Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha zoezi la kuwasha umeme kwenye vijiji vilivyosalia katika Jimbo la Momba?

Supplementary Question 1

MHE. CONDESTER M. SICHALWE: Mheshimiwa Spika, nakushukuru na nimesikia majibu ya Serikali, naomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, katika vijiji ambavyo vimesalia nguzo zimepelekwa maeneo hayo na zimeachwa kwa muda mrefu na wananchi wamechukulia kwamba nguzo hizi zimetelekezwa; je, ni lini shughuli itaendelea kwa ukamilifu kuona nguzo zinasimikwa na vijiji hivi vinawashwa umeme?

Mheshimiwa Spika, swali la pili, katika vijiji ambavyo vimepatiwa umeme, umeme umekuwa sio toshelevu hivyo wawekezaji kuvunjika moyo kushindwa kufanya shughuli zao zinazohitaji umeme mkubwa; je, ni lini Serikali itatuwekea capacitor au booster kwenye vijiji hivyo ikiwa ni sambamba na kujenga kituo cha umeme mkubwa kwenye Kata ya Nkangamo?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, naomba kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Condester kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi, kwenye hivi vijiji 20 ambavyo vimebaki kazi katika hatua mbalimbali zinaendelea. Mkandarasi anayefanya kazi katika Mkoa wa Songwe kwa ujumla anaitwa DEM, ni mkandarasi ambaye anaendelea kutekeleza kazi yake na katika mkoa yuko zaidi ya asilimia 80.

Mheshimiwa Spika, nimhakikishie Mheshimiwa Condester kwamba kabla ya Disemba mwaka huu maeneo yote yatakuwa yamepatiwa umeme kwa sababu hatua ni moja moja kwenye maeneo tofauti tofauti, lakini nimhakikishe kwamba vifaa hivi ambavyo vimewekwa katika maeneo hayo ni vile ambavyo vitakuja kutumika katika maeneo hayo, havijatelekezwa na vitatumika kufanya kazi ambazo zinastahili kufanyika.

Mheshimiwa Spika, katika swali la pili, ni kweli kwamba kumekuwa kuna upungufu wa umeme katika maeneo mbalimbali na ni kwa sababu ya mahitaji kuwa makubwa na sisi kama Wizara ya Nishati tunaendelea kufanya assessment, na katika awamu hiiya kwanza ya Mradi wetu wa Gridi Imara tumetenga vituo vya kupoza umeme 15 katika maeneo mbalimbali kulingana na mahitaji makubwa yalivyo. Namhakikishia Mheshimiwa Condester pia kwamba nia ya Serikali ni kuhakikisha ifikapo angalau mwaka 2030 kila Wilaya iwe imepata kituo cha kupoza umeme kulingana na uwezekano wa upatikanaji wa fedha kutoka Serikalini, ili kuhakikisha kwamba tunafikisha umeme wa kutosheleza katika maeneo yote, lakini nimuombe baada ya hapa tutawasiliana ili tuone hilo eeo ambalo ni mahususi analolisema lina upungufu sana wa umeme saa hizi tulichukulie hatua mahususi na za haraka zaidi, ili kuwavutia wawekezaji zaidi.

Name

Husna Juma Sekiboko

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha zoezi la kuwasha umeme kwenye vijiji vilivyosalia katika Jimbo la Momba?

Supplementary Question 2

MHE. HUSNA J. SEKIBOKO: Mheshimiwa Spika, nashukuru sana kwa nafasi hii.

Mheshimiwa Spika, wananchi wa Kijiji cha Mgwashi, Kata ya Lukozi wamekata tamaa kabisa na upatikanaji wa umeme baada ya kuwa wameahidiwa mara nyingi kwamba umeme unakwenda kuwashwa kwenye Kijiji chao. Naomba commitment ya Serikali, ni lini hasa Serikali itaenda kuwasha umeme katika Kijiji cha Mgwashi? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, kama nilivyosema kwenye jibu la msingi nak ama ambavyo tumeeleza mara zote hapa, kabla ya Disemba mwaka 2023 vijiji vyote ambavyo havina umeme vitakuwa vimewashiwa umeme na Kijiji cha Mgwashi pia kitakuwa ni kimojawapo kitakachowashiwa umeme.

Name

Ally Anyigulile Jumbe

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Kyela

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha zoezi la kuwasha umeme kwenye vijiji vilivyosalia katika Jimbo la Momba?

Supplementary Question 3

MHE. ALLY A. J. M. JUMBE: Mheshimiwa Spika, Serikali iliahidi kwamba kufika tarehe 30 Juni, wananchi wa Ikomba watakuwa wamefikishiwa umeme wa REA, leo ninavyoongea hata nguzo zilizokuwepo kule wameziondoa; je, Serikali haioni kwamba haiwatendei haki wananchi wa Ikombe? (Makofi)

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Spika, nimuahidi Mheshimiwa Jumbe kwamba, Mradi wa REA III, Round II unatakiwa kukamilika ifikapo Disemba, 2023. Yale maeneo ambayo bado hayajakamilika na nguzo pengine zimeenda zimepelekwa sehemu nyingine zitarudishwa zitapelekwa hapa, lakini nia ni kuhakikisha kwamba ifikapo mwezi Disemba, 2023 kila kijiji kimepata umeme na wananchi waweze kupata huduma hiyo, kwa hiyo, ahadi hiyo tutaitekeleza kwa kadri ilivyotolewa.