Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikai itajenga kwa kiwango cha lami km 76 za barabara ya Karatu – Mbulu kwa kuwa usanifu wake ulifanyika 2021/2022?

Supplementary Question 1

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru. Hivi sasa kampuni ya Kichina inatekeleza ujenzi wa barabara ya lami kutoka Mbulu kwenda Garbabi kilometa 25, lakini barabara hiyo kwa jiografia ya milima inahama kwenda nje ya mita 22.5 kutoka katikati ya Barabara: Je, Serikali haioni kuwa ni wakati muafaka wa kwenda kuwaelimisha wananchi ili tujue wanaofidiwa na wasiofidiwa ndani ya corridor hiyo ya barabara? (Makofi)

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Zacharia Paul Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kama ulivyo utaratibu kwamba pale ambapo tunajenga barabara tunatumia sheria za barabara na hasa kwenye kutoa fidia. Kwa wananchi ambao wako ndani ya mita 22.5 kutoka katikati ya barabara kwa pande zote wanakuwa wako kwenye hifadhi, lakini wale ambao wako mita 7.5 kwa pande zote ambazo zimeongezeka, barabara inakuwa imewafuata, na hao kwa kweli wanatakiwa wafanyiwe tathmini, waainishwe na walipwe fidia.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, nina hakika kama hivyo ndivyo, Mheshimiwa Mbunge suala hilo litafanyika kwa hao wananchi wa Mbulu hadi Garbabi, ahsante. (Makofi)

Name

Samweli Xaday Hhayuma

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Hanang'

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikai itajenga kwa kiwango cha lami km 76 za barabara ya Karatu – Mbulu kwa kuwa usanifu wake ulifanyika 2021/2022?

Supplementary Question 2

MHE. SAMWELI X. HHAYUMA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Naomba kufahamu kwenye mikataba iliyosainiwa, barabara ya Hydom – Mogitu yenye urefu wa kilometa 68, ipo? Ahsante sana.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Haydom – Mogitu ilikuwa ni sehemu ya barabara ya Serengeti Southern Road wakati wa design ya awali, lakini katika mpango huu wa EPC + F barabara hii kwa sasa tunaifanyia usanifu, maana ilikuwa imefanyiwa usanifu wa awali, sasa tumeiingiza tuifanyie usanifu ili tutakapokamilisha hiyo barabara ambayo ni ya EPC + F tuweze kuijenga hiyo pia kwa sababu ndiyo inayounganisha barabara ya Hydom kwenda Sibiti na barabara ya Singida kwenda Babati, ahsante.

Name

Dennis Lazaro Londo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mikumi

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikai itajenga kwa kiwango cha lami km 76 za barabara ya Karatu – Mbulu kwa kuwa usanifu wake ulifanyika 2021/2022?

Supplementary Question 3

MHE. DENNIS L. LONDO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali la nyongeza. Barabara ya kutoka Dumila kwenda Kilosa, kutoka Kilosa kwenda Mikumi kupitia Masanze – Zombo – Ulaya na Muhenda mpaka Mikumi ni uti wa mgongo kwa uchumi wa Mkoa wa Morogoro: Nini Kauli ya Serikali kuhusiana na hali ya barabara hii?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Dennis Londo, Mbunge wa Mikumi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, tunakubaliana na Mheshimiwa Londo kwamba, kwa kweli hiyo ni barabara muhimu sana na hasa tutakapokamilisha hii barabara ya kutoka Lumecha – Malinyi – Kidatu hadi Mikumi. Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba, kwa sababu ya umuhimu wake, katika bajeti inayokuja tumeitengea fedha ili kuendelea kuijenga kwa kiwango cha lami ili kuunganisha Kilosa na Mikumi kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikai itajenga kwa kiwango cha lami km 76 za barabara ya Karatu – Mbulu kwa kuwa usanifu wake ulifanyika 2021/2022?

Supplementary Question 4

MHE. BUPE N. MWAKANG’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ni lini barabara ya Chombe – Kaoze – Igonda mpaka Ilemba itajengwa? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Bupe Mwakang’ata, Mbunge wa Viti Maalum, Rukwa, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kitu cha kwanza ni kuifanyia usanifu wa kina hiyo barabara halafu baada ya hapo Serikali itajua gharama halisi ya kuijenga hiyo barabara na ndiyo sasa tutaiingiza kwenye mpango wa kuijenga kwa kiwango cha lami, ahsante.

Name

Francis Leonard Mtega

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbarali

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikai itajenga kwa kiwango cha lami km 76 za barabara ya Karatu – Mbulu kwa kuwa usanifu wake ulifanyika 2021/2022?

Supplementary Question 5

MHE. FRANCIS L. MTEGA: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru sana kwa kuniona. Barabara ya Igawa – Kinyanambo – Mafinga huko imefanyiwa upembuzi yakinifu kwa muda mrefu na iko kwenye Ilani ya Chama cha Mapinduzi pia: Je, ni lini Serikali itaanza ujenzi kwa kiwango cha lami? Ahsante.

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Mbunge, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara ya Igawa – Kinyanambo ipo kwenye ilani na kwa kweli, inatakiwa ijengwe kwa kiwango cha lami hasa tukizingatia umuhimu wa barabara hii inayopita maeneo yanayozalisha sana hasa mpunga. Serikali inaendelea kutafuta fedha kuhakikisha kwamba barabara hii inajengwa kwa kiwango cha lami.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa sasa mpango uliopo ni kuhakikisha kwamba inafanyiwa ukarabati iweze kupitika kwa kipindi chote cha mwaka. Mheshimiwa Mbunge atakubaliana nami kwamba Serikali imeendelea kujitahidi sana kuhakikisha barabara hii inafanyiwa matengenezo mara kwa mara na kupitika kwa muda wote wa mwaka, ahsante.

Name

Daniel Awack Tlemai

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Karatu

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: - Je, ni lini Serikai itajenga kwa kiwango cha lami km 76 za barabara ya Karatu – Mbulu kwa kuwa usanifu wake ulifanyika 2021/2022?

Supplementary Question 6

MHE. DANIEL A. TLEMAI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Je, ni lini barabara ya Oldiani – Mang’ola – Matala – Lalago itajengwa kwa kiwango cha lami na kuwa ni barabara inayounganisha Mkoa wa Arusha na Mkoa wa Simiyu? Ni Sera ya Wizara ya Ujenzi kuunganisha Mkoa kwa Mkoa. Ni lini ujenzi wake utaanza?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu swali la nyongeza la Mheshimiwa Awack, Mbunge wa Karatu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, barabara aliyotaja ni kweli, ni barabara kuu, lakini mpango wa Serikali kwa sasa ni kutafuta fedha kwanza kuijenga kutoka Oldiani mpaka Mang’ola kwenye eneo ambalo wanazalisha sana zao la vitunguu. Kadri tutakavyopata fedha, basi tutaendelea kutoka Mang’ola hadi Sibiti kwa kiwango cha lami, lakini kwa sasa Serikali tunafikiria kuijenga kwa kiwango cha lami Oldiani Junction mpaka Mang’ola, ahsante.