Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 725 2023-06-26

Name

Issa Jumanne Mtemvu

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kibamba

Primary Question

MHE. ISSA J. MTEMVU aliuliza: -

Je, Serikali ipo tayari kutenga sehemu kwa ajili ya shule ya sekondari katika Pori Tengefu Mabwepande lililopo Kibesa, Jimbo la Kibamba?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Issa Jumanne Mtemvu, Mbunge wa Jimbo la Kibamba, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Pori la Akiba Pande lenye ukubwa wa kilometa za mraba 15.39 limetengwa kwa sababu kuu zifuatazo; kufyonza hewa chafu (carbon sink) inayotokana na shughuli za kibinadamu ili isisababishe madhara kwa wakazi wa Jiji la Dar es Salaam, na kuhifadhi mimea na viumbe hai wengine kama wadudu na wanyamapori ambao ni muhimu katika kuhakikisha mifumo ikolojia ya maeneo husika inaimarika na kutoa huduma za kiikolojia. Aidha, eneo hilo pia linatumika kwa shughuli za utalii na kwa sasa Serikali inaendelea kuboresha miundombinu ya utalii ndani ya pori hilo ili kuvutia watalii wengi na kuongeza mapato yatokanayo na utalii.

Mheshimiwa Spika, kutokana na sababu hizo na kuzingatia kwamba eneo hilo ni dogo, Wizara haioni busara kuendelea kumega eneo hilo kwa shughuli za kijamii.