Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Silvestry Fransis Koka

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibaha Mjini

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza:- Je, ni lini Mji wa Kibaha utakuwa Manispaa ambao kwa sasa ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani?

Supplementary Question 1

MHE. SYLVESTRY F. KOKA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Mkoa wa Pwani ni mkoa mkongwe toka mwaka 1975 na maombi haya yalipelekwa Serikalini hadi kwa Katibu Mkuu Kiongozi toka mwaka 2016 tukiwa ni pamoja na Geita na Kahama.

Mheshimiwa Spika, hawa wenzetu walikwishapata Manispaa, vigezo alivyovizungumzia Mheshimiwa Naibu Waziri vinanipa utata, kwa sababu ukiangalia Manispaa ya Kigamboni wana kata nane, lakini wamepewa Manispaa na hadi sasa vigezo vyote alivyovizungumza hapo Mji wa Kibaha umekwishavitimiza. Sasa je, ni kwanini hatujapatiwa manispaa na ni lini tutapata Manispaa ya Mji wa Kibaha ili tuweze kufikia hadhi tunayostahili?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Sylvestry Francis Koka, Mbunge wa Kibaha Mjini kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu katika swali la msingi, sababu ambayo imechelewesha Halmashauri ya Mji wa Kibaha kupewa hadhi ya Manispaa ni kutokukidhi vigezo ambavyo tumeviainisha na Halmashauri inavifahamu. Kwa hiyo, ndiyo ilikuwa sababu kubwa ambayo imesababisha kuchelewa kwa Halmashauri hiyo.

Lakini lini itapewa hadhi ya Manispaa kwa sasa hivi kwanza Serikali tunajikita katika kuboresha maeneo yaliyopo na naamini kwamba mara baada ya Halmashauri ya Kibaha itakavyokuwa imekidhi vigezo na mamlaka husika kuona haja ya kuipandisha, tutafanya hivyo. Ahsante sana.

Name

Japhet Ngailonga Hasunga (CPA)

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Vwawa

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza:- Je, ni lini Mji wa Kibaha utakuwa Manispaa ambao kwa sasa ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani?

Supplementary Question 2

MHE. JAPHET N. HASUNGA: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, Mji wa Vwawa una Mamlaka Ndogo ya Mji wa Vwawa na Mkoa wa Songwe kwa muda mrefu umekuwa hauna Manispaa.

Je, ni lini Serikali utaupandisha hadhi Mji wa Vwawa ili iwe Manispaa kwa ajili ya kuhudumia Mkoa mpya wa Songwe?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Japhet Hasunga, Mbunge wa Jimbo la Vwawa kama ifuatavyo;

Mheshimiwa Spika, bahati nzuri Mheshimiwa Mbunge anayezungumza anajua kabisa katika eneo alilolitaja na mimi mwenyewe nina interest nalo kwa sababu ni mkoa wangu. Ni moja ya mjadala ambao tumekuwa tukijadili katika vikao vya RCC. Kwa hiyo, ambacho tulishauri Mkoa wa Songwe ni kwamba wafuate zile taratibu ambazo zimeianishwa kuleta maombi, halafu yatapelekwa kwa mamlaka, wakati huo sasa hivi mamlaka imejikita zaidi kwenye kuboresha. Kwa hiyo, tufuate taratibu na baada ya taratibu kukamilika basi tutashauri mamlaka kuona namna bora ya kulitekeleza hili. Ahsante.

Name

Prof. Kitila Alexander Mkumbo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ubungo

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza:- Je, ni lini Mji wa Kibaha utakuwa Manispaa ambao kwa sasa ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani?

Supplementary Question 3

MHE. PROF. KITILA A. MKUMBO: Mheshimiwa Spika, ahsante, je, Serikali haioni haja ya kushughulikia mkanganyiko na mtanziko uliopo kuhusu dhana na mipaka ya Jiji la Dar es Salaam, na kama inaona haja hiyo lini itafanya hivyo?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Profesa Kitila Mkumbo, Mbunge wa Jimbo la Ubungo kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa ameainisha dhana ya kuangalia upya mipaka katika Jiji la Dar es Salaam kutokana na ukubwa wake na umuhimu wake kwa Taifa, sisi tumepokea jambo hilo na tutakwenda kushauriana na timu yetu tuone muda gani tunaweza tukalitekeleza ili tuangalie hivi vigezo ambavyo Mheshimiwa Mbunge ameviainisha ahsante.

Name

Jackson Gedion Kiswaga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kalenga

Primary Question

MHE. SYLVESTRY F. KOKA aliuliza:- Je, ni lini Mji wa Kibaha utakuwa Manispaa ambao kwa sasa ni Makao Makuu ya Mkoa wa Pwani?

Supplementary Question 4

MHE. JACKSON G. KISWAGA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, Halmashauri ya Iringa Vijiji ina majimbo mawili ambayo ni Kalenga pamoja na Isimani na tayari upande wa Isimani mwenzangu alishaomba tupate Halmashauri. Je, ni lini sasa Serikali itatekeleza ombi hili?

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DAVID E. SILINDE): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la nyongeza Mheshimiwa Kiswaga, Mbunge wa Kalenga kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kupandisha hadhi majimbo kuwa Halmashauri yanafuata vigezo, na Halmashauri ambazo hapo nyumba zilikidhi vigezo zilipewa hayo mamlaka. Kwa hiyo, hili lililoombwa na Halmashauri ya Isimani maana yake lipo katika utekelezaji, kwa hiyo, sisi kazi yetu ni kuendelea kupitia vigezo na jambo hili litakapokuwa limekamilika maana yake tutatangaza kupitia sheria ambazo ziko nchini. Ahsante.