Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka nishati ya gesi asilia katika vijiji vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro ili kupunguza matumizi ya kuni?

Supplementary Question 1

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru na niishukuru Serikali kwa majibu ya kutia moyo. Nina maswali mawili ya nyongeza: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwenye kaya nyingi kule Uchaggani na maeneo mengi ya Tanzania, kaya zote zina wanyama kama vile ng’ombe, mbuzi na kondoo: -

Je, Serikali ina mkakati gani wa kuwekeza kwenye gesi endelevu kwa mfano tupate nishati ya kupikia na kuwasha taa kutoka kwenye kinyesi cha wanyama ili kuzuia matumizi ya kuni?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili; je, Serikali haioni umuhimu wa kuhamasisha wananchi watumie majiko bunifu na mikaa ya tofali inayotokana na pumba za mpunga na masalia mengine ya mimea ili kupunguza matumizi ya kukata miti na kuwapatia wananchi nishati?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali mawili ya nyongeza ya Mheshimiwa Profesa Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza namshukuru Mheshimiwa Prof. Ndakidemi, kwa ufuatiliaji wa eneo hili ambalo ni eneo jipya ambalo Serikali imetilia mkazo kuhakikisha kwamba tunatumia nishati safi, hasa ya kupikia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba nijibu maswali yote mawili kwa pamoja kwa kutoa maelezo yafuatayo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, tangu mwaka jana Mheshimiwa Rais alizindua mjadala wa Kitaifa wa nishati safi ya kupikia, na ni azma ya Serikali kupitia Wizara ya Nishati, mmeona tukijikimu kuelekea sasa kwenye nishati safi ya kupikia. Na katika eneo hili tunahamasisha utumiaji wa gesi ya mitungu, lakini gesi asilia, lakini pia maeneo mengine waliyoyasema ya kutumia biomass, kwa maana vinyesi vya wanyama, na mikaa hii ambayo ni ya kutengeneza ambayo haitoi moshi sana.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Wizara ya Nishati kupitia REA inawezesha na ku-facilitate wale wagunduzi na watengenezaji wa majiko banifu na hii mikaa ya asili, kama mlivyotembelea mabanda yetu mliwakuta pale wabunifu wa namna hiyo. Kwenye Serikali itakuwa siyo rahisi sana kutumia nguvu ya Serikali kuzalisha umeme au gesi ya kupikia kwa pesa ya Serikali kutumia vinyesi vya wanyama na maeneo mengine. Kwa hiyo, Serikali inatoa pesa lakini pia tunapata mifuko mingine kama Green Fund ambayo ina-facilitate wananchi na wawekezaji binafsi katika maeneo hayo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nimhakikishie Mheshimiwa Prof. Ndakidemi kwamba tutaendelea kusimamia eneo hili kuhakikisha kwamba tunawawezesha wananchi na kuwapa fedha za mitaji ili waendelee kupata vitendea kazi vya maeneo hayo kuweza kuzalisha gesi asilia na kuweza kutumika katika kuwasha umeme, lakini pia katika nishati safi ya kupikia. (Makofi)

Name

Mariamu Nassoro Kisangi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka nishati ya gesi asilia katika vijiji vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro ili kupunguza matumizi ya kuni?

Supplementary Question 2

MHE. MARIAM N. KISANGI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuwa gesi asilia ina gharama ndogo sana kuliko ile gesi ya mitungi, na kwa kuwa Serikali imeshawekeza katika Mkoa wa Dar es Salaam, maeneo ya Mikocheni na Msasani: -

Je, Serikali ina mpango gani sasa kuhakikisha gesi hiyo asilia inapelekwa katika wilaya zote za Mkoa wa Dar es Salaam?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Mariam Nassoro Kisangi, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali inayo azma ya dhati kabisa, na katika bajeti ya mwaka huu imetenga pesa kwa ajili ya kuendelea kupanua miundombinu ya upelekaji wa gesi asilia katika maeneo mbalimbali nchini.

Mheshimiwa Mwenyekiti, uunganishaji wa gesi asilia kwa mteja mmoja nyumbani kwake kwa miundombinu tuliyokuwa nayo sisi ina-range kutoka milioni mbili mpaka sita kwa mteja mmoja. Kwa hiyo, Serikali inaendelea kutafuta uwezeshaji wa kuweza kutambaza mabomba mengi zaidi katika maeneo yetu na kufikisha miundombinu hii ya gesi ili wananchi walio wengi zaidi waweze kupata nishati hii na kuitumia kwenye maeneo yao.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika eneo hili tumefungua milango kwa wawekezaji wengi zaidi ili waje washirikiane pamoja na Serikali kuweza kuendelea kusambaza gesi asilia katika Mkoa wa Dar es Salaam. Lakini tunao mpango wa kuleta mpaka Mkoa wa Dodoma na maeneo mengine ambayo wanaendelea kutumia na kuhitaji nishati ya gesi.

Name

Esther Lukago Midimu

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka nishati ya gesi asilia katika vijiji vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro ili kupunguza matumizi ya kuni?

Supplementary Question 3

MHE. ESTHER L. MIDIMU: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mikoa tisa iliyokabiliwa na ukame, Mkoa wa Simiyu ni mmoja wapo, je, Serikali ina mpango gani kupeleka gesi asilia?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Esther Lukago Midimu, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama nilivyojibu kwenye swali la msingi, gesi asilia inaweza kupelekwa kwa njia ya mabomba au kwa kugandamizwa na kuwekwa kwenye magari.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa tuko katika Mikoa ya Dar es Salaam, Pwani, Mtwara na Lindi, lakini mipango iliyopo Serikalini ni kusogea sasa kuja katika Mikoa ya Bara kwa ndani zaidi kwa njia zote hizo, kwa maana ya kuwekeza katika kuleta kwa malori na treni au kuleta kwa bomba.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika Mkoa wa Simiyu na maeneo ya Mkoa wa Mwanza ambapo kuna watumiaji wengi wanahitaji gesi kwenye viwanda, mipango ya Serikali ni kuendelea kupanua wigo wa upelekaji wa gesi katika maeneo hayo. Mkoa wa Simiyu nao pia utafikiwa pale ambapo uwezeshaji utakuwa umekamilika.

Name

Aida Joseph Khenani

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Nkasi Kaskazini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: - Je, kuna mpango gani wa kupeleka nishati ya gesi asilia katika vijiji vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro ili kupunguza matumizi ya kuni?

Supplementary Question 4

MHE. AIDA J. KHENANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kunipatia nafasi niulize swali dogo la nyongeza.

Mheshimiwa Mwenyekiti, wananchi wengi wa vijijini wanatumia kuni na mkaa kwa sababu ndiyo nishati inayopatikana kwa wepesi kwenye maeneo yao: -

Serikali ina mkakati gani wa kupeleka nishati mbadala ambayo ni gesi asilia ili iendane na nguvu tunayotumia kupiga marufuku kutumia kuni na mkaa?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Aida Joseph Khenani, Mbunge wa Nkasi Kaskazini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, nakubaliana na Mheshimiwa Mbunge kabisa kwamba watu wengi wa vijijini wanatumia mkaa na kuni katika hasa nishati ya kupikia. Tunalifahamu hilo na tumeliona na Serikali imeanza jitihada za kuanza kupunguza jambo hili.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa kuanzia kwa namna ambayo imeonekana ni rahisi zaidi kuliko nishati ya gesi ya asili, ni kuwezesha wananchi kupata mitungi ya gesi ya viwandani kwa kuanza kupikia, na ninyi Waheshimiwa Wabunge ni mashahidi kwenye eneo hilo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka huu wa fedha ilitengwa mitungu 70,000, tumetenga kwenye bajeti inayokuja mitungi takribani 200,000 ili angalau tutoe mtaji wa mwananchi kuweza kupata kianzio cha kupata gesi halafu baada ya hapo sasa ataanza kununua na kuelekea kwenye kutumia gesi hii.

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunaboresha na kuona namna tunavyoweza kupunguza gharama za hii mitungi ya gesi ili wananchi walio wengi waweze kui-afford kwenye maeneo yao, Serikali inaweka ruzuku lakini tutaangalia namna nyingine ya kuweza kupunguza gharama hizi ili kila mwananchi aweze kutumia gesi safi ya kupikia.