Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: - Je, Serikali ipo tayari kutenga sehemu kwa ajili ya shule ya sekondari katika Pori Tengefu Mabwepande lililopo Kibesa, Jimbo la Kibamba?

Supplementary Question 1

MHE. ISSA J. MTEMVU: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu mazuri sana ya Serikali, naomba niulize swali moja tu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, kwa kuwa wananchi wale wa Kibesa sehemu ya Mpiji Magohe, wanatembea kilometa 8.2 kufuata sekodari pale Mpiji Center.

Je, Mheshimiwa Waziri utakuwa tayari kuja ili uone ushuhudie ile adha ya wananchi wale wanayopata ili mimi na wewe tushirikiane kufuata taratibu, sheria na miongozo ili waweze kupewa hilo eneo katika sehemu ya hifadhi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Spika, ahsante. Naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Jimbo la Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, eneo nalifahamu na nilishafanya ziara mara nyingi. Na ukiangalia jibu la msingi, nimejibu kiufasaha, kwamba maeneo ni machache na Jiji la Dar es Salaam linaendelea kukua, tukikosa maeneo ya kupumulia watu wanazidi kuongezeka lakini tukaendelea kunyima maeneo ambayo angalau watu wanapopumua…

Mheshimiwa Spika, kama nilivyojibu kwenye jibu langu la msingi, ni kwamba haya maeneo tunayatenga, si kwa sababu tu ya msuala ya utalii. Serikali inatambua kwamba kuna umuhimu wa ku-balance ikolojia. Kuna maeneo kama Pugu tumetenga ile Kazimzumbwi na upande wa Kibamba na huku kaskazini tumetenga hili Pori la Mambwepande. Lakini lengo ni kuifanya Dar es Salaam ipate maeneo ya kupumulia kwa sababu watu wanazidi kuongezeka.

Mheshimiwa Spika, kama ambavyo nimejibu, kilometa za mradba katika eneo hili ni 15 tu, ni chace sana. tulitamani hata ziwe nyingi. Sasa tukiendelea kuzimega tena, kwanza tunawafanya wana-Dar es Salaam wakose pa kupumlia; cha pili, ni kufanya sasa maeneo mengi ambayo tunajitahidi kuyatunza kwa ajili ya ku-balance ikolojia yatakuwa yanazidi kupungua zaidi.