Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 54 Home Affairs Wizara ya Mambo ya Ndani ya Nchi 713 2023-06-23

Name

Noah Lemburis Saputi Mollel

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Arumeru-Magharibi

Primary Question

MHE. NOAH L. S. MOLLEL aliuliza:-

Je, lini Serikali itajenga Kituo cha Polisi katika Mji Mdogo wa Ngaramtoni?

Name

Eng. Hamad Yussuf Masauni

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kikwajuni

Answer

NAIBU WAZIRI WA ARDHI, NYUMBA NA MAENDELEO YA MAKAZI K.n.y. WAZIRI WA MAMBO YA NDANI YA NCHI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, ahsante. Kwa niaba ya Waziri wa Mambo ya Ndani ya Nchi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Noah Lemburis Saputu Mollel, Mbunge wa Arumeru Magharibi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kwa sasa Polisi haina eneo lililotengwa na Halmashauri kwa ajili ya kujenga Kituo cha Polisi na nyumba za makazi ya Askari. Tunazo taarifa kwamba Mamlaka ya Mji Mdogo wa Ngaramtoni inaendelea na mchakato kwa Halmashauri ya Wilaya ya Arumeru kupata eneo na kutenga kwa ajili ya ujenzi wa ofisi za taasisi za umma ikiwemo Kituo cha Polisi na nyumba za makazi ya Askari. Pindi eneo hilo litakapopatikana Wizara itatenga fedha za ujenzi wa kituo na nyumba za makazi ya Askari kupitia Jeshi la Polisi, ahsante.