Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 52 Regional Administration and Local Government Authorities Ofisi ya Rais TAMISEMI. 682 2023-06-21

Name

Esther Nicholus Matiko

Sex

Female

Party

CHADEMA

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. ESTHER N. MATIKO aliuliza: -

Je, lini Serikali itajenga Vituo vya Afya katika Kata za Mji wa Tarime kwa kuwa kuna Kituo kimoja tu cha Afya Nkende?

Name

Deogratius John Ndejembi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Chamwino

Answer

NAIBU WAZIRI, OFISI YA RAIS, TAWALA ZA MIKOA NA SERIKALI ZA MITAA (MHE. DEORGRATIUS J. NDEJEMBI) alijibu: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Waziri wa Nchi, Ofisi ya Rais - TAMISEMI, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Esther Nicholas Matiko, Mbunge wa Viti Maalum, kama ifuatavyo: -

Mheshimiwa Mwenyekiti, katika mwaka wa fedha wa 2021/2022, Serikali ilitenga shilingi milioni 500 kwa ajili ya ujenzi wa Kituo cha Afya cha kimkakati cha Ketare katika Halmashauri ya Mji wa Tarime kwa kujenga jengo la kuhudumia wagonjwa wa nje (OPD), Maabara, Jengo la Wazazi, Jengo la upasuaji na Jengo la Kufulia na ujenzi umekamilika na kituo kimeanza kutoa huduma.

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali itaendelea kutenga bajeti kwa ajili ya ujenzi wa vituo vya Afya katika Kata za kimkakati kote nchini, zikiwemo Kata za Mji wa Tarime.