Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MAGUNGUSI aliuliza:- Je, Serikali haioni haja ya kuwatumia vijana waliopata mafunzo ya JKT kutumikia Jeshi la Uhifadhi kwa mkataba wa muda mfupi?

Supplementary Question 1

MHE. ANTIPAS Z. MGUNGUSI: Mheshimiwa Mwenyekiti, nashukuru. Nina maswali mawili ya nyongeza. Pamoja na nia njema ya kutumia SUMA JKT kwa ajili ya kuongeza nguvu kwenye jeshi la uhifadhi na ninajua malipo yao kidogo ni makubwa ukilinganisha na watu ambao wana- volunteer; je, Wizara sasa haioni haja ya kutumia vijana ambao wapo kambini au mtaani lakini hawapo SUMA JKT? (Makofi)

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili, vijana wetu waliomaliza elimu ya wanyapori kwa maana ya Mweka, Pasiansi na Olmotonyi ambao wapo mtaani kwa sasa, Wizara haioni haja ya kuwapa mkataba wa muda mfupi na kuwalipa posho? Ahsante. (Makofi)

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII: Mheshimiwa Mwenyekiti, nimtoe wasiwasi Mheshimiwa Mbunge, pamoja na kuwa ni Mhifadhi Mkuu na amekuwa akitumikia Serikali kwa miaka ya nyuma akiwa Mhifadhi, lakini kwa sasa hivi Serikali ilishaanza kuwatumia hao vijana wa JKT. Hivi ninavyoongea, tayari taasisi zinaajiri. Pia tumeanzisha makampuni ambayo vijana ambao hawajapata ajira za Serikali wanaingizwa kule na taasisi zetu zinachukua vijana kutoka kwenye makampuni hayo. Kwa hiyo, utaratibu huu tunaendelea nao. Wale waliopo kambini tunawatumia pia kwa ajili ya doria za muda mfupi pale ambapo inapojitokeza changamoto za wanyama wakali na waharibifu.