Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kupitia SIDO kutoa mashine ndogo na rahisi kwa vikundi vya wanawake vya ubanguaji korosho Mkoani Mtwara?

Supplementary Question 1

MHE. AGNES E. HOKORORO: Mheshimiwa Spika, ahsante, pamoja na majibu mazuri ya Serikali naomba kuuliza maswali mawili madogo ya nyongeza.

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuongeza ajira zaidi kwa wanawake kwa kuwa hawa 241 bado ni wachache katika zao la korosho Mkoani Mtwara? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, swali la pili, kwa kuwa Mkoa wa Mtwara haujapata block farming katika zao la korosho; Serikali ina mkakati gani wa kuwatengenezea vijana programu mahsusi katika mnyororo wa thamani kwa zao la korosho ili vijana wa Mtawara waweze kunufaika na project za Wizara ya Kilimo? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, mkakati wa Serikali ni kuhakikisha ifikapo mwaka 2025 zaidi ya asilimia 60 ya korosho inayozalishwa ndani iweze kubanguliwa na hivyo kutunza ajira zetu za akina mama na vijana kuliko ilivyo hivi sasa ambavyo ajira nyingi zinasafirishwa nje ya nchi.

Mheshimiwa Spika, pamoja na mkakati huo pia hivi sasa tunatazamia kuanza maandalizi ya ujenzi wa industrial park katika eneo la Nanyamba ambako tutajenga viwanda vya ubanguaji wa korosho na zaidi ya tani 300,000 zitabanguliwa na akina mama na vijana hawa wataunganishwa katika mfumo uliyosehemu pia ya ajira yao na kutatua changamoto hiyo ya korosho kutokubanguliwa.

Mheshimiwa Spika, la pili la kuhusu mashamba makubwa ya pamoja, utaratibu huo chini ya Bodi ya Korosho umekwisha kuanza na umeanza kuwapanga wakulima katika mashamba makubwa na ninaamini kabisa kwamba wakulima wa Mtwara wakiwemo akina mama na vijana watanufaika na mpango huo mkubwa sambamba na mkakati mkubwa wa ujenzi wa miundombinu ya skimu za umwagiliaji katika mabonde ambayo pia tutayaweka maeneo kwa ajili ya umwagiliaji wa kilimo cha korosho na hakika pia kupitia utaratibu huu akina mama na vijana wa Mkoa wa Mtwara watanufaika katika mfumo wa mashamba makubwa ya pamoja.

Name

Shally Josepha Raymond

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:- Je, Serikali ina mpango gani kupitia SIDO kutoa mashine ndogo na rahisi kwa vikundi vya wanawake vya ubanguaji korosho Mkoani Mtwara?

Supplementary Question 2

MHE. SHALLY J. RAYMOND: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, kwa kuwa uhitaji wa kuongeza thamani kwenye zao la korosho Mtwara unafanana kabisa na uhitaji wa kuongeza thamani kwenye zao la ndizi Kilimanjaro.

Je Serikali ina mpango gani kuwasaidia wanawake wa Mkoa wa Kilimanjaro mashine hizo za SIDO ili waweze kuongeza thamani kwenye zao la ndizi kwa kutengeneza clips na vitu vingine vinavyotokana na ndizi? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Spika, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni dhamira ya Serikali kuhakikisha ya kwamba mazao yetu ya kilimo yanachakatwa ili kuongeza thamani na vilevile kuongeza kipato kwa wazalishaji au wakulima wetu na tupo katika mkakati wa pamoja sisi pamoja na Wizara ya Viwanda, Biashara na Uwekezaji kuhakikisha kwamba tunatumia taasisi zetu za ndani kama CAMARTEC, TIRDO na SIDO kutengeneza mashine ndogo ndogo na ambazo zitakuwa zina bei rahisi ili kuweza kuwafikia wakulima wengi zaidi kuongeza thamani ya mazao haya.

Kwa hiyo, nimuondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba wakulima pia wa ndizi wa Mkoa wa Kilimanjaro hasa akina mama na wenyewe pia tutawaweka na kuhakikisha kwamba na wenyewe wanafanya kazi ya uchakataji.