Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Busanda ili kiweze kutoa elimu ya uchimbaji madini na hatimaye kuongeza tija kiuchumi?

Supplementary Question 1

MHE. TUMAINI B. MAGESSA: Mheshimiwa Spika, pamoja na majibu mazuri ya Serikali nina maswali mawili ya nyongeza. Swali la kwanza, kwa kuzingatia idadi kubwa ya wananchi katika Jimbo la Busanda ambayo ni takribani laki saba.

Je, Serikali haioni kwamba kuna umuhimu wa kujenga Chuo cha VETA kwenye maeneo hayo?

Mheshimiwa Spika, lakini swali la pili, kwa vile jibu la msingi linathibitisha kwamba Chuo hicho kimejengwa Geita Mji na sisi tuko Geita Vijijini.

Je, Serikali haioni umuhimu wa kujenga Chuo cha VETA Geita vijijini badala ya Geita Mji?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Tumaini Magessa kwa pamoja kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, kama nilivyokwisha eleza kwenye maswali ya msingi kwamba tuna chuo ambacho tumejenga pale Geita; lakini ni sera ya Serikali kwa Awamu hii ya Kwanza kujenga vyuo hivi katika ngazi za Wilaya, na tutakapokuwa tumekamilisha ujenzi huu katika ngazi za Wilaya ambapo mnafahamu Waheshimiwa Wabunge wote katika mwaka huu Mheshimiwa Rais ametoa zaidi ya bilioni 100 kwa ajili ya ujenzi wa vyuo hivyo katika zile Wilaya ambazo tumekosa na katika Mkoa mmoja wa Songwe ambao ulikuwa hauna chuo hiki.

Mheshimiwa Spika, sasa baada ya kukamilisha awamu hii, tutafanya tathmini na kuona maeneo yapi yana idadi kubwa ya wananchi au ya wakazi na kuweza kuangalia namna gani tunaweza tukasogeza huduma hii karibu na maeneo hayo likiwemo na hili eneo la Busanda. Vile vile tunaweza kuzingatia katika Halmashauri au Wilaya ambazo zina Majimbo au Halmashauri zaidi ya moja kuweza kuwafikishia huduma hii katika Halmashauri hizo kulingana na upatikanaji wa fedha lakini vile vile na kukidhi kwa sifa za maeneo hayo.