Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 57 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 758 2023-06-28

Name

Agnes Elias Hokororo

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. AGNES E. HOKORORO aliuliza:-

Je, Serikali ina mpango gani kupitia SIDO kutoa mashine ndogo na rahisi kwa vikundi vya wanawake vya ubanguaji korosho Mkoani Mtwara?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo naomba kujibu swali la Mheshimiwa Agnes Elias Hokororo, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Bodi ya Korosho imeanza kuchukua hatua stahiki ili kuhakikisha korosho zote zinazozalishwa nchini zinabanguliwa na kuuzwa nje ya nchi zikiwa zimebanguliwa (kernel). Lengo kuu ni kuongeza thamani katika zao, kipato kwa wakulima na ajira kwa vijana na wanawake.

Mheshimiwa Spika, aidha, katika kutekeleza mpango huo Serikali imenunua mashine 100 za kubangua korosho zilizotengenezwa na wajasiriamali walio chini ya mwamvuli wa SIDO na kuzigawa kwa vikundi 22; vikundi 15 vya Mkoa wa Mtwara na Lindi vikundi saba ambapo jumla ya wanawake 241 na wanaume 18 wamenufaika.

Mheshimiwa Spika, Serikali kupitia Bodi ya Korosho Tanzania inaendelea kuhamasisha watengenezaji na wauzaji wa mashine za kubangua korosho ikiwa ni pamoja na SIDO, CAMARTEC na TIRDO ili kurahisisha upatikanaji wa mashine hizo.