Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Livestock , Fisheries, Agriculture, Food Security and Cooperatives Wizara ya Kilimo 688 2023-06-21

Name

Stella Simon Fiyao

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. SOPHIA H. MWAKAGENDA K.n.y. MHE. STELLA S. FIYAO aliuliza:-

Je, Serikali ina mkakati gani wa kutafuta masoko ya mazao ya kilimo?

Name

Anthony Peter Mavunde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Dodoma mjini

Answer

NAIBU WAZIRI WA KILIMO alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Kilimo, napenda kujibu swali la Mheshimiwa Stella Simon Fiyao, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa mwaka 2023/2024, Serikali kupitia Wizara ya Kilimo itaendelea kuimarisha upatikanaji wa masoko ya mazao ya kilimo ndani na nje ya nchi kwa kujenga masoko ya kimkakati mipakani, ujenzi wa vituo vya masoko na kuboresha miundombinu ya maabara za TPHPA ili ziweze kupata ithibati itakayowezesha kufanya uchunguzi na kutoa vyeti vya ubora vinavyokubalika Kimataifa, kuongeza tija na kupunguza gharama za uzalishaji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, aidha, Serikali inaendelea na majadiliano na nchi mbalimbali na kufungua masoko ya mazao katika nchi hizo. Hadi sasa tumefanikiwa kufungua soko la korosho nchini Marekani, soko la parachichi China, India na Afrika Kusini na tunaendelea kuhudumia masoko ya nafaka katika nchi mbalimbali za Afrika.