Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: - Je, ni lini Mamlaka ya Viwanja vya Ndege itaruhusiwa kukusanya na kutumia passenger service charge kuboresha viwanja vya ndege ?

Supplementary Question 1

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE: Mheshimiwa Spika, ahsante sana, pamoja na majibu mazuri ya Serikali ninaomba kuuliza maswali mawili ya nyongeza kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, moja, kwa kuwa Bunge lilishazimia Kampuni ya KADCO kurejeshwa chini ya Mamlaka ya Viwanja vya Ndege, sasa ni lini Serikali itafanya hivyo kutii Azimio la Bunge? (Makofi)

Mheshimiwa Spika, sawali la pili, ni lini sasa Serikali itakamilisha mchakato wa sheria kuipa Mamlaka ya Viwanja vya Ndege kusimamia kuendeleza viwanja vya ndege nchini?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) : Mheshimiwa Spika, napenda kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Engineer Mwanaisha Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, ni kweli mwezi Novemba, 2022 Bunge lako tukufu liliazimia KADCO kuwepo chini ya viwanja vya ndege nchini. Swali la pili, uanzishwaji wa Sheria ya Viwanja vya Ndege nchini. Ninaomba nijibu yote kwa pamoja.

Mheshimiwa Spika, mara baada ya Bunge lako tukufu kuazimia kwamba lazima KADCO iwe chini ya TAA, hatua ambayo Serikali tumefanya mpaka sasa, kwanza tuliielekeza TAA kuandaa draft kwa maana ya mapendekezo ya sheria, na tayari draft hiyo imeshakuja Wizarani na tuliyapitia, kuyaboresha na kuyapeleka kwa Mwanasheria Mkuu ili kupata idhini au kibali. Tayari Mwanasheria Mkuu alishatoa kibali na sasa ipo ngazi ya wataalamu kwa maana ya Makatibu Wakuu.

Mheshimiwa Spika, tunategemea tutaomba kibali kwenye Baraza la Mawaziri ambalo litafanyika mwezi wa saba na hatimaye matarajio ya Wizara mwezi wa tisa sheria hiyo iweze kuwasilishwa hapa Bungeni. Sheria hii itaweka msingi wa viwanja vyote vya ndege nchini kuwa chini ya TAA.

Mheshimiwa Spika, sasa hivi kuna viwanja vya ndege vilivyo chini ya TANAPA, kuna viwanja vingine viko chini ya mamlaka nyingine za Serikali. Sasa sheria hii itaweka msingi kwamba viwanja vyote vya Serikali hapa nchini viwe chini ya TAA, ahsante.