Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:- Je, lini Serikali itawalipa mafao yao watumishi waliokuwa Kiwanda cha Magunia Moshi?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER E. MALLEKO: Mheshimiwa Spika, nakushukuru sana kwa majibu ya Serikali, lakini nina ushahidi kupitia kwa Mwenyekiti na Katibu wa Wastaafu hawa, na pia wamepeleka vielelezo vyao kwa Waziri Mheshimiwa Ndalichako kwamba mpaka sasa hawajalipwa stahiki zao;

Je, nini kauli ya Serikali kuweza kuwalipa wastaafu hawa haki zao?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru, hii Kampuni ya Magunia mwaka 1996 baada ya kuona haiendeshwi kwa faida iliamua kuwapumzisha au kuwastaafisha wafanya kazi hao lakini pia mwaka huo huo iliingia mkataba wa hiari kwa watumishi hao baada ya kukubaliana kustaafu kwa maana ya kupata mshahara wa mwezi mmoja, malimbikizo ya likizo, malimbikizo ya mishahara, gharama za kusafirisha mizigo na malimbikizo ya michango mingine baada ya kuingia mkataba wa hiari kwamba watalipwa kama vibarua kwa siku shilingi 1,000 na wangelipwa marupurupu mengine kama kiwanda kingepata faida.

Mheshimiwa Spika, lakini kiwanda hiki baada ya kuona kinashuka faida mwaka 1998 kilibinafsishwa kwenda kwenye kampuni ya TPM ambayo ni Kampuni tanzu ya Mohamed Enterprises. Kwa hiyo, maana yake madai haya nadhani ndio hayo ambayo walidhani watalipwa kama kiwanda hiki kingeweza kupata faida kwa wakati huo, nakushukuru.