Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Energy and Minerals Wizara ya Nishat 687 2023-06-21

Name

Prof. Patrick Alois Ndakidemi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Moshi Vijijini

Primary Question

MHE. PROF. PATRICK A. NDAKIDEMI aliuliza: -

Je, kuna mpango gani wa kupeleka nishati ya gesi asilia katika vijiji vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro ili kupunguza matumizi ya kuni?

Name

Stephen Lujwahuka Byabato

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Bukoba Mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA NISHATI alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Nishati, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Prof. Patrick Alois Ndakidemi, Mbunge wa Moshi Vijijini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, gesi asilia inaweza kusafirishwa kwa njia ya mabomba au kwa njia ya mitungi/tanki inayobebwa na malori/treni/meli ambapo gesi asilia inakuwa katika hali ya gesi iliyogandamizwa (Compressed Natural Gas – CNG) ama kimiminika (Liquefied Natural Gas – LNG). Hadi sasa, gesi asilia inachimbwa Mtwara na hivyo maeneo yaliyounganishwa na kuweza kutumia nishati ya gesi asilia ni yale yanayopitiwa na miundombinu ya mabomba ya kusafirishia gesi ambayo ni Mikoa wa Mtwara, Lindi, Pwani na Dar es Salaam.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Mradi wa Bomba la Kusafirisha Gesi Asilia kwenda Mombasa Nchini Kenya kupitia Mkoani Tanga, ni moja ya miradi inayotoa fursa ya kuunganisha Mikoa ya Kaskazini na gesi asilia ikiwemo Kilimanjaro kwa kuweka toleo katika eneo la Segera (Tanga). Mradi huu wa bomba bado unafanyiwa kazi Serikalini, utakapokamilika gesi asilia itaweza kufikishwa Mkoani Kilimanjaro, vikiwemo vijiji vinavyozunguka Mlima Kilimanjaro na katika maeneo mengine mkoani humo na mikoa ya jirani, nakushukuru.