Jamhuri ya Muungano ya Tanzania

Supplementary Questions

Name

Selemani Moshi Kakoso

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Mpanda Vijijini

Primary Question

MHE. MOSHI S. KAKOSO aliuliza:- Je ni lini Serikali itakamilisha ujenzi wa skimu za umwagiliaji za Karema na Kabage Mkoani Katavi?

Supplementary Question 1

MHE. MOSHI S. KAKOSO: Mheshimiwa Mwenyekiti, nishukuru kunipa nafasi ya kuuliza maswali mawili ya nyongeza.

Kwa kuwa, mradi huu wa skimu ya umwagiliaji ya Karema umechukua muda mrefu zaidi ya miaka kumi na swali kama hili nimeliuliza hapa Bungeni zaidi ya mara tano.

Je, Serikali sasa ina mkakati gani wa kwenda kubomoa ile miundombinu ambayo waliiweka ambayo haiwasaidii wananchi na kabla ya kuweka mradi ule wananchi walikuwa wakinufaika wanapata mazao yao. Lini Serikali wataenda kubomoa ule mradi?

Swali la pili, kwa kuwa ndani ya miaka kumi wananchi wamekuwa wakilima wakipata hasara kwa sababu ya miundombinu iliyowekwa mibovu. Serikali ina mkakati gani wa kuwalipa fidia wakulima hao ambao wamelima kwa miaka kumi wakiteseka? (Makofi)

Name

David Ernest Silinde

Sex

Male

Party

CCM

Constituent

Tunduma

Answer

NAIBU WAZIRI WA MIFUGO NA UVUVI K.n.y. WAZIRI WA KILIMO: Mheshimiwa Mwenyekiti, ahsante sana. Kwanza ninampongeza Mheshimiwa Mbunge kwa kufuatilia kwa ukaribu juu ya ujenzi wa mradi wa Karema wa umwagiliaji, lakini nimuondoe shaka kwamba ndiyo maana ukiona katika jibu la msingi tumeandika hapa kwamba mradi huu wa Karema ambao sasa hivi uko katika hatua za mwisho za usanifu wa bwawa pamoja na miundombinu ya umwagiliaji na tumeahidi kabisa hapa kwamba utakamilika katika mwaka wa fedha 2022/2023.

Kwa hiyo, nimuondoe shaka kwa sababu Serikali imeona hiyo kero ya wananchi na katika mwaka wa fedha unaokuja litatekelezeka kama ambavyo Wizara ya kilimo imeahidi na itafanya hivyo.

Mheshimiwa Mwenyekiti, swali la pili kuhusu hasara ambayo wananchi wameipata kutokana na kushindwa kulima vizuri katika eneo lao, nimwambie tu kwamba ukweli ni kwamba hatuwezi kulipa fidia kwa hasara ambazo zilitokana na wao kulima eneo lile, lakini Serikali imekuwa ikizingatia umuhimu wa wakulima nchini na ndiyo maana umeona Serikali katika ku-boost kilimo ikawa imekuja na mradi wa kutoa ruzuku za pembejeo, yote hii ni kutaka kuwanufaisha wananchi ambao wanapata faida kutokana na ruzuku hizo. Kwa hiyo, tutaendelea kuboresha kilimo nchini ili kuhakikisha wananchi wetu wanaendelea kupata faida. Ahsante sana. (Makofi)