Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Afya katika Kata za Mji wa Tarime kwa kuwa kuna Kituo kimoja tu cha Afya Nkende?

Supplementary Question 1

MHE. ESTHER N. MATIKO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nakushukuru.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Kata za pembezoni katika Halmashauri wa Mji wa Tarime ni pamoja ya Kata ya Nyandoto na Kata ya Kenyamanyori. Wananchi wa Kata ya Kenyamanyori walishaanza kujenga kituo cha afya kwa nguvu zao wenyewe na baadhi ya maboma yamekamilika kuanzia mwaka 2019, Serikali iliahidi kwamba itapeleka fedha kuhakikisha kwamba kituo kile kinakamilika maana wako nje ya mji.

Mheshimiwa Mwenyekiti, ninataka kujua commitment ya Serikali sasa ni lini watapeleka fedha ili waweze kukamilisha Kituo cha Afya cha Kenyamanyori kupunguza adha ambayo wanaipata kuja kupata huduma kwenye hospitali ya Mji wa Tarime?

Swali langu la pili, katika Kata za Susuni na Mwema katika Halmashauri ya Wilaya ya Tarime ni Kata ambazo zipo pembezoni na wanapata huduma sana sana wakienda kituo cha Sirari kule au hospitali ya Nyamwaga lakini wengi wanakuja Hospitali ya Halmashauri ya Mji wa Tarime. Ninataka kujua ni lini Serikali itahakikisha kwamba Kata hii ya Susuni na Kata ya Mwema na zenyewe zinapata vituo vya afya ili kuweza kupunguza adha ya wananchi wale kusafiri mwendo mrefu kutafuta huduma ya afya? (Makofi)

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEORGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, naomba kujibu maswali mawili ya Mheshimiwa Esther Matiko.

Mheshimiwa Mwenyekiti, hili la kwanza la lini fedha itakwenda kwa ajili ya kukamilisha ujenzi wa Kituo cha Afya Kenyamanyori.

Kwanza nichukue nafasi hii kuwapongeza wananchi wa Kata ya Kenyamanyori kwa kuweza kuanza kwa jitihada zao wenyewe ujenzi wa kituo chao cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kuhusu suala la fedha tutatuma timu pale ya Mganga Mkuu wa Mkoa kwa ajiili ya kufanya tathmini ya ujenzi ule ambao umefanyika na kuona kama vinakidhi mahitaji yanayotakiwa ili kusajili kituo cha afya kipya katika Kata ile na baada ya tathmini ile wataiwasilisha Ofisi ya Rais – TAMISEMI, kwa ajili ya kuhakikisha kwamba tunatafuta fedha ya kupeleka kuunga mkono juhudi hizi za wananchi wa Kenyamanyori kumalizia kituo kile cha afya.

Mheshimiwa Mwenyekiti, nikienda kwenye swali lake la pili la Kata ya Susuni na Mwema zilizoko kule Halmashauri ya Wilaya ya Tarime. Tutafanya vivyo hivyo kama ambavyo nimemjibu swali lake la kwanza la kuhakikisha timu ile inapoenda Tarime Mji, wafike vilevile kwenye Halmashauri ya Wilaya Tarime na kufanya tathmini katika Kata hizi mbili ambazo amezitaja Mheshimiwa Matiko na kisha walete taarifa Ofisi ya Rais - TAMISEMI ili tuweke katika mipango yetu ya kutafuta fedha na kuhakikisha kwamba tunapeleka kwa ajili ya kujenga vituo hivi vya afya.

Name

Regina Ndege Qwaray

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Afya katika Kata za Mji wa Tarime kwa kuwa kuna Kituo kimoja tu cha Afya Nkende?

Supplementary Question 2

MHE. REGINA N. QWARAY: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kuniona. Wananchi wa Tarafa ya Msitu wa Tembo wamekuwa na changamoto kubwa ya kufuata huduma za afya kwa umbali mrefu. Je, ni lini sasa Serikali itawajengea wananchi hao kituo cha afya?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEORGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itajenga vituo hivi vya afya ambavyo ametaja Mheshimiwa Regina Ndege, katika mwaka wa fedha unaofuata tutaangalia kama kuna fedha iliyotengwa kujenga kama hakuna tutatenga katika mwaka wa fedha wa 2024/2025.

Name

Jeremiah Mrimi Amsabi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Serengeti

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: - Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Afya katika Kata za Mji wa Tarime kwa kuwa kuna Kituo kimoja tu cha Afya Nkende?

Supplementary Question 3

MHE. JEREMIAH A. MRIMI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Ni lini, sasa Serikali itatusaidia fedha ya nyongeza kwa ajili ya ukamilishaji ujenzi kituo cha afya Machochwe kama tulivyoomba? Ahsante.

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEORGRATIUS J. NDEJEMBI): Mheshimiwa Mwenyekiti, hili Mheshimiwa Mrimi amekuwa akilifuatilia sana kuhusu fedha hizi za Kituo cha Afya Machochwe na tutaendelea kama ambavyo nimeonana naye ofisini mara kadhaa kumueleza kwamba, tunaangalia namna gani bora tutapata fedha ya kumalizia kituo hiki cha afya na pale ambapo Serikali itapata fedha basi tutapeleka katika kituo hiki cha afya cha Machochwe ili kiweze kukamilika. (Makofi)