Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:- Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Mji Mdogo wa Ngaramtoni?

Supplementary Question 1

MHE. NOAH L. S. MOLLEL: Mheshimiwa Spika, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza:-

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa, eneo linalotumiwa na Kituo Kidogo cha Polisi cha Ngaramtoni linatumiwa tangu mwaka 1984 ambalo liko chini ya Wizara ya Kilimo; je, Serikali kupitia Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi, haioni ni vizuri sasa wakaomba eneo hilo ili waweze kurasimishiwa moja kwa moja badala ya kusema hawana eneo? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili. Kwa kuwa Jeshi la Polisi ndiyo limepewa mamlaka ya kuangalia raia na mali zao: Je, Serikali inaona ni vizuri Askari kukaa kwenye makuti bila nyumba wala Kituo cha Polisi?

Name

Geophrey Mizengo Pinda

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kavuu

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA, NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI: Mheshimiwa Spika, kuhusu suala la Wizara ya Kilimo na Wizara ya Mambo ya Ndani kuzungumzia suala ambalo limetengwa kwa ajili ya shughuli za kilimo na sasa limekosa kibali cha watu wa Polisi kujenga, mazungumzo yanaendelea kati ya Wizara hizi mbili ili kupata kibali cha kuhalalisha hilo eneo ili liweze kujengwa Kituo cha Polisi.

Mheshimiwa Spika, kwenye hili eneo la usalama wa mali za wananchi, Polisi wanatambua umuhimu mkubwa kabisa wa usalama wa wananchi na mali zao, na hivyo basi ndiyo maana msukumo wa mazungumzo unaendelea kati ya hizi taasisi mbili ili kuweza kuhalalisha hiyo eneo na badae kujenga kwa ajili ya usalama wa wananchi.

WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, nilitaka tu nimshauri Mheshimiwa Mbunge wa Arumeru wakakae na Halmashauri yao watafute eneo. Eneo la Wizara ya Kilimo linatumika kwa ajili ya wafanyakazi wa utafiti na pale tuliwapa hifadhi ya muda, watafute eneo lingine. Wizara haitatoa kipande cha ardhi cha uzalishaji wa mbegu. (Makofi)