Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Sophia Hebron Mwakagenda

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutafuta masoko ya mazao ya kilimo?

Supplementary Question 1

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza kwa niaba ya Mheshimiwa Stella Fiyao. Mji wa Tunduma ni mji ambao unavuna sana mahindi, na uko mpakani na nchi ya Zambia: Ni lini Serikali itawekeza pale kuhakikisha wakulima wale hawauzi kwa hasara ndani, wapeleke hata nje kwa sababu wao wako karibu na nchi ya Zambia?

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili. Zao la kokoa ni zao ambalo hapa Tanzania ni la pili kwa Afrika kwa ubora; na inasemekana zao hili linanunuliwa sana katika nchi ya uingereza: Ni lini mtamsaidia mkulima wa Kyela aweze kuuza zao la kokoa kwa bei nzuri ambayo yeye kama mkulima atanufaika kuliko madalali wa katikati wanaonufaika? (Makofi)

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu maswali ya Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli mpaka wa Tunduma ni kati ya mipaka ambayo imekuwa ikitumika sana kusafirisha mazao. Nataka tu nimwondoe hofu Mheshimiwa Mbunge kwamba, hivi sasa tunawekeza nguvu kubwa kuhakikisha tunawasaidia wakulima wetu ili mwisho wa siku waweze kunufaika na mazao yao na hasa katika utaratibu wa kurasimisha biashara ya mazao na urahisi wa usafirishaji mazao ili mkulima aweze kunufaika na mazao yake ikiwemo katika mpaka huu wa Tunduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, la pili la kuhusu kokoa. Ni kweli katika eneo la kokoa tunafanya vizuri, lakini mkulima pia ana haki ya kupata bei nzuri kutokana na ushindani wa kimasoko uliopo. Kama Serikali tutahakikisha kwamba tunaweka miundombinu rafiki ili kuwaruhusu wakulima wetu kutafuta masoko makubwa nje ya nchi ambayo yatawasaidia pia kupata bei ya uhakika na hasa katika kilimo hai cha kokoa ambacho bei yake imekuwa ni kubwa sana kimataifa.

Name

Daniel Baran Sillo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Babati Vijijini

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutafuta masoko ya mazao ya kilimo?

Supplementary Question 2

MHE. DANIEL B. SILLO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi niweze kuuliza swali moja la nyongeza. Wananchi wa Babati Vijijini wanatumia sana zao la mbaazi kama zao lao la biashara: Ni nini mkakati wa Serikali wa kutafuta soko la zao hili la mbaazi kwa ajili ya manufaa ya kiuchumi ya wananchi wa Babati Vijijini?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, tumeendelea kutafuta soko la uhakika la mbaazi na hasa kwa kuishirikisha Serikali ya India, ikiwa ni mmoja kati ya wanunuzi wakubwa. Wiki moja iliyopita, tulimtuma Naibu Katibu Mkuu wetu wa Wizara ya Kilimo, kwenda India kwa ajili ya kufuatilia yale makubaliano ya awali yaliyokuwepo ya soko la mbaazi na majadiliano yanakwenda vizuri ili tuweze kuwahakikishia wakulima wetu masoko ya uhakika, hasa ya mbaazi ambapo India wamekuwa wanunuzi wakubwa.

Name

George Ranwell Mwenisongole

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbozi

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutafuta masoko ya mazao ya kilimo?

Supplementary Question 3

MHE. GEORGE R. MWENISONGOLE: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, hivi karibuni Serikali imeweka zuio la kuu za mahindi nje ya nchi. Hali hiyo imesababisha bei ya mahindi kushuka. Kwa mfano, kwenye Jimbo langu la Mbozi debe sasa hivi ni shilingi 8,000 na bei inazidi kushuka; nini kauli ya Serikali ili kuwaokoa hawa wakulima ambao kwa sasa wamevunjika moyo na kuporomoka kwa hii bei?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, moja kati ya changamoto kubwa ambayo tunaipata katika biashara ya mazao ni uholela. Serikali ilichokifanya siyo kuzuia moja kwa moja. Imetoa mwongozo na kuweka utaratibu wa namna ya kufanya biashara ya mazao nchini Tanzania ambapo tumeelekeza kwamba, hivi sasa kila mfanyabiashara wa mazao, ahakikishe kwanza kabisa anapata Business License; pili, awe ana TIN; na tatu, kabla hajaenda mpakani kusafirisha mazao, ahakikishe kwamba ameshapata kibali cha kusafirisha mazao nje ya nchi (Export Permit).

Mheshimiwa Mwenyekiti, lengo la kufanya hivi ni kuweka takwimu sawa, kwa sababu kumekuwepo na wafanyabiashara ambao wanakwenda mashambani moja kwa moja kwa wakulima kwenda kununua mazao na hivyo Serikali kupoteza mapato mengi sana. Serikali ipo kwa ajili ya kuwalinda wakulima na kuhakikisha kwamba wakulima wanapata bei bora tukishawasimamia, kwa sababu ndiyo azma ya Mheshimiwa Rais kuhakikisha kwamba mkulima ananufaika na kilimo chake. (Makofi)

Name

Yustina Arcadius Rahhi

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutafuta masoko ya mazao ya kilimo?

Supplementary Question 4

MHE. YUSTINA A. RAHHI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Je, Serikali ina mpango gani wa kuzuia uuzaji wa mazao ghafi nje ya nchi, badala yake yaongezwe thamani kwa kusindikwa?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, anachokisema Mheshimiwa Mbunge ni sahihi na ndiyo mkakati wa Serikali. Hivi sasa tunajielekeza katika kuongeza thamani ya mazao yanayozalishwa nchini badala ya kuyapeleka ghafi nje ya nchi. Kwa mfano, katika eneo la zao la korosho hivi sasa tunaweka mkakati mkubwa kuhakikisha kwamba, zaidi ya asilimia 60 ya korosho yetu ifikapo mwaka 2025 iwe inabanguliwa hapa ndani na kuongezewa thamani. Hivi sasa tumeshaandaa eneo la Nanyamba kwa ajili ya ujenzi wa kiwanda kikubwa cha ubanguaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, vilevile katika maeneo mengine ikiwemo parachichi na mazao mengine pia, mkakati ni huo huo wa kuhakikisha kwamba tunaweka miundombinu rafiki kwa kushirikiana na Wizara ya Uwekezaji, Viwanda na Biashara ili tuwe tuna mnyororo mzima wa kuongeza thamani ya mazao yetu ya kilimo na mwisho wa siku kuliongezea Taifa mapato kupitia mazao haya.

Name

Asha Abdullah Juma

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:- Je, Serikali ina mkakati gani wa kutafuta masoko ya mazao ya kilimo?

Supplementary Question 5

MHE. ASHA ABDULLAH JUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa nafasi. Liko soko kubwa sana la mazao ya kilimohai, kwa mfano pamba yetu ya Tanzania iko namba tatu: Je, ni lini Serikali itaweka angalau kitengo mahususi cha kushughulikia kilimohai katika Wizara ya Kilimo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni kweli, mazao mengi ya kilimohai yana soko kubwa na yana uhakika sana wa masoko nje ya mipaka ya Tanzania. Kama Serikali, tumekuwa ni sehemu ya washiriki katika kuhakikisha kwamba tunafanikisha wakulima wetu kuweza kuyafikia masoko hayo makubwa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ndani ya Wizara ya Kilimo pia tunaweka utaratibu mzuri wa kuhakikisha kwamba tunashirikiana na wadau wakubwa wa kilimohai kwa kuweka kitengo maalum ambacho tutakuwa tunashirikiananao ili mwisho wa siku tufanye kazi kwa pamoja, maana wadau wakubwa wa kilimohai ni taasisi nyingi za binafsi ambazo zimekuwa zina mchango mkubwa. Nasi kama Serikali lazima tuhakikishe pia tunashirikiananao. Kwa hiyo, tunao watu ambao ni focal person katika Wizara ya Kilimo. Tutaendelea kuwaimarisha ili wafanye kazi kwa pamoja na sekta binafsi kwenye kilimohai.