Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itavigawa Vijiji vya Makangara, Mkomazi, Mkalamo, Mwenga, Kwemasimba, Mkwajuni, Sekioga na Bungu?

Supplementary Question 1

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA: Mheshimiwa Spika, nakushukuru. Pamoja na majibu ya Serikali ambayo ni ya jumla sana, naomba kuuliza swali dogo moja tu la nyongeza.

Mheshimiwa Spika, maeneo ambayo yanataka kumegwa kutoka kwenye vijiji ambavyo nimevitaja ni maeneo makubwa na tayari pande zote za vijiji zina miundombinu muhimu kama vile shule na zahanati na kuna ahadi ya viongozi wakiwemo Mheshimiwa Waziri Mkuu. Ni lini, Serikali itavigawa vijiji hivi ili kurahisisha shughuli za maendeleo na kuwasogezea wananchi huduma?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, kama ambavyo ametoka kusema Mheshimiwa Mnzava hapa, kwamba kama maeneo haya tayari yana miundombinu muhimu kwa ajili ya kukidhi vigezo vile vinavyotakiwa kuwepo kwa ajili ya kugawa vijiji vipya, basi tutatuma timu katika maeneo hayo ili kuweza kufanya tathmini hiyo na kisha baada ya thathmini hiyo tutakaa na wataalam pale kwetu Ofisi ya Rais - TAMISEMI na kisha kuona ni namna gani tunaweza kuwapatia vijiji hivyo kwa sababu tayari maeneo hayo yameshakidhi vigezo vile vinavyotajwa kwa mujibu wa sheria na kanuni zilizopo.

Name

Francis Isack Mtinga

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Iramba Mashariki

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: - Je, lini Serikali itavigawa Vijiji vya Makangara, Mkomazi, Mkalamo, Mwenga, Kwemasimba, Mkwajuni, Sekioga na Bungu?

Supplementary Question 2

MHE. FRANCIS I. MTINGA: Mheshimiwa Spika, ahsante kwa kuniona. Ni lini Serikali itaigawa Kata ya Mwangeza ambayo ina idadi ya watu 32,000 na hivyo huduma ni ngumu sana kwa wananchi?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Spika, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mtinga ni kwamba, kwa sasa Serikali imeweka kipaumbele katika kuboresha maeneo yale ambayo tayari yameshagawanywa, kwa sababu tutapogawanya Kata mpya maana yake itabidi kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa sekondari nyingine, ambapo nyinyi ni mashahidi Waheshimiwa Wabunge humu ndani, kwa sasa Serikali inapeleka fedha katika kila Halmashauri kwa ajili ya ujenzi wa shule mpya za sekondari na hivyo tunaendelea kutafuta fedha kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya afya vya kimkakati kote nchini.

Mheshimiwa Spika, hivyo basi tukimaliza kupeleka vitu vya msingi katika Kata zilizopo ambazo ni mpya zilianzishwa mwaka 2010 na nyingine zilianzishwa mwaka 2015 Serikali ikikamilisha katika kuweka mazingira bora katika maeneo hayo tutaangalia vilevile katika Kata ambayo ameitaja Mheshimiwa Mbunge.