Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 57 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 755 2023-06-28

Name

Mwanaisha Ng'anzi Ulenge

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ENG. MWANAISHA N. ULENGE aliuliza: -

Je, ni lini Mamlaka ya Viwanja vya Ndege itaruhusiwa kukusanya na kutumia passenger service charge kuboresha viwanja vya ndege ?

Name

Atupele Fredy Mwakibete

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Busokelo

Answer

NAIBU WAZIRI WA UCHUKUZI (MHE. ATUPELE F. MWAKIBETE) alijibu:-

Mheshimiwa Spika, Kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Engineer Mwanaisha Ng’anzi Ulenge, Mbunge wa Viti Maalum kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Spika, Mamlaka ya Viwanja vya Ndege (TAA) imewekewa utaratibu wa kukusanya moja kwa moja ada za kutua na maegesho ya ndege; ada ya usalama (security fee); tozo za ukodishaji wa ofisi, karakana, majengo ya kuhifadhia mizigo, migahawa na maduka; tozo za maegesho ya magari, na tozo za mabango. Aidha, Sheria ya Huduma za Viwanja vya Ndege (The Airport Service Charge Act) Sura ya 365 inaipa Mamlaka ya Mapato Tanzania (TRA) jukumu la kukusanya tozo kwa abiria wanaosafiri kupitia viwanja vya ndege (passenger service charge) na kuwasilisha Hazina.

Mheshimiwa Spika, fedha zinazokusanywa na TRA kutoka kwa abiria na kuwasilishwa Hazina zinatumika kuendeleza miundombinu ya viwanja vya ndege nchini pamoja na kulipa mishahara ya watumishi, matumizi ya uendeshaji wa TAA na kufanya matengenezo ya viwanja. Aidha, Serikali hutoa fedha kila mwaka kwa ajili ya ujenzi na ukarabati wa miundombinu ya viwanja vya ndege, ahsante.