Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 723 2023-06-26

Name

Condester Michael Sichalwe

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Momba

Primary Question

MHE. CONDESTER M. SICHALWE aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani wa kukamilisha zoezi la kuwasha umeme kwenye vijiji vilivyosalia katika Jimbo la Momba?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Condester Michael Sichalwe, Mbunge wa Momba, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali inatekeleza Mradi wa Kusambaza Umeme Vijijini Awamu ya Tatu, Mzunguko wa Pili ambapo vijiji vyote visivyo na umeme vitafikiwa na huduma ya umeme. Mradi huu unahudumia vijiji 42 vilivyosalia katika Jimbo la Momba ambapo kati ya hivyo vijiji 22 vimekwishawashiwa umeme na vijiji 20 kazi mbalimbali zinaendelea. Mradi huu unatarajiwa kukamilika ifikapo mwezi Disemba, 2023. Nakushukuru.