Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Works and Transport Wizara ya Ujenzi na Uchukuzi 685 2023-06-21

Name

Issaay Zacharia Paulo

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mbulu Mjini

Primary Question

MHE. ZACHARIA P. ISSAAY aliuliza: -

Je, ni lini Serikai itajenga kwa kiwango cha lami km 76 za barabara ya Karatu – Mbulu kwa kuwa usanifu wake ulifanyika 2021/2022?

Name

Eng. Godfrey Msongwe Kasekenya

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ileje

Answer

NAIBU WAZIRI WA UJENZI (MHE. ENG. GODFREY K. MSONGWE) alijibu: -

Mheshimiwa Spika, kwa niaba ya Waziri wa Ujenzi na Uchukuzi, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Zacharia Paulo Issaay, Mbunge wa Mbulu Mjini, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Spika, Serikali ipo kwenye maandalizi ya kujenga kwa kiwango cha lami kwa utaratibu wa EPC+F (Engineering, Procurement, Construction plus Finance). Barabara ya Karatu – Mbulu – Haydom – Sibiti – Lalago – Maswa (km 389) ambapo barabara ya Karatu – Mbulu (km 76) ni sehemu ya barabara hii. Hadi sasa Mkandarasi amepatikana na mkataba wa kuanza ujenzi umesainiwa tarehe 16 Juni, 2023.