Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 55 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 721 2023-06-26

Name

Timotheo Paul Mnzava

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Korogwe Vijijini

Primary Question

MHE. TIMOTHEO P. MNZAVA aliuliza: -

Je, lini Serikali itavigawa Vijiji vya Makangara, Mkomazi, Mkalamo, Mwenga, Kwemasimba, Mkwajuni, Sekioga na Bungu?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEOGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais, TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Timotheo Paul Mnzava, Mbunge wa Korogwe Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, uanzishaji wa maeneo ya utawala hutekelezwa kwa mujibu wa Sheria za Serikali za Mitaa Sura Na. 287 na Na. 288 pamoja na mwongozo wa uanzishaji wa maeneo ya utawala wa mwaka 2014 ambao umeanisha utaratibu na vigezo vinavyopaswa kufuatwa. Miongoni mwa vigezo hivyo ni uwezo wa Halmashauri kujitegemea katika bajeti ya uendeshaji kutokana na mapato ya ndani, uwezo wa kutoa huduma za kijamii na kiutawala, upatikanaji wa huduma za mawasiliano ya simu na uwepo wa huduma ya umeme.

Mheshimiwa Spika, Serikali imetoa kipaumbele kuboresha na kukamilisha miundombinu msingi kwenye maeneo yaliyoanzishwa ili yaweze kutoa huduma kwa jamii na baadae kuendelea na maeneo mengine kwa kufuata taratibu na vigezo vilivyoainishwa.