mwaka 2009. Fedha za Mfuko wa Jimbo ni mahususi kwa ajili ya kutekeleza miradi ya kijamii iliyoanzishwa na wananchi wa Jimbo husika.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri zilielekezwa kuwapatia Wabunge Ofisi kwa ajili ya shughuli zao ikiwa ni pamoja na samani kulinganaa na uwezo wao wa ukusanyaji mapato yao ya ndani. Nachukua fursa hii kuwasihi Wakurugenzi wa Halmashauri kushirikiana na Wabunge katika kutekeleza majukumu yao.