Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Education, Science,Technology and Vocational Training, Wizara ya Elimu, Sayansi na Teknolojia 729 2023-06-26

Name

Tumaini Bryceson Magessa

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busanda

Primary Question

MHE. TUMAINI B. MAGESSA aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Chuo cha VETA Busanda ili kiweze kutoa elimu ya uchimbaji madini na hatimaye kuongeza tija kiuchumi?

Name

Omary Juma Kipanga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mafia

Answer

NAIBU WAZIRI WA ELIMU, SAYANSI NA TEKNOLOJIA alijibu: -

Mheshimiwa Spika, ahsante sana. Kwa niaba ya Waziri wa Elimu, Sayansi na Teknolojia, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Tumaini Bryceson Magessa, Mbunge wa Busanda, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatambua umuhimu wa Vyuo vya Ufundi Stadi nchini ili kuwapatia ujuzi wananchi utakaowawezesha kutekeleza shughuli za kiuchumi katika maeneo yao. Katika mwaka wa fedha 2021/2022 Serikali ilipeleka fedha kiasi cha shilingi za Kitanzania bilioni 4.2 kwa ajili ya ujenzi wa Chuo cha Ufundi Stadi cha Mkoa wa Geita kilichojengwa katika Halmashauri ya Mji wa Geita. Ujenzi wa Chuo hiki upo katika hatua za mwisho za ukamilishaji wa ujenzi.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa Halmashauri ya Busanda ipo katika Wilaya ya Geita, Serikali inaomba wananchi wa Busanda kutumia chuo hicho cha Mkoa kilichojengwa katika Wilaya ya Geita ambapo elimu ya uchimbaji wa madini itatolewa.