Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka wa Pori la Usumbwa Forest Reserve na Hifadhi ya Pori la Kigosi Moyowosi - Ushetu?

Supplementary Question 1

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa kuwa wananchi hawa walizoea kufanya shughuli zao za kibinadamu wakati pori hili halijaingizwa kwenye Hifadhi ya Taifa TANAPA; tathmini hii sasa itakamilika lini, kwa sababu nimekuwa nikiahidiwa kila mara, ili wananchi waweze kumegewa eneo lao waweze kuendelea kufanya shughuli za kibinadamu hasa katika Kata ya Ulewe, Kata ya Ubagwe na Kata ya Idahina? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali langu la pili. Kamishna wa Ardhi katika Mkoa wa Shinyanga kakamilisha tathmini katika Pori la Ubagwe Forest Reserve katika mpaka wa Kaliua ambapo sasa inahitajika gharama ya kwenda kuhakikisha wanaweka mipaka ili kuondoa mgogoro pia uliopo katika eneo hili. Serikali lini sasa itapeleka fedha ili mipaka hii iweze kuwekwa? (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, kwanza nampongeza sana Mheshimiwa Mbunge. Ushetu nilifika na nilizungumza na wananchi wa pale na tuliwaahidi kwamba migogoro hii tunaishughulikia. Kwenye upande wa eneo hili ambalo wananchi wanadai, nataka tu niwaambie wananchi wa Ushetu kwamba wakati Usumbwa Forest Reserve ikiwa kwenye hadhi ya msitu kwa maana ya Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania wanalisimamia, pori hili lilikuwa linaruhusu shughuli za kibinadamu na hadhi yake tulikuwa tunaruhusu ufugaji wa nyuki na wananchi walikuwa wanarina asali katika maeneo hayo. Ndiyo maana leo hii wananchi wanaona ni kama walinyang’anywa, lakini hadhi ya pori ilibadilishwa kutoka kwenye forest reserve, ikapanda kuwa National Park. National Park inazuia shughuli za kibinadamu ndani yake.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa hiyo, kwa sasa hivi tunaangalia utaratibu wa kuyashusha hadhi baadhi ya maeneo ili wananchi waendelee kuanza kupata faida ya uhifadhi, na pia waendelee kufuga nyuki kwa ajili ya kurina asali. Kwa hiyo, niwatoe wasiwasi wananchi wa Ushetu, suala hili tunalishughulikia na Mbunge wao amekuwa akiliulizia mara kwa mara. Kwa hiyo, muda siyo mrefu tunatarajia kuleta azimio Bungeni. Nadhani kuna baadhi ya maeneo yatashushwa hadhi na wananchi wataanza kufaidika na urinaji wa asali. Kwenye suala hili la lini tutaweka mipaka, kwa kuwa tathmini tayari imeshakamilika ni wakati wowote tu kuanzia sasa. Kwa kuwa ni jukumu letu Wizara ya Maliasili na Utalii kuweka mipaka, basi tutaendelea kuainisha mipaka halisi, ahsante.

Name

Bupe Nelson Mwakang'ata

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:- Je, lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka wa Pori la Usumbwa Forest Reserve na Hifadhi ya Pori la Kigosi Moyowosi - Ushetu?

Supplementary Question 2

MHE. BUPE N. MWAKANGA’ATA: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante kwa kunipa nafasi ya kuuliza swali dogo la nyongeza. Kwanza kabisa nichukue nafasi hii kuipongeza Serikali kwa kumaliza mgogoro wa uwanda wa game reserve Mkoani Rukwa lakini nina swali dogo la nyongeza. Je, ni lini sasa Serikali itapunguza tozo za token ambazo wananchi wanalipa wanapoingia kuvuna na kutoka? Ni lini Serikali itapunguza hizo tozo? Ahsante. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, niwashukuru kwa sababu mgogoro huu umeisha. Kwenye suala la token sasa tutaenda uwandani kuangalia ni jinsi gani tukae na wadau ili tuone bei ambayo ni nzuri zaidi kwa wao na kwetu sisi twende sambamba na mahitaji ya wananchi, ahsante.