Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Primary Question

Term Session Sitting Sector Ministry Qn No Date
2020-2025 Session 11 Sitting 51 Natural Resources and Tourism Wizara ya Maliasili na Utalii 678 2023-06-20

Name

Antipas Zeno Mgungusi

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Malinyi

Primary Question

MHE. ANTIPAS Z. MAGUNGUSI aliuliza:-

Je, Serikali haioni haja ya kuwatumia vijana waliopata mafunzo ya JKT kutumikia Jeshi la Uhifadhi kwa mkataba wa muda mfupi?

Name

Mary Francis Masanja

Sex

Female

Party

CCM

Constituent

Special Seats

Answer

NAIBU WAZIRI WA MALIASILI NA UTALII alijibu:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante. Kwa niaba ya Mheshimiwa Waziri wa Maliasili na Utalii, naomba kujibu swali la Mheshimiwa Antipas Zeno Magungusi, Mbunge wa Jimbo la Malinyi, kama ifuatavyo:-

Mheshimiwa Mwenyekiti, Serikali kupitia Jeshi la Uhifadhi wa Wanyamapori na Misitu imekuwa ikiajiri Askari wenye taaluma kuu tatu ambazo ni Askari waliohitimu Astashahada ya Wanyamapori, Astashahada ya Misitu na Askari waliohitimu Jeshi la Kujenga Taifa.

Mheshimiwa Mwenyekiti, kutokana na upungufu mkubwa wa watumishi hususan Askari, SUMA JKT wamekuwa wakiingia mikataba ambayo inawezesha vijana waliohitimu JKT kupata kazi za mikataba kwa shughuli mbalimbali za ulinzi wa maliasili (wanyamapori na misitu). Mfano, kwa sasa Wakala wa Huduma za Misitu Tanzania (TFS) wameingia mkataba na SUMA JKT kwa ajili ya kuongeza nguvu ya ulinzi wa misitu kwenye maeneo yenye upungufu mkubwa wa Askari.