Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Industries and Trade Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara 732 2023-06-26

Name

Esther Edwin Maleko

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER E. MALLEKO aliuliza:-

Je, lini Serikali itawalipa mafao yao watumishi waliokuwa Kiwanda cha Magunia Moshi?

Name

Exaud Silaoneka Kigahe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mufindi Kaskazini

Answer

NAIBU WAZIRI WA UWEKEZAJI, VIWANDA NA BIASHARA alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Uwekezaji, Viwanda na Biashara, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Esther Edwin Malleko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, napenda kulifahamisha Bunge lako tukufu kuwa Ofisi ya Msajili wa Hazina ilipokea madai ya waliokuwa wafanyakazi wa Kiwanda cha Magunia Moshi na kuyashughulikia kwa kuunda Kamati ya Uhakiki. Taarifa ya Kamati hiyo ilibainisha kuwa Watumishi hao walishalipwa mafao yao na kujulishwa kwa barua yenye Kumb. Na. CKB.87/406/02/C/80 ya tarehe 3 Mei, 2019. Hata hivyo, pamoja na kuwajibu, wadai wameendelea kuandika barua kwenda kwenye Taasisi mbalimbali za Serikali kuwasilisha malalamiko yao; na kwa upande wetu tumekuwa tukiwajibu na kutoa ufafanuzi kuwa walalamikaji hao walilipwa stahiki zao ipasavyo.