Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 680 2023-06-20

Name

Emmanuel Peter Cherehani

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Ushetu

Primary Question

MHE. EMMANUEL P. CHEREHANI aliuliza:-

Je, lini Serikali itamaliza mgogoro wa mpaka wa Pori la Usumbwa Forest Reserve na Hifadhi ya Pori la Kigosi Moyowosi - Ushetu?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Emmanuel Peter Cherehani, Mbunge wa Jimbo la Ushetu, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Pori la Usumbwa Forest Reserve ambalo kwa sasa ni hifadhi ya Taifa Kigosi haina mgogoro wowote wa mpaka na wananchi wa Ushetu. Kwa sasa kilichopo ni wananchi wa Ushetu waliwasilisha maombi ya kumegewa eneo, ambapo Serikali inaendelea na tathmini na pindi litakapokamilika, wananchi watajulishwa. (Makofi)